Mama mkwe ananipiga mizinga balaa

Wakwe wengi wasumbufu ndugu... Ata sio kua ana uwezo au hana. Nadhani mtu akioza binti yake anafikiri kajipatia suluhisho la kifedha... Sa ukikuta asiekua mstarabu ka huyo wa kwako ndo kero zaidi. Kama una uhusiano mzuri na mkeo ongea nae kuhusu swala hilo. Yeye ndo ataweza kusuluhisha bila wewe kuonekana vibaya. La sivyo utaumia tu kaka.
 
Watanzania tuna nidhamu, aibu, haya, heshima na hivi vinaturudisha nyumba. Kumwambia huyu mama ukweli vitakuweka huru maisha yako yote.
 
Mpige Jando
 
Itakuwa unaubaili kwa mkeo siku nyingine Fanya hivi akikuomba ela jaribu kumpa mtoto wake amtumie akikuomba tena mpe mtoto wake amtumie kuna kitu atajifunza lazima atapunguza alafu asipopunguza mchunie kibishi akikuuliza tena unamwambia mambo ajakaa sawa Hali ngumu. Ukimwambia mara mbili tatu atakukaushia kuna wamama wengine wanaomba ela bila watoto wao kujua Na wewe unajikuta unamtunia tu bila ata kumtaarifu mwanaye
 
Ishi katika uhalisia,jinsi unavyojiweka na ndivyo atakavyo kuchulia...usione sifa mkweo akisema mbele za watu kuwa ''MKWE WANGU HUYU HANA ROHO MBAYA JAMANI..MUNGU AZIDI KUKUPA''...wewe ongea na mkeo ili ajue kama hufurahishwi na tabia ya mama yake...jifanye tahira wenzio yao yatazidi kuwanyookea.
 
Mtongoze mama yako Mkwe ili akuchukie yaishe..ila usitumie simu tumia verbal tuu..
 
Kama ni mizunga vumilia hata yeye alilea kwa tabu usione vyaelea vimeundwa ndio nyie mliobanwa na makufuli mbona zama za kikwete ulikuwa hulalamiki bado mtakula mapera
 
Kama ni mizunga vumilia hata yeye alilea kwa tabu usione vyaelea vimeundwa ndio nyie mliobanwa na makufuli mbona zama za kikwete ulikuwa hulalamiki bado mtakula mapera
Hii si haki kwani huyu kijana hakulelewa kwa tabu? Kuna watu wanapenda sana vya mteremko inakera sana.
 
Kula yeye au vipi?
 
Kuna mtu ananisumbuaga sana kwa vibomu, mazingira niliyoyaweka ni kuwa nikiwa kazini siwezi kupokea simu na voice box siku zote iko full. Nilikutana nae akaniambia nidelete voice box. Hajui kuwa yeye ndio chanzo chake.
voice box ipoje uzuri wake..? inaweza kuwa suluhu ya matatizo yangu.
 
Umeshauri vizuri sana
Nahisi jamaa atumie hii mtoto wake ndo atakaye mwambia Hali yako mbaya.....
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…