Mama hajawahi kustaafu

Mama hajawahi kustaafu

Na katika kufanya kazi kwao huko miili yao inakuwa imara ndiyo maana hawaondoki mapema. Sisi wanaume kubweteka tu eti mzee wa kaya kucheza bao siku nzima halafu sigara, sijui pombe kufikisha 70 bahati sana. Hongera zao akina mama [emoji1545][emoji1545][emoji1545]
 
Baba yangu amestaafu akiwa na miaka 60.

Mama yangu pia ni mstaafu kazini, lakini kila napoona shughuli za Mama na Baba najifunza kitu kuwa hakuna mwanamke ambaye huwa anastaafu.

Huamka asubuhi na kumuandalia(Mumewe) Baba yangu chai ili hali naye ni mzee sana.

Mara amuandaliapo huingia katika maandalizi ya chakula cha mchana.

Huenda sokoni kutafuta mboga kwa ajili ya kupika, hata mara kadhaa amekuwa akitembea umbali mrefu kwenda bustanini kwetu kuchuma mboga na matunda.

Anapika kwa ajili ya wanae, ahakikishe wamekula chakula, tena huwauliza endapo wameshiba au apike chakula kingine.

Hata wageni wanapokuja nyumbani nyakati za usiku, Baba husema mimi naingia chumbani kulala atawaandalia Mama chakula mtalala “Usisahau kuwaonyesha sehemu ya kulala”

Mama huwaandaa wajukuu zake kwa ajili ya kwenda shule sambamba na kuhakikisha wamekunywa uji kabla ya kuondoka.

Anamjali na kumhudumia kila mwenye uhitaji ajaye nyumbani kwetu.

Hutembea umbali mrefu kwa ajili ya kutafuta kuni, kwa ajili ya kumpikia mumewe na familia nzima inayomzunguka.

Mama mara nyingi.huwa wa.mwisho kulala akihakikisha milango yote imefungwa na watoto wamelala ndani ya neti

Ni mama pekee hajawahi kustaafu.



Umejifunza nini kingine kwa mama?
Wafariji akina Mama kwa kushare ujumbe huu

C&PView attachment 1227943View attachment 1227944View attachment 1227945
Una bahati sana mkuu kwa kuwa na mama. Hakikisha unamwangalia na kumtunza sana. Tena wao hawana maneno mengi. Hata kama huna pesa kumjulia hali mara kwa mara. Kumwambia kuwa unampenda sana. Vizawadi vidogo vidogo vya mara kwa mara. Hata kama ni kipande cha sabuni. Na usipitishe wiki bila kusema naye...

Hakuna kitu kinachouma kama kuondokewa na mama. Na siku akiondoka kama mtu hukuwa sawa naye au kama ulikuwa unamchukulia hivi hivi tu aisee utajuta sana. Wapendeni na kuwaangalia sana mama zenu jamani [emoji1545][emoji1545][emoji1545]
 
Back
Top Bottom