mchawi wa kusini
JF-Expert Member
- Apr 18, 2018
- 805
- 810
Habari Ya Sabatho WanaJF Twende Na Mimi Katika Uzi Huu
TAFUTA MAISHA LAKINI PIA ISHI:
Hapa duniani kuna watu wengi ambao wanatafuta maisha ambayo kihuhalisia,tayari wanayo.Wanatafuta hayo maisha kiasi kwamba hawaishi kabisa,yaani wanaumia!
Baadhi yetu tunatafuta maisha kwa nguvu inafikia muda wa kuyapata maisha yanakuta huwezi kuishi tena. Huwezi kuyala,ndiyo umekwisha! Una gari zuri huwezi kuendesha; una nyumba nzuri ya ghorofa huwezi kupanda juu, unaumwa miguu; una mifugo ya kila aina huwezi kula nyama, huli sukari, huli chumvi, huli mafuta, hunywi soda, wakikuletea chakula chenye mafuta na chumvi nyingi unafoka sana,nini sasa?
Ebu kataa kujikataa! Tunapaswa kufanya jitihada kubwa za kutafuta maisha na kuyaishi hayo maisha.Kwa nini ujinyime saana eti hela zote zinakaa benki,haziguswi akigusa mtu unakufa kwa presha!
Kula vizuri na kulala pazuri ni sehemu ya maisha pia. Siyo mtu unalala njaa.Umefungua biashara lakini unalala dukani kulinda biashara mpaka asubuhi,huendi nyumbani,huoni mwenzio,huwaoni watoto,eti unatafuta PESA/MAISHA! Wakikuua?
Tafuta mlinzi, mlipe ili nawe upate muda wa kupumzika ili uchaji akili upate mawazo mapya ya kutafuta maisha.Utakuwa umemsaidia na huyo mlinzi umempa maisha!
Kukosa usingizi kunakufanya uonekane umerukwa na akili. Kumbe ni uchovu wa kutafta maisha,really?
Hata unapotafuta maisha ya wanao kumbuka kutafuta na maisha yako pia. Watoto wanabadilika. Usijisahau sana ukaishi kwenye kiatu cha mwanao ukasahau ya kwako!Huu ni ujinga tu kama ujinga mwingine!
Tumeona wazazi wengi wakijipa jukumu la kulaani kila anayewanyima kwa sababu tu watoto wao waliwaacha solemba. Ukimwacha mtoto ujue nawe utaachwa naye!
Mpende mtoto wako kama unavyojipenda mwenyewe. Siyo unashindwa hata kuvaa kiatu kizuri kwa sababu unasomesha. Ebu jaribu kalance bhana! Kujipenda siyo ubinafsi hata kidogo,kujipenda ni kujithamini na ndo mwanzo wa kuwapenda wengine,kwa sababu vitabu vya dini vinasema "mpende kama unavyojipenda".Hii inamaana wazi kwamba utampenda mtu mwingine kwenye levo ileile ya unavyojipenda.....
ZINGATIA....Hakuna binadamu atakayekupenda kuliko anavyojipenda,ni mbwembwe tu na uwongo!
Kuna watu hawajawahi kuishi tangu wazaliwe. Wao ni busy kutafuta maisha tu. Hawana muda wa kupumzika, hawana wikendi, hawana likizo, hawana muda wa kula,hawana usiku na hawana mchana,wao wanachakarika,alafu wakipata tu paaa,wanaondoka hawapo duniani!
KWA NINI?
Wanapata maisha, wanashindwa kuyafaidi, wameishaumizwa na mapambano ya kutafuta maisha. Wanaanza kutumia walivyochuma kutafuta afya!Wamepata pesa lakini afya imeondoka?
Ishi kabla ya kuchoka. Tafuna mifupa ungali una meno. Enjoy na familia yako iwezekanavyo,watakukumbuka endapo utakuwa umetangulia!
Yaani inashangaza,mwingine,hata akiumwa anaona heri akafie kazini kuliko kujipa muda wa kupumzika na kupona vizuri.
Toka out, kula vizuri, shushia na pepsi baridi, rudi nyumbani kwa mbwembwe, soma kitabu au sikiliza mziki mpaka usingizi ukupitie, asububi nenda katafute maisha.
Maisha ni uwiano wa kazi na bata. Kimoja kikizidi kingine kikapungua utapata shida. Hata kuulisha mwili tu bila kuilisha akili ni hatari kabisa kwa usalama wako.
Ushauri wa bure huu,acha au uchukue..
TAFUTA MAISHA LAKINI PIA ISHI:
Hapa duniani kuna watu wengi ambao wanatafuta maisha ambayo kihuhalisia,tayari wanayo.Wanatafuta hayo maisha kiasi kwamba hawaishi kabisa,yaani wanaumia!
Baadhi yetu tunatafuta maisha kwa nguvu inafikia muda wa kuyapata maisha yanakuta huwezi kuishi tena. Huwezi kuyala,ndiyo umekwisha! Una gari zuri huwezi kuendesha; una nyumba nzuri ya ghorofa huwezi kupanda juu, unaumwa miguu; una mifugo ya kila aina huwezi kula nyama, huli sukari, huli chumvi, huli mafuta, hunywi soda, wakikuletea chakula chenye mafuta na chumvi nyingi unafoka sana,nini sasa?
Ebu kataa kujikataa! Tunapaswa kufanya jitihada kubwa za kutafuta maisha na kuyaishi hayo maisha.Kwa nini ujinyime saana eti hela zote zinakaa benki,haziguswi akigusa mtu unakufa kwa presha!
Kula vizuri na kulala pazuri ni sehemu ya maisha pia. Siyo mtu unalala njaa.Umefungua biashara lakini unalala dukani kulinda biashara mpaka asubuhi,huendi nyumbani,huoni mwenzio,huwaoni watoto,eti unatafuta PESA/MAISHA! Wakikuua?
Tafuta mlinzi, mlipe ili nawe upate muda wa kupumzika ili uchaji akili upate mawazo mapya ya kutafuta maisha.Utakuwa umemsaidia na huyo mlinzi umempa maisha!
Kukosa usingizi kunakufanya uonekane umerukwa na akili. Kumbe ni uchovu wa kutafta maisha,really?
Hata unapotafuta maisha ya wanao kumbuka kutafuta na maisha yako pia. Watoto wanabadilika. Usijisahau sana ukaishi kwenye kiatu cha mwanao ukasahau ya kwako!Huu ni ujinga tu kama ujinga mwingine!
Tumeona wazazi wengi wakijipa jukumu la kulaani kila anayewanyima kwa sababu tu watoto wao waliwaacha solemba. Ukimwacha mtoto ujue nawe utaachwa naye!
Mpende mtoto wako kama unavyojipenda mwenyewe. Siyo unashindwa hata kuvaa kiatu kizuri kwa sababu unasomesha. Ebu jaribu kalance bhana! Kujipenda siyo ubinafsi hata kidogo,kujipenda ni kujithamini na ndo mwanzo wa kuwapenda wengine,kwa sababu vitabu vya dini vinasema "mpende kama unavyojipenda".Hii inamaana wazi kwamba utampenda mtu mwingine kwenye levo ileile ya unavyojipenda.....
ZINGATIA....Hakuna binadamu atakayekupenda kuliko anavyojipenda,ni mbwembwe tu na uwongo!
Kuna watu hawajawahi kuishi tangu wazaliwe. Wao ni busy kutafuta maisha tu. Hawana muda wa kupumzika, hawana wikendi, hawana likizo, hawana muda wa kula,hawana usiku na hawana mchana,wao wanachakarika,alafu wakipata tu paaa,wanaondoka hawapo duniani!
KWA NINI?
Wanapata maisha, wanashindwa kuyafaidi, wameishaumizwa na mapambano ya kutafuta maisha. Wanaanza kutumia walivyochuma kutafuta afya!Wamepata pesa lakini afya imeondoka?
Ishi kabla ya kuchoka. Tafuna mifupa ungali una meno. Enjoy na familia yako iwezekanavyo,watakukumbuka endapo utakuwa umetangulia!
Yaani inashangaza,mwingine,hata akiumwa anaona heri akafie kazini kuliko kujipa muda wa kupumzika na kupona vizuri.
Toka out, kula vizuri, shushia na pepsi baridi, rudi nyumbani kwa mbwembwe, soma kitabu au sikiliza mziki mpaka usingizi ukupitie, asububi nenda katafute maisha.
Maisha ni uwiano wa kazi na bata. Kimoja kikizidi kingine kikapungua utapata shida. Hata kuulisha mwili tu bila kuilisha akili ni hatari kabisa kwa usalama wako.
Ushauri wa bure huu,acha au uchukue..