Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,320
- 33,125
Michelle akiwa na mumewe na watoto wao 18 Friday, September 04, 2009 2:27 AM
Mama mwenye watoto 18 ambao wote amewapa majina yanayoanzia na herufi 'J' anategemea kuzaa mtoto wa 19 hivi karibuni. Mama wa watoto 18 Michelle Duggar kutoka Tontitown, Arkansas, Marekani anategemea kupata mtoto wake wa 19 mwezi machi mwakani ikiwa ni wiki chache baada ya kupata mjukuu kwa mara kwanza.
Mama huyo mwenye umri wa miaka 42 pamoja na mumewe Jim Bob ambaye anafanya biashara ya majumba wametengenezewa kipindi maalumu kwenye luninga kinachoelezea maisha yao na watoto wao 18 kinachoenda kwa jina la "18 Kids And Counting".
Bi Duggar alisema kwamba alishuku kuwa ana mimba nyingine baada ya mtoto wake wa 18 mwenye umri wa miezi nane kuanza kukataa kataa maziwa yake wakati alipokuwa akimnyonyesha.
Kwa kutumia uzoefu wa mimba zake zilizopita, alijua kuwa hii ni dalili ya ujauzito na alipofanya vipimo vya ujauzito alirukaruka kwa furaha baada ya kugundua ni kweli ana mimba.
"Tuna furaha kubwa sana" alisema Michelle na kuongeza "Tunasubiria kwa hamu kumuona mtoto wetu wa 19 na mjukuu wetu wa kwanza".
Mtoto wa kwanza wa kiume wa Michelle mwenye umri wa miaka 21, Josh na mkewe Anna, 21, wanategemea kupata mtoto wa kike hivi karibuni.
"Namshukuru mungu, nina miaka 42 wakati nikifikiria kuwa siwezi kupata mtoto tena , mungu ametubariki kwa mtoto mwingine" alisema Michelle.
Michelle na mumewe hivi sasa wanafikiria jina la kumpa mtoto wao wa 19 ambaye atajiunga na familia ya watoto 10 wa kiume na nane wa kike ambapo watoto wote wana majina yanayoanzia na herufi "J".
Ukianzia kwa mtoto wao wa kwanza Josh mwenye umri wa miaka 21, watoto wao wengine majina yao ni Jordyn-Grace mwenye umri wa miezi nane, mapacha Jana na John-David wenye umri wa miaka 19, Jill, 18, Jessa, 16, Jinger, 15, Joseph, 14, Josiah, 13, Joy-Anna, 11, mapacha Jeremiah na Jedidiah, 10, Jason, 9, James, 8, Justin, 6, Jackson, 5, Johannah, 3, na Jennifer, 2.
Matumizi ya chakula na mahitaji mengine ya lazima huigharimu familia hiyo kiasi cha Tsh. Mil. 2.5 kwa mwezi.
Wakati walipofunga ndoa, Michelle na mumewe walikuwa wakifikiria kuwa na watoto wawili au watatu tu.
Lakini baadae kutokana na imani yao ya kikristo waliona ni bora wamuachie Mungu aamue wawe wana watoto wangapi.
Habari Zaidi bonyeza hapa Website ya huo Mama >http://www.duggarfamily.com/photos.html