Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 10,129
- 35,148
Haya ni mambo muhimu 7 mabaya usiyoyajua kuhusu Mifuko ya Pensheni (Mafao) hapa Tanzania. Ni sehemu ya maelezo kutoka kwa baadhi ya wakurugenzi katika mifuko hiyo.
1/Inaendeshwa kwa mtindo wa UPATU (Yaani Michango ya wanachama wake wa sasa ndio inatumika kulipa mafao ya mstaafu wa Leo. Kasheshe ni pale wanachama wake wengi wakijitoa mara moja..)
2/Mwisho wa siku mifuko yote ITAFIRISIKA. (Katika hilo hakuna ujanja, ni jambo la kiasili na kihistoria, lipo tu na limeshatokea sana duniani, kinachofanyika ni kusukuma siku tu ili kizazi kingine kifie nalo..)
3/Mifuko yote inaendeshwa kwa msukumo wa KISIASA zaidi na sio kiuchumi. (Mwenendo wa mifuko hiyo iko kuwaridhisha wanasiasa wakuu ndani ya serikali kwa sababu watendaji wake wote wa juu wanateuliwa kisiasa zaidi)
4/Mifuko yote ni AKIBA ya dharula ya serikali (Wakati wowote serikali inaweza kuamuru kutumia mitaji ya kifedha ya mifuko hiyo ili kukidhi mahitaji ya uendeshaji wa miradi na mipango ya kiserikali)
5/Miradi yake mingi imewekezwa kwa HASARA.
(Mifuko hii ndio inayoongozwa kuwekeza kwenye miradi mingi isiyokuwa na faida ya maana kibiashara, mingi ya miradi yake ni ili kulinda mtaji tu)
6/Inaendeshwa kwa GHARAMA kubwa sana.
(Mifuko hii imeajiri watumishi wengi sana, ina kurugenzi nyingi sana, ina matumizi makubwa sana huku mengine yakiwa ni matumizi ya Anasa. Gharama za uendeshaji wa mifuko hii ni zaidi ya Faida inayoweza kupatikana katika miradi yake)
7/Mifuko hii haifanani katika kulipa MAFAO.
(Kila mfuko unatumia kanuni yake, kanuni nyingine zinapunja na kanuni nyingine zinalipa vizuri, kanuni hizi sio za kudumu milele, ziliwahi kubadilika, zinabadilika na zitabadilika kufuatana na msukumo kutoka kwa wanasiasa nk).
*UJUMBE.
Wafanyakazi walioajiriwa wajipange namna bora ya kuishi kwa kuweka Akiba ya Mali na Pesa binafsi wakati wakiwa bado wanafanyakazi, suala la kungojea Mafao ya Kustaafu kutoka kwenye mifuko ya Pensheni ili wafanikishe mambo yao huko baadaye ni hatari sana hasa hasa kwa kipindi hichi na huko tunapoelekea.
1/Inaendeshwa kwa mtindo wa UPATU (Yaani Michango ya wanachama wake wa sasa ndio inatumika kulipa mafao ya mstaafu wa Leo. Kasheshe ni pale wanachama wake wengi wakijitoa mara moja..)
2/Mwisho wa siku mifuko yote ITAFIRISIKA. (Katika hilo hakuna ujanja, ni jambo la kiasili na kihistoria, lipo tu na limeshatokea sana duniani, kinachofanyika ni kusukuma siku tu ili kizazi kingine kifie nalo..)
3/Mifuko yote inaendeshwa kwa msukumo wa KISIASA zaidi na sio kiuchumi. (Mwenendo wa mifuko hiyo iko kuwaridhisha wanasiasa wakuu ndani ya serikali kwa sababu watendaji wake wote wa juu wanateuliwa kisiasa zaidi)
4/Mifuko yote ni AKIBA ya dharula ya serikali (Wakati wowote serikali inaweza kuamuru kutumia mitaji ya kifedha ya mifuko hiyo ili kukidhi mahitaji ya uendeshaji wa miradi na mipango ya kiserikali)
5/Miradi yake mingi imewekezwa kwa HASARA.
(Mifuko hii ndio inayoongozwa kuwekeza kwenye miradi mingi isiyokuwa na faida ya maana kibiashara, mingi ya miradi yake ni ili kulinda mtaji tu)
6/Inaendeshwa kwa GHARAMA kubwa sana.
(Mifuko hii imeajiri watumishi wengi sana, ina kurugenzi nyingi sana, ina matumizi makubwa sana huku mengine yakiwa ni matumizi ya Anasa. Gharama za uendeshaji wa mifuko hii ni zaidi ya Faida inayoweza kupatikana katika miradi yake)
7/Mifuko hii haifanani katika kulipa MAFAO.
(Kila mfuko unatumia kanuni yake, kanuni nyingine zinapunja na kanuni nyingine zinalipa vizuri, kanuni hizi sio za kudumu milele, ziliwahi kubadilika, zinabadilika na zitabadilika kufuatana na msukumo kutoka kwa wanasiasa nk).
*UJUMBE.
Wafanyakazi walioajiriwa wajipange namna bora ya kuishi kwa kuweka Akiba ya Mali na Pesa binafsi wakati wakiwa bado wanafanyakazi, suala la kungojea Mafao ya Kustaafu kutoka kwenye mifuko ya Pensheni ili wafanikishe mambo yao huko baadaye ni hatari sana hasa hasa kwa kipindi hichi na huko tunapoelekea.