Mama wa kambo kaniharibia kila kitu

Wewe ndo baba?
 
Unaulizwa BABA na MAMA YAKO walikuwa WAMEFUNGA NDOA?? au kwa namna nyingine elezea vizuri kivipi huyu ni MAMA WA KAMBO KWAKO?? isije ikawa mama yako ndio aliyeivuruga ndoa ya huyu unayemuita mama wa kambo. Sorry though
 
Pole san Mungu atakuwa kimbilio na msaada kwako.
 
Alikua anathamini watoto wake kuwarithisha elimu kuliko mambo mengine. Ndugu wengine walikua hawajikita sana huko ndio kisa chakutengwa
Unatumia lugha ngumu na za picha, za nini hizo? Baba aliwekeza kwenye elimu ndo maana alitengwa, hapa unataka kusema nini?

Swali, je mzee kuna mali ameziacha? Kama ndiyo ongea na mama wa kambo kiupole, mwambie unaona kabisa huko mbele mtagombana, akugawie kitu kidogo kibinadamu tu ii usongeshe maisha yako, ikishindikana nenda mahakaman, maana hata ndugu zako wamekutenga kama unavyosema, ukiendelea kulia unazid kutengeneza giza, na giza likizid zaid itakuwa ngumu sana kujinasua
 
Nunua dumu la petrol choma kila kilicho cha maana alichoacha baba yako. Mkoswe wote kisha ingia mtaani pambana kama sisi
 
Haya maswali kila mtu anajiuliza, akijibu haya maswali ndo tutapata picha kamili, maana uandishi wake ni changamoto, anadhan kama anaonge nasisi live wakat anaandika
 
Haya maswali kila mtu anajiuliza, akijibu haya maswali ndo tutapata picha kamili, maana uandishi wake ni changamoto, anadhan kama anaonge nasisi live wakat anaandika
Hayo maswali nimejibu yote mkuu
 
Pole sana nimejarb kuvaa viatu vyako vimenishinda

Sent from my TECNO WX3 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu pole sana kwa hali yako.
Tafakari upya na kwa hekima yawezekana ulimkwazwa omba msamaha. Husisha watu wake wa karibu au ndugu zake au ndugu zako wakushauri. Ikishindikana nenda ofisi za ustawi wa jamii kwenye ofisi za kata ili uweze saidiwa.

Lakini yoote tisa kumi ni kwamba wanawake nahisi kwenye kile kikao chao na shetani pale bustani ya edeni swala la mtoto wa kambo walilijadili na figisu zilipangwa pale pale.
Nimeishi na mama wa kambo. Nilimuheshimu yy na watoto wake. Baba alinieleza hulka za yule mama. Kwa hiyo kwenye kazi za nyumban tulikuwa tunajituma mm na dada yangu na wadogo zangu wawili ambao hatukuwa ni watoto wa kuzaa kwa yule mama. Lakini yule mama alikuwa anatuchukia. Kazi zoote zilikuwa zetu. Kuanzia kupika, kufua , kufanya usafi kulima bustani na za hapa na pale. Watoto wake wali starehe huku ss tunapigika. Majungu na fitina kama zoote kila saa kumtukana mama yetu ambae hakuwepo pale. Cha aajabu wanae ilikuwa mwendo wa kufeli madarasa sisi tunafaulu. Mwanae akifika chuo DISCO ilikuwa inamuhusu. Ajira sisi tumepata wanae bado wanamsubiri MAGU afungue neema. Sifurahii mtoso wake lakini laana zoote alizokuwa anatupatia zimemrudi.


Ndugu yangu pambana, muombe sana mungu akusimamie jamani mama wa kambo ni kiumbe wa tofauti sana emu tuseme na ukweli.
Baba wa kambo anaweza kuwa zaidi ya baba hata kwa asilimia elfu moja ilia mama wa kambo ni wachache wenye moyo ya utu
 
Mama yako yuko wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…