HorsePower
JF-Expert Member
- Aug 22, 2008
- 3,612
- 2,566
Miaka michache nyuma, nikiwa ndiyo nimemalizia shahada yangu ya pili na kuanza kazi kwenye kampuni moja ya Insurance, nilibahatika kukutana na dada mmoja, mpole na mwenye muonekano wa unyenyekevu na tabia njema. Nilimpenda, akanipenda tukaamua kuwa wapenzi.
Baada ya miezi kama tisa hivi ya mawasiliano ya karibu mno, niliamua kwenda kujitambulisha kwao na nilipokelewa vzr mno na mama mkwe(bamkwe alitangulia mbele za hakii). Mamkwe aliniambia amefurahi kumpata kijana kama mimi kupitia kwa mwanae. Na pia alisisitiza kuwa mwanae ni binti mwenye tabia njema na hakuwahi kumletea kijana hapo nyumbani isipokuwa mimi. Nilifurahi.
Pamoja na kuwa na uhusiano wa karibu, bado mimi na huyu dada hatukuwa tunaishi nyumba moja ingawa yeye alikuwa akija nyumbani na kukaa hata wiki kabla ya kurudi kwake. Miezi michache baadaye mpenzi wangu alipata mimba. Sikuona kama tatizo sana maana nilijua kuwa hali kama hiyo ingeweza kutokea.
Cha ajabu wiki chache zilizopita, nilipokea ujumbe kwa mtu mwanaume nisiyemfahamu kuwa kuna ishu muhimu mno anataka kuongea nami ana kwa ana. Nilikataa. Baadaye yule kaka aliniletea ushahidi wa cheti cha ndoa na picha za harusi kuwa mpenzi wangu ni mkewe halali wa ndoa. Nilishangaa mno.
Nilipokuja kumbana mpenzi wangu alikiri kuwa alikuwa ameolewa kwa ndoa ila walitengana na mumewe kwa sababu za kifamilia na migogoro. Nilipombana mamkwe naye alikiri kuwa mwanae alikuwa ameolewa na walinidanganya ili wasije kunikosa.
Naomba ushauri jamani maana binti ana mimba, na mumewe naye anataka mkewe! Niwafanyaje hawa mtu na mamaye kwa uovu walionitendea? Ushauri pliz!
**** Haya yamemkuta rafiki yangu mmoja ambaye alinitafuta kuomba ushauri. Nami bila hiana nimeona niwafikishie wana JF wenzangu kupata mawazo yenu ****
Wenu,
HorsePower R. Kufakunoga
Baada ya miezi kama tisa hivi ya mawasiliano ya karibu mno, niliamua kwenda kujitambulisha kwao na nilipokelewa vzr mno na mama mkwe(bamkwe alitangulia mbele za hakii). Mamkwe aliniambia amefurahi kumpata kijana kama mimi kupitia kwa mwanae. Na pia alisisitiza kuwa mwanae ni binti mwenye tabia njema na hakuwahi kumletea kijana hapo nyumbani isipokuwa mimi. Nilifurahi.
Pamoja na kuwa na uhusiano wa karibu, bado mimi na huyu dada hatukuwa tunaishi nyumba moja ingawa yeye alikuwa akija nyumbani na kukaa hata wiki kabla ya kurudi kwake. Miezi michache baadaye mpenzi wangu alipata mimba. Sikuona kama tatizo sana maana nilijua kuwa hali kama hiyo ingeweza kutokea.
Cha ajabu wiki chache zilizopita, nilipokea ujumbe kwa mtu mwanaume nisiyemfahamu kuwa kuna ishu muhimu mno anataka kuongea nami ana kwa ana. Nilikataa. Baadaye yule kaka aliniletea ushahidi wa cheti cha ndoa na picha za harusi kuwa mpenzi wangu ni mkewe halali wa ndoa. Nilishangaa mno.
Nilipokuja kumbana mpenzi wangu alikiri kuwa alikuwa ameolewa kwa ndoa ila walitengana na mumewe kwa sababu za kifamilia na migogoro. Nilipombana mamkwe naye alikiri kuwa mwanae alikuwa ameolewa na walinidanganya ili wasije kunikosa.
Naomba ushauri jamani maana binti ana mimba, na mumewe naye anataka mkewe! Niwafanyaje hawa mtu na mamaye kwa uovu walionitendea? Ushauri pliz!
**** Haya yamemkuta rafiki yangu mmoja ambaye alinitafuta kuomba ushauri. Nami bila hiana nimeona niwafikishie wana JF wenzangu kupata mawazo yenu ****
Wenu,
HorsePower R. Kufakunoga