Wewe mleta mada ndio nakushangaa, tatizo lako umeishi kwa kukariri sasa umeona kitu tofauti unaona ni kosa, guu kwako ni ushamba, tembea maeneo tofauti uone mambo yanavyokwenda.
Suala la wahudhuriaji msibani kuwa wengi au wachache nalo kwangu halina maana, na zaidi hata hilo suala la kusema kwasababu walikuwa hawadhurii kanisani ndio maana wakakosa mchungaji sijui padre wa kuwazika nalo kwangu pia halina maana, hizo ni sheria za kanisa sio za Mungu, kama unaamini hizo sheria zina maana basi tuambie hapa Yesu alikuwa dhehebu gani?
Huyo mchungaji hawezi kumuondolea dhambi baba yake na rafikiyo hata kama akiendesha misa ya maziko, hilo walilofanya hao wachungaji sijui padre ni kuwahukumu hiyo familia ya rafiki yako wakati tumeambiwa tusihukumu tusije hukumiwa, hukumu ya haki iko mbinguni pekee.
Hao wachungaji wanajiona wako vizuri wakati nao siku ya mwisho wanaweza chomwa moto tu, kwani imeandikwa sio kila anaesema Bwana Bwana atauona ufalme wa Mungu, wachungaji/ mapadre kukataa kuzika ni siasa tu zimeingia makanisani, tumeona "wazito" wengi wanazikwa hata km walikuwa hawaendi makanisani.
Masuala ya kuzikwa na mchungaji, kuhudhuriwa mazishi yako na watu milioni mbili nk ni mbwembwe za ulimwenguni tu, haziisaidii chochote roho inayosubiri hukumu, tusidanganyike na vya ulimwengu huu.
Mwisho, huyo rafiki yako ana haki ya kumkataa huyo kaka yake kwasababu baba yake hakuwai kumwambia kama ana kaka, hilo sio kosa la binti ni kosa la mzazi baba, angempanga mapema huyo rafiki yenu hilo la kumkataa kaka yake lisingetokea.