Mambo si shwari tena Tanzania vs USA

Mambo si shwari tena Tanzania vs USA

Beggers cant be choosers! Imf and the wb and other donors are controlled by the US!

We are bankrupted! Dolla juu , hospital s going without drugs and civil servents going months without pay.

is this what you promised Mr. President?
 
east daima,nani aende west ,unapewa condom kisha masharti kibao.
..........Kweli Mkuu, heri aegemee upande wa East anapopewa Suti na tende bila ya masharti magumu ya kubadilishana kwa Hotel na Wanyama pori wetu tu!.
 
Kula au pokea pesa ya Mla Rushwa ila kwenye kura mpe yule asiyetoa rushwa... Fumula yake ndio hiyo.. Mwache Putin aje tule pesa yake pia...
 
Uongozi ni talanta na sio uswahiba! huwezi kuwa rafiki na taifa kama la marekani na uingereza ukaishia pazuri! haya ngoja tuone mtinange huu utakuwaje!

well said. huwez kuwa rafik wa tajir halaf unamsalit. mwisho wa tanzania ni uchochez wa migogoro ya wenyew kw wenyewe na wakuu wale kuishia kuleta majesh na kuwekeza kwa mwamvuli mwngine
 
Hii hapa post yenyewe;

Nakubaliana nawe kabisa mkuu.
Ni kweli Marekani na U.K zinatuhumiwa kuleta vurugu sehemu mbalimbali duniani ili kushinikiza maslahi yake na wamekuwa wakileta vita nchi nyingi ilimradi kama vurugu inasaidia maslahi yao.

Hata hivyo jamaa si wapuuzi kivile,ni wakoloni na wezi wazoefu tangu enzi. Wanachotazama ni mazingira ya eneo husika kama panahitajika vita au amani ili kudumisha maslahi yao.

Ukitazama Tanzania,wananchi wake wako chini mno katika kutambua na kudai haki zao.

Hali hiyo ndio inayoipa Tz sifa ya utulivu wa muda mrefu.

Watz wanahitaji basic needs fulani tu ili waione dunia ni pepo,ukiwapa hizo hata ukiwaibia they dont care.

Hii inaifanya Tz kuwa very special case.

Serikali iliyopo madarakani Tanzania hivi sasa,hasa kuanzia awamu ya tatu hadi ya nne,imekuwa ikiharibu uchumi wa watz walalahoi kufikia kiwango cha kuwastusha na wameanza kujitambua taratibu.

Serikali hii haijui kula na kipofu.

Wamarekani wanalijua hili vizuri,so usishangae wakajenga uhasama na serikali hii,kwani wanaona kwamba dalali wanayemtumia atawagharimu kutumia nguvu kulinda maslahi katika siku za usoni,mahala ambapo pasingekuwa na ulazima wowote kufanya hivyo,kama dalali huyo,angejua namna ya kula na kipofu.

Tena C.I.A wanaweza kutumia scenario hiyo kujenga trust kwa watz before it's too late,kwa kuipiga vita serikali inayochukiwa na watz wengi,wakapandikiza mtu wao katika mazingira yanayokubalika na watz,wakampa support,wakampaisha,wakamuingiza kwenye siasa zenu kisiri,mkampigia kura na kujipatia "Yeltsin" wenu,mkaanza kuongozwa kwa remote from Washington bila kujua,tena mkaridhika nae kwa kuwa kafundishwa namna ya kula na kipofu,na U.S ikatumia nguvu ndoogo kudumisha maslahi yake ndani ya Tz kwa miaka mingi hadi kitokee kizazi cha wenye macho badala ya vipofu,huku na wao wakiwa wameshaiba sana.

So,tusifikiri wakati wote mmarekani anataka vita,no,kuna wakati anataka amani kabisa ikiwa amani ndiyo tool nzuri kulinda maslahi yake kulingana na eneo husika unless eneo hilo halina umuhimu mkubwa sana kwake.

Kwa jinsi tabia ya utulivu ya watz ilivyo,tena walivyo consistent kwenye tabia hiyo,nina wasiwasi kama C.I.A wanafurahia ukandamizaji wa "mchana kweupe" unaofanywa na hawa mafisadi wetu,kwa sababu utaondoa utulivu wa watz mapema mno,bila ulazima wa kufanya hivyo.

Na utulivu wa watz ni wa wajinga,so ni tool nzuri kuwaibia.

We waachie uchumi wa kuchangia harusi,kucheza ngoma,kununua Toyota ipsum,kujenga nyumba ya vyumba viwili,kula kitimoto,bhaas,utaiba mafuta bila kuulizwa,tena watakusaidia uyabebe vizuri.

Kwa hiyo CCM huenda wako kwenye wakati mgumu sana,hawakubaliki na wananchi,hawapati support ya "mabwana wakubwa" wa dunia,kilichobaki ni hao wakubwa kuwatengenezeeni "Yeltsin" wao wampigie debe mumkubali kabla wananchi hamjajitengenezea "Yeltsin" wenu,kitu ambacho kitakuwa ni worst case scenario kwa mafisadi wote,wa ndani na nje.

Na maneno ya uzi kama huu,ikiwa mleta mada ni mwandani wa serikali,basi "wambea" tumeanza kunusa harufu kuwa serikali yetu ipo juu ya misumari ya moto,inatapatapa.

Hata huyo Putin si mjinga,KGB wake watampa mrejesho ili ajue wabongo tulipishana wapi na wazungu wenzie,halafu atafanya maamuzi akiwa influenced na factor hiyo pia.

Sidhani kama mbia wa biashara asiyekuamini ni mzuri kwako,ataishi nawe kwa tahadhari iliyopitiliza ambayo muda wowote ukijichanganya anaweza kukutia hasara kubwa.

Tabia ya ufisadi uliopitiliza ya viongozi wetu imevuka mipaka na kutoaminika hata na hawa wezi wenzao wa kimataifa.

Hata wizi nao unahitaji kuwa smart ili uwe mwizi wa kudumu.

wenye akili kumbe mpo.wape mfano Syria ilipo lleo
 
Si kweli hata kidogo wala asingeweza, kama alikuwa kidume kwa nini aliondoka madarakani? Kwa uhakika aliondoka ili kuficha aibu ya sera zake kufa kifo cha mende.

mwl alikuwa mjanja. aliwahi kijitoa. kweny hotuba zake aliwakejel wanaopenda madaraka. kimsingi rais anatakiwa awatumie wataalam kusoma alama za nyakat. siku zote hata wewe lazima uwape nafas maadui na marafiki ili uish salama. Tanzania tunawaibia hata wafadhili. hatuna msimamo
 
hii ni habari ya kufikirika, hakuna ukweli ndani yake, marekani ipo huru kudeal na yeyote yule, that is known and respected by other sovereign states, we are also free to meet, talk, deal or not deal with any one as a free and sovereign state, that should be respected by other free sovereign states, USA is and has been our good and trusted partners for a very long time, that is undisputed fact and it will remain like that for years.

uko nyuma ya kila ktu
 
USA watapandikiza Ebola hao China na Russia watakimbia wenyewe 😉

USA hawawezi kutumia risasi kwa watu wasiojua hata haki zao za msingi.

Miaka 50 bado tunajisifia kuomba!!!
 
Safi sana..bora US waipige choni Tanzania , hawa magamba wametuharibia nchi
 
Acha uongo wako wewe hao watu wa west ni yupi aliyetoa hela ya bajeti katika historia ya taifa hili tanzania?

am sure hujui hata bajet ya Tanzania kwa mwaka ni sh ngapi, na hujui hata make up ya budget na source yake.

Poor you, nakuhurumia
 
well said. huwez kuwa rafik wa tajir halaf unamsalit. mwisho wa tanzania ni uchochez wa migogoro ya wenyew kw wenyewe na wakuu wale kuishia kuleta majesh na kuwekeza kwa mwamvuli mwngine

Kama kiongozi wa Taifa la kiafrika ni bora ukasahau kuwa eti iko siku uta watawala wakoloni wako wa miaka ile kwa formular ya "DEVIDE AND RULE" zaidi ya hapo ni wazi watakushughulikia kama mchonganishi. huna maliasili za kuwatosheleza haya mataifa makubwa namna hii na yenye nguvu kwa kila sekta! saini mkataba na mmoja na u dili naye huyo huyo tena kwa akili sana! sasa mikataba ile ile nchi kubwa duniani zooote umesaini nao kifuatacho ni nini? haya bwana!
 
DON'T PLAY WITH U.S.A.... never CHEAT U.S.A...

U.S they can sabotage J.K or any PRESIDENT HARAKA SANA.....U.S.A ni danger...

Mm ningependekeza JK. aachane na mikataba ya CHINA...na PUTIN asikanyage hapa TZ.....na hiyo mikataba 16 aachane nayo sbb ITATUDHURU SANA...NA U.S.A wanaweza sababisha vita vya kwetu wenyewe kwa wenyewe...i.e CIVIL WARS, like ARAB SPRING...ni U.S.A who financed and main player of ARAB SPRING....so tuwe makini sana...!!!

Mkuu mbona umejikatia tamaa namna hiyo, USA huwa hana permanent friend wala permanent enemy na hata ujipendekeze vipi anakubadilikia ghafla, wanaweza wakakuita gaidi alafu baadae tena ukawa rafiki yao kikubwa wawe na interest kwenye nchi yako. Hizo siasa za West na East ni zao wenyewe zilianza kitambo zamani zile za maporoko ya kiuchumi ya Ulaya (enzi za Marshall plan)

Tz kama nchi inashirikiana na mtu yoyote kikubwa tu kuheshimu terms and conditions yenu, urafiki na USA unatakiwa uwe wa design hiyo yaani uwe nusu nusu usiende mazima na kuwasahau wadau wengine
 
USA watapandikiza Ebola hao China na Russia watakimbia wenyewe 😉

USA hawawezi kutumia risasi kwa watu wasiojua hata haki zao za msingi.

Miaka 50 bado tunajisifia kuomba!!!
Alafu na sie tunajifanya kuondoa operation ombaomba mtaani wakati hao wanaotuongoza katika ngazi za kimataifa ni ombaomba
 
Hii ni sera ya zamani sana...

Ambayo ilianza tangu 1961 ambapo CHINA mwenyewe alikuwepo, na kwa jinsi China ilivyopiga hatua ni kama imeshaondoka automatically maana ipo katika kundi la vigogo wa kicuhumi
 
Kula au pokea pesa ya Mla Rushwa ila kwenye kura mpe yule asiyetoa rushwa... Fumula yake ndio hiyo.. Mwache Putin aje tule pesa yake pia...
Putin, Obama, Xi Ping, Cameron et el wote ni WANAUME wa kazi, sasa kumbuka vya MWANAUME haviliwi bure ati!
 
Back
Top Bottom