Mambo kumi usiyoyajua kuhusu marehemu Aboud Jumbe

1. Rais wa Awamu ya Pili wa Zanzibar, Alhaj Sheikh Aboud Jumbe MIAKA 32 iliyopita, Januari 1984, Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama cha Mapinduzi (CCM), iliyoketi mjini Dodoma kwa dharura, ilimvua (ilimpindua?) nafasi zote za uongozi, Nyadhifa alizovuliwa kiongozi huyo na kubakia kuwa raia wa kawaida ni pamoja na urais wa Zanzibar, uenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, umakamu wa Rais wa Tanzania na umakamu Mwenyekiti wa CCM Taifa.
2. Marehemu mzee Jumbe alikuwa mrithi wa Rais wa kwanza wa Zanzibar, Sheikh Abeid Amani Karume, aliyeuawa katika jaribio la mapinduzi ya kijeshi lililoshindwa, Aprili 7, 1972. Kabla ya hapo, Jumbe alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, akishughulikia mambo ya Muungano.
3. Jaribio la mapinduzi lililoshindwa liliandaliwa na wanasiasa makini wa Kizanzibari kwa kuhusisha baadhi ya wanajeshi wa Jeshi la Zanzibar, ambalo hadi akiuawa, Karume alikuwa bado Amiri Jeshi Mkuu wake; kwa kushirikisha pia wanajeshi kadhaa wa Kizanzibari waliokuwa kwenye Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWT) kwa upande wa Bara.
4. Mwalimu Nyerere hakutaka mauaji ya Rais Karume yatafsiriwe au yahusishwe na jaribio la mapinduzi, bali alitaka yatafsiriwe kama mauaji ya kisiasa tu. Akasema, hatua yoyote ya kumteua Kanali Seif Bakari ambaye ni mwanajeshi, kuchukua nafasi ya Karume aliyeuawa na mwanajeshi pia, kungetafsiriwa kama Mapinduzi ya Kijeshi. Hapo, Wazanzibari wakanywea, wakatazamana kwa ishara bila kupata jibu kwa hoja ya Mwalimu Nyerere. Hawakuwa na namna isipokuwa kufuta pendekezo la uteuzi wa Kanali Seif Bakari kumrithi Karume.

5. Ndipo ikawadia zamu ya Mwalimu Nyerere kushawishi na kushauri nani ateuliwe. Akasema, pamoja na kuuawa kwa Karume, ambaye alikuwa mwasisi mwenza wa Muungano wa Tanzania, Muungano huo lazima uendelezwe bila kuyumba; na mtu pekee aliyefaa, kwa maoni ya Nyerere, alikuwa ni Aboud Jumbe Mwinyi, kwa sababu kuu tatu:-

(a). ni msomi na mwanasiasa mkongwe mwenye kuzielewa vyema siasa na migongano ya jamii ya Kizanzibari.
(b). ni mtu ambaye hakuwa na majungu wala makundi yenye kuhasimiana.
(c). wadhifa wake wa Waziri wa nchi, Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais (Mambo ya Muungano) kwa muda mrefu, ilikuwa ni sifa ya ziada iliyompa uzoefu, na uwezo wa kuendeleza na kudumisha Muungano.
Hoja ya Mwalimu ikapita; Jumbe akapaa, akawa Rais wa Zanzibar wa awamu ya pili.
5. Oktoba 1976, maridhiano yalifikiwa ya kuunda Chama kipya, Chama cha Mapinduzi' (CCM), kilichozinduliwa Februari 5, 1977, tarehe na mwezi sawa na ilipozaliwa ASP miaka 20 nyuma, mwaka 1957.
Licha ya Wazanzibari kushinikiza tarehe na mwezi wa kuzaliwa chama chao, yaani Februari 5, walishinikiza pia na kufanikiwa kubakiza neno;Mapinduzi' yaliyoleta uhuru wao Januari 12, 1964, liwe sehemu ya jina la chama kipya. Kwa maana ya Chama cha Mapinduzi bila kuwa na tafsiri yake kwa lugha ya Kiingereza.

6. Hofu ilitanda miongoni mwa Wazanzibari pale Mwalimu alipopendekeza mabadiliko zaidi ya Katiba kutaka kuunda Serikali moja badala ya Serikali mbili, wakihofia nchi yao kumezwa na Tanganyika. Hali hii ilimweka pabaya Jumbe Visiwani juu ya uswahiba wake na Nyerere, wakimwita ;msaliti' wa Mapinduzi ya Zanzibar na Wazanzibari.
kuona hivyo, Jumbe alianza kugeuka nyuma kwa kuchanganyikiwa; akawa njia panda. Wakati hilo halijapoa, jingine kubwa zaidi lilikuwa njiani likija. Mwaka 1983, Edward Moringe Sokoine, aliyekuwa Waziri wa Ulinzi wa Muungano, aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu. Sokoine alikuwa na mvuto wa watu, shupavu na mwadilifu kiasi kwamba katika kipindi kifupi tu alijidhihirisha kuwa chaguo la watu na mrithi halali wa Mwalimu, ambaye naye alimkubali kwa ishara na kwa vitendo.

7. Kwa kuridhika na Sokoine, taratibu Mwalimu alianza kumbeza Jumbe kwa sababu nyingi, lakini Wacha nitaje mbili tu.
(a), alimwona kama kiongozi mpweke asiye na sapoti na aliyepoteza mvuto Visiwani, pia kama dikteta mkimya asiyeshaurika na watu wa chini yake.
(b); Mwalimu aliudhika kwa Jumbe kugeuka mhafidhina wa kidini na mpambanaji wa Kiislamu katika Taifa lisilo na dini. Kwa hili, Jumbe alizuru nchi nzima akitoa hotuba kwenye misikiti, na Serikali ikalazimika kutoa Waraka mkali wa Rais, kuwakumbusha na kuwataka viongozi wa kitaifa kutojipambanua au kuendekeza mambo ya kidini. Jumbe alipuuza Waraka huo; kwake ndio kukawa kumekucha.

Habari za Mwalimu kupoteza imani na upendeleo kwa Jumbe hatimaye zilimfikia kiongozi huyo, zikamuuma sana na kumvunja moyo. Hapo uhasama ukazuka kati yake na Mwalimu kwa njia ya kukomoana. Kwa hasira na kukata tamaa, Jumbe akaanza maandalizi ya kuumbua Muungano, kwa minyukano na Mwalimu.

8. Kuanzisha minyukano hiyo, ilikuwa ni lazima kwanza Jumbe arejeshe imani yake iliyopotea kwa Wazanzibari, kutokana na hatua yake ya kuhamia Mji mwema, Kigamboni na kwa kuwatelekeza Wazanzibari. Baada ya kuridhika kwamba mambo ameyaweka sawa, aliomba mawazo ya Makatibu Wakuu wa Wizara zote na Watendaji Wakuu wengine wa Serikali, ni aina gani ya Muungano unaotakiwa.
Wote, isipokuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali wa Zanzibar, Damian Lubuva, walikataa muundo wa sasa wa Serikali mbili au wa Serikali moja uliokuwa umeanza kupigiwa upatu na Mwalimu na baadhi ya wanasiasa. Jumbe na watendaji wake hao ndani ya Serikali ya Zanzibar wakapendekeza muundo wa Shirikisho lenye Serikali tatu. Serikali ya Tanganyika, Serikali ya Zanzibar na Serikali ya Muungano kwa mambo kumi na moja tu yaliyoainishwa katika Mkataba wa awali wa Muungano.

9. Mtizamo huo ndio aliouweka wazi Jumbe baadaye katika kitabu chake kiitwacho;The Partnership,' yaani ;Ubia kati ya Tanganyika na Zanzibar,' kilichosambazwa mwaka 1984. Kuthibitisha hilo, ananukuu ibara ya tano ya Mkataba wa Muungano inayosema kwamba kufuatia kuundwa kwa Serikali ya Muungano, "Sheria za Tanganyika zilizopo na zile za Zanzibar, zitaendelea kuwa na nguvu katika nchi hizo." (The Partnership, uk. 22).

10. Kuanzia hapo, madai ya Wazanzibari kutaka mabadiliko ya Katiba, huku wengine wakitaka warejeshewe Visiwa vyao (Zanzibar), kupitia mihadhara, magazeti na redio, yalipamba moto ambapo wanajeshi wa Kizanzibari nao walikuwa na malalamiko yao.
Hadi Mungu kamchukua, Mzee jumbe alikuwa ni kiongozi mpambanaji asiyeyumbishwa na kutishwa. Mzee Jumbe amekuwa mgonjwa kwa sikuu kadhaa kabla ya kifo chake,Pamoja na hayo, Mzee Jumbe amekuwa mnyonge kutokana na familia yake kukumbwa na dholuba la maladhi kwa kipindi kilefu, Akiwemo mkewe, na mwanae ambao nao taarifa zinaonyesha kusumbuliwa na maladhi.
...hii ndio historia fupi ya mzee wetu mpendwa aliye tutoka; Mungu aipokee na kuilaza mahali pema peponi;
Ameen ya rabi
Shukrani sana kaka kwa darsa mujarabu!
 
Hizi ni propaganda kama zile zilizotumia kumchafua ahmed salim kuwa siyo mzanzibar na nyengine nyingi..
Yaan mtu anaekubalika zanzbar ndyoo anaechafuliwa sana ili akose sifa za kuwa kwenye ile nafasi anayostahili...

mahasimu wa malim seif..walipoona kuwa malim anakubalika zanzbar haswa baada ya kuvuliwa uanachama dodoma kule..wakaona kuwa njia rahisi na nzuri ni kumchafua kwa kile kitu kinachoitwa kumchongelea mzee jumbe kwa nyerere..wakijua kuwa kiu ya zanzbar ni serikal tatu na zanzbar yenye mamlaka kamili na mzee jumbe nae akiwa mstari wa mbele juu ya hili.sasa kutofanikiwa kwa mzee jumbe kukafanya wazanzbar wamchukie kila mtu aliekwamisha nia hii nzuri ya jumbe..ndipo kitengo cha propaganda cha chama kile kikajua kuwa huu ni wakat muafaka wa kumuhusisha maalim na usaliti ili achukiwe zanzba..
Sisi tuliokuwepo zanzbar miaka ile tukishriki mambo ya chama na gvt tunajua hili...

Mungu ampumzishe jumbe mzee wetu..muumini wa fikra huru



Katika hili kama kuna Mtu kamchafua Maalim Seif basi ni yeye Mwenyewe kwa kuwa amekiri kupinga andiko la Jumbe kwa hoja kuwa Jumbe alitaka Serikali tatu ili apate Mamlaka zaidi ya kulishughulikia kundi la Kina Maalim Seif lililiokuwa linaitwa Front liners dhidi ya kundi la Mahasimu wao la Wahafidhina la Conservatives.
Uwe unafuatilia Masuala ya Kisiasa kwa ukaribu kabla ya kujikweza na kujipa Uwakili wa kutetea Mambo ambayo hata Wanasiasa wenyewe wamekiri kuyafanya.
 
Serikali ya CCM haiwezi fundisha busara za Mzee Jumbe sababu anachukuliwa kama mpinzani wa Mungu Mtu wao Nyerere!

Ukionana na wazee Unguja watakuambia wazi kabisa mtu pekee ambaye alikuwa anaweza kumuambia Mzee Karume kama hapo umekosea na tufanye hivi alikuwa ni Aboud Jumbe

Alikuwa haogopi kusema ukweli hata akijua kufanya hivyo anahatarisha maisha yake
alikuwa shujaa!mwache apumzike kwa amani!
 
Jumbe January 1984 alicho sema na kufanya kimefanywa juzi tu hapa na AG wa ZNZ alipo tamka wazi kuwa yy kama AG wa ZNZ msimamo wao ni serikali 3!Mzee Jumbe alisimamia anacho amini ni kweli

Nyerere na Kamati kuu yote ilipomuuliza kama ni kweli anataka serikali 3,Mzee Jumbe bila kuogopa akasema YES na akatoa sababu nzito!

Usiku huo huo ikatangazwa hali ya hatari ZNZ;Mzee Thabit Kombo Mzanzibar mwingine mwneye msimamo nae akiwa matibabuni KCMC Moshi akawekwa chini ya ulinzi asiongee na media!

Wanafiki CCM Dar wakaitisha maandamano makubwa kumkashifu Mzee Jumbe na baadae maandamano kmq hayo yalifanyika TZ nzima na kuhutubiwa na viongozi wa kitaifa wa CCM na serikali Kwa ujumla. Nyerere mwenyewe akaongoza pambio la kumtusi Mzee Jumbe la "Jumbe analia,analia kunyonya"alipokuwa anahutubia maafisa wa JWTZ Milambo Tabora

Kwa sisi tuliokuwa wakubwa tulijionea jinsi Mzee Jumbe alivyo dhihakiwa hata alipotiwa kizuizi cha nyumbani Mji Mwema ambako hakutakiwa mtu yyt kwenda zaidi ya mkewe!

Kama kuna Jehanam nitashangaa sana siku hiyo nisipomkuta Mwl Nyerere!

Tangulia Mzee Jumbe,misimamo yako na kusimamia ulichokuwa una kiamini kimekufanya uishi kama mtumwa ndani ya nchi yako
Daaaah!! Inauma mno!! Mungu amlaze peponi mzee Jumbe,
 
Nyerere hakupenda watu wenye kumchallenge kama kina

1) Karume
2) Kambona
3)Malechela
4)Kolimba
5) mzee Jumbe (baadae)
6) Abdulwahid Sykes

Yeye alipenda watu loyal sana kwake kina

1)Msekwa
2) Mkapa
3) Kawawa
4) Butiku

Lilikuwepo pia kundi la wajanja wasiopingana naye wazi, wao wanamsikiliza, hawambishii, lakini wakitoka hapo wanafanya wanavyoona wao inafaa kama vile.

Mzee Mwinyi
 
Mh wazir dokta rais wa zanzibar anaongoza kutumia remote pale dodoma hana power yyte

R.i.p mzee jumbe
 
sana,nakumbuka wakati niko middle school mwaka wa pili ndo lubuva akaja kuanza mwaka wa kwanza,ni zamani sana
Hapa pana darsa lingine tutapata kwanza kujua hiyo shule na pili waweza kutuambia kijana wa waqt huo lubuva namna yake na mwenendo wake hapo shuleni.
 
Natafuta kitabu chake cha " The Partnership: miaka 30 ya Dhoruba " kwa anayejua vinapopatikana wakuu...
 
Jumbe ALIZALIWA mwaka 1920 huko MPITIMBI-Ruvuma
Wazazi wake walihamia Makunduchi Unguja toka Bara kwenye miaka ya 1925 Jumbe akiwa na miaka mi 5
Jumbe atakumbukwa kwa uwezo wake wa kupangua hoja bila kumuogopa Nyerere
Hakika alitendea haki sana elimu yake kubwa
Kumbe Jumbe ni Mtanganyika
 
Back
Top Bottom