Mambo ya ajabu niliyoshuhudia msibani

Mambo ya ajabu niliyoshuhudia msibani

Kuna chakujifunza hapa, malezi bora kwa watoto yanahusika
 
Oyaa ulilala msibani siku tatu, ukasafirisha mwili kisha ukazika. Huo muda ulitoa wapi wakati chuo masomo yanaendelea.
Mimi siwezi kaa siku tano bila kufika chuo, sanasana nikitoka Ijumaa usiku narudi Jumapili mchana.
Mfano ukipata msiba wa mtu wako wakaribu, pia hutaweza kukaa siku tano bila kufika chuo, we unaongea tu mzee, watu wanakaa hata week kutokana na changa moto na chuo masomo yanaenda kama kawaida mzee, hofu ya chuo tu hiyo mzee
 
Oyaa ulilala msibani siku tatu, ukasafirisha mwili kisha ukazika. Huo muda ulitoa wapi wakati chuo masomo yanaendelea.
Mimi siwezi kaa siku tano bila kufika chuo, sanasana nikitoka Ijumaa usiku narudi Jumapili mchana.
Watu tulikua hatuwendi wiki mbili na wala hatupo msibani wala wapi, tunangalia movie,series na games..sasa msiba ndio wala hatuwaz, ww msuli sana usipoingia lecture uwezi elewa, tulia mkuu
 
"siku ya pili" imejirudia mara 2.
Kuna "kesho","siku ya pili" halaf siku ya tatu.
Rekebisha hiyo story mkuu
 
Watu tulikua hatuwendi wiki mbili na wala hatupo msibani wala wapi, tunangalia movie,series na games..sasa msiba ndio wala hatuwaz, ww msuli sana usipoingia lecture uwezi elewa, tulia mkuu
Itakuwa umbebobea katika hizo games na movies ndio maana unaandika maneno ya hivi katika Kiswahili: "hatuwendi", "uwezi".
Kwanza kuhudhuria lectures sio kupiga msuli.

Anyway, roho nzuri ya kukaa msibani kwa masimango uku nikitumikishwa kazi kibabe kwa siku ngapi siiwezi, nina madhaifu sana.
 
Duh aibu kwlkwl ,mie nilihudhuria msiba wa haya madhehebu ya kiroho baadhi ya masharti mi kutokulia unapofiwa,marehemu ameenda kupumzika halafu na wewe utake usitake utakufa tu ndio yalikuwa madai yao kwnn usilie,basi ulikuwa msiba wa wameru wakavumilia sana sana vijisheria visivyoeleweka ikiwemo kutokutamka marehemu amefariki unatakiwa useme ametwaliwa,Mara gari wanaita punda,majina yao Mara waumini wanaitana kama kwa code unakuta MTU anaitwa Jiwe kuu,Upendo wa madhabahu Mara Adamu wa pili nk. Wameru wakatulia tuliii ikafika SAA ya mahubiri mchungaji akaiambia hadhira bila kupepesa macho hivi mnaolia mnalilia nn? Nashangaa SAA mkizini hamlii mnakuja kulia msiban' Duh Mimi binafsi nikajiuliza hivi haya ninayoyasikia kaongea kwl au? Mara kukazuka vurugu Weee wameru walisimama ulitokea ugomvi katikati ya ibada mchungaji ma waumini wake woote wakatolewa nje wao waumini walikuwa wamevaa mavazi meupe duhhh kilichoendelea msiniulize Ila marehemu alizikwa .ni kwl mkuu mambo haya na visanga kama hivi vipo.
Hahaa mkuu ni wasiloamu hao

Kwakweli wananishangaza
 
Mfano ukipata msiba wa mtu wako wakaribu, pia hutaweza kukaa siku tano bila kufika chuo, we unaongea tu mzee, watu wanakaa hata week kutokana na changa moto na chuo masomo yanaenda kama kawaida mzee, hofu ya chuo tu hiyo mzee
Nikitoka siku nyingi lazima niwe na jambo la msingi na linalonigua zaidi.

Mtu hata kwao kumbe hapajui wala wadogo zake na mama yake hawajui, huyo hawezi kuwa mtu wa karibu. Mtu kisa unamfahamu jina akifiwa haiwezi kuwa changamoto kwako, unless una maslahi nae. Wanafiwa watu kibao, utalala misiba mingapi.
 
Ndo ilivo; ukiacha kushirikiana na watu na kujiskia, nao pia wataacha kushirikiana nawe

Mtaani kulikua na wazee wawili.mmoja nadhani ni mchaga,ana hela kila kitu kuko kwake,watoto huwaoni nje ya ukuta hata wakicheza na majirani, wakienda shule wanafungiwa boarding wakirudi ndani..mke wake sasa sio social hata kipaimara haudhurii..misiba hata jirani hatua mbili hawaendi. Siku alivokufa mtaa mzima kila mtu yuko bize na shughuli zake.

Kuna wa pili nae ni mjita mwanajeshi aliwekeza mtaani.siku kafa nawauliza wakubwa si kuna msiba kule mbona hamuendi...wazee wapo tu kama hamna kitu.

Kuna mtu ananiambia yule mzee aliekufa alikua haudhurii msiba,yani hata kuja dakika moja akupe mkono wa pole kisha aondoke hawezi.unaweza kura msiba na yeye anapita hapo pembeni barabarani anaenda kazini.
 
Back
Top Bottom