Jogoo mbegu
JF-Expert Member
- Jun 28, 2023
- 824
- 3,406
Mambo ya kipekee ambayo katika maisha ya umasaini ni nadra sana kuyasikia au kuyaona, ili hali sehemu nyingine ni mambo ya kawaida kutoke katika jamii
Hutasikia wake wanagombania mume, ndio kwanza mke mkubwa humwambia mumewe aoe mke mwingine wasaidiane katika majukumu. Wake hawaoneani wivu, hawapigani wala kununiana
Neno yatima ni halipo, huwezi kuoneshwa mtoto/watoto yatima. Wazazi wakifariki watoto huendelea kwa ndugu husika, neno yatima ni nadra sana kulisikia
Wanawake kutoa mimba ni nadra sana kusikia, unaweza mtia mimba na usimuoe wala kulea, utakuwa umempa mtoto kama zawadi tu. Kama ilivyo hakuna neno yatima pia mtoto wa kambo ni hakuna
Wanawake kuvaa nusu uchi ni hakuna japo wana hijifunga mashuka yao unaweza hisi muda wowote atamwaga radhi upepo ukija uone paja au upapa, hapo utakesha sana zaidi utaambulia kuona upara kichwani tu.😂😂
Huwezi sikia mtu kajinyonga au kunywa sumu iwe kisa mapenzi, ugonjwa sugu au ugumu wa maisha
Huwezi sikia mambo ya ushoga.
Huwezi sikia kesi kwamba mwanamke kabakwa
Vilevile kuna mambo ambayo umasaini ni kawaida Sana Ila kwa jamii nyingine ni mshangao
Kutotumia vyoo na ni kawaida kukuta boma la zaidi ya watu hamsini bila choo hata cha kuegesha, wao hupendelea kwenda vichakani na makorongoni. Hata kama choo kipo ni hakitumiki.🤔🤔
Wanawake hawana haki za msingi wala hawana maamuzi yeyote mbele ya mwanaume, wakiitwa hata vikaoni wao ni wasikilizaji tu.
Swala la elimu wazazi huzaa watoto wengi, huchagua wa kwenda shule, machungani au wakuolewa mapema iwezekanavyo
Wanaume kuoa vibinti vidogo ambavyo wakati mwengine hata havijapevuka.
Wanaume kutofanya kazi za mikono kama kujenga, kufua, au kulima. Mwanaume yupo tayari aende na mkewe kibarua cha kulima, mke alime yeye amsimamie nyuma akimpigia story 😂😂
Supai bhookee😃
Hutasikia wake wanagombania mume, ndio kwanza mke mkubwa humwambia mumewe aoe mke mwingine wasaidiane katika majukumu. Wake hawaoneani wivu, hawapigani wala kununiana
Wanawake kutoa mimba ni nadra sana kusikia, unaweza mtia mimba na usimuoe wala kulea, utakuwa umempa mtoto kama zawadi tu. Kama ilivyo hakuna neno yatima pia mtoto wa kambo ni hakuna
Wanawake kuvaa nusu uchi ni hakuna japo wana hijifunga mashuka yao unaweza hisi muda wowote atamwaga radhi upepo ukija uone paja au upapa, hapo utakesha sana zaidi utaambulia kuona upara kichwani tu.😂😂
Huwezi sikia mtu kajinyonga au kunywa sumu iwe kisa mapenzi, ugonjwa sugu au ugumu wa maisha
Huwezi sikia mambo ya ushoga.
Huwezi sikia kesi kwamba mwanamke kabakwa
Vilevile kuna mambo ambayo umasaini ni kawaida Sana Ila kwa jamii nyingine ni mshangao
Kutotumia vyoo na ni kawaida kukuta boma la zaidi ya watu hamsini bila choo hata cha kuegesha, wao hupendelea kwenda vichakani na makorongoni. Hata kama choo kipo ni hakitumiki.🤔🤔
Wanawake hawana haki za msingi wala hawana maamuzi yeyote mbele ya mwanaume, wakiitwa hata vikaoni wao ni wasikilizaji tu.
Swala la elimu wazazi huzaa watoto wengi, huchagua wa kwenda shule, machungani au wakuolewa mapema iwezekanavyo
Wanaume kuoa vibinti vidogo ambavyo wakati mwengine hata havijapevuka.
Wanaume kutofanya kazi za mikono kama kujenga, kufua, au kulima. Mwanaume yupo tayari aende na mkewe kibarua cha kulima, mke alime yeye amsimamie nyuma akimpigia story 😂😂
Supai bhookee😃