Naombeni mchango wenu wana jf ili niweze msaidia huyu rafiki yangu. Anaitwa jane ni rafk yangu yapata miezi 5. Lakini juzi amenistajabisha aliponipa habari hii ya kusisimua, "mama yangu anamtaka mchumba wangu". Nilistuka sana kusikia hivyo. lakini nilijaribu kumuuliza yeye anaushaidi gani kuhusu jmbo hilo akasema hivi, nanukuu "mika ndio ameniambia na namumini xana hawezi kunidanganya hata siku moja, hususana kwa jambo kama hili" na pia akasema siku hizi mama yake amekua akimkaripia kuhusu mahusiano yake. Nilijaribu kumshauri lakini inaonekana amesha athirika kisaikolojia, imefiki kiasi kwamba anamchukia mama yake kupita kiasi. Ushauri wenu tafadhali. Maoni yangu: jamani akina mama na baba zetu tunao tamani wapenzi wa watoto zetu hamuoni mnakosea. Hebu tuweni na haya hata kidogo jamani basi kwa sababu haileti picha nzuri kwa family hata jamii. Tubadilikeni