Mama bado anaupiga mwingi?

Mama bado anaupiga mwingi?

Unapomwita Rais Samia Suluhu Hassan garasa unamaanisha nini? Au alipoteuliwa kuwa mgombea mwenza hamkujua maana yake?

Au Ulitaka itokee chadema halafu Salum Mwalimu ndio awe ikulu leo? Au wapinzani mlipokua mnachagua mgombea mwenza hamkuijua katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania?

Kati ya vitu vinaifanya CCM iendelee kuwa bora ni upinzani kuendelea kuwa dhaifu, kulialia, kudeka na kudemka
Mama D, ni wewe kweli!? Huzuni na majonzi vimeisha? Au umepata uteuzi😂!
 
Neno ‘mama’ lina maana kubwa maishani mwakila mmoja wetu. Ninapotamka ama kusikia neno mama mawazo yangu yanazama kwenye fikiria za matumaini, Faraja,huruma na upendo wa dhati usikuwa na kipimo kutoka kwa mama.

Rais wa awamu ya sita alipoingia madarakani akiwa ni mwanamama mioyo ya watanzania walio wengi ilipata matumaini, matarajio mapya Pamoja nakudhani nuru mpya imeingia.

Watazania walio wengi walidhani wakati wa uonevu hasa kwa wanasiasa wa upinzani, wafanya biashara wakubwa nchini na wale wote wenye mawazo kidhani na serikali yamezikwa na Magufuli kule Chato.

Mama naye hakuanza kinyonge kabisa alianza kwa bwebwe na kwa kauli zenye kuchochea matumaini makubwa ndani ya mioyo ya watanzania. Nakumbuka tarehe 01/04/2021 akiwa ikulu Chamwino Dododma akiwaapisha baadhi ya Mawaziri wake wapya aliowateua alimwambia Waziri wa fedha DR. Mwigulu Mchemba

“Muende mkatanue wigo wa walipa kodi, lakini pia mtengeneze walipa kodi wapya wengi Zaidi. Trend unayoenda nao sasa hivi nikuua walipa kodi, mnaua wafanya biashara, mnatumia nguvu Zaidi kuliko akili na maarifa kupata kodi.

Sasa wale mnao wakamua mkaenda kuchukua vifaa vyao vya kazi, kienda mkafungia akaunti zao, mkaenda chukua pesa kwa nguvu kwenye akanti kisa sheria inakuruhusu kufanya hivyo akitoka hapo anakwenda kufunga biashara anahamia nchi ya pili mnapunguza walipa kodi”. – Rais Sahia Suluhu Hassani.

Hii ni kauli yenye matumaini makubwa na inaleta Faraja kwa kila mtanzania hata mimi nisiyekuwa mfanyabiashara.

Fikira zetu zilianza kuamini maneno matupu kama haya na kudhani maisha mapya yanakuja and things will never be the same again.

Furaha ya kupata Rais wa awamu ya sita tena mwanamama ilifunika akili zetu kuzitafakari kwa kina kauli zake kama hizi ; “Ukinizingua tutazinguana” haya nayo ni maneno ya mama aliyoyasema tena uso na mikono yake ikionyesha msisitizo mkubwa huki pia kila akisimama kuhutubia anarudia rudia kauli yake ya “Mimi na Magufuli ni kitu kimoja”.

Ni kweli Mama na Magufuli ni kitu kimoja kwani wote wamepikwa na kuiva vizuri na Chama Cha Mapinduzi. Wote wawili ni mazao bora ya CCM.

Hawa wote wamepatikana kwa kupitia Katiba tunayoitumia sasa iliyoandika enzi ya chama kimoja na kufanyanyiwa marekebisho kadha wa kadha.

Tukumbuke Katiba hii iliandikwa na wanaCCM na marekebisho hata yake ya mwaka 1995 ya kuruhusu vyama vingi yaliongozwa na wanaCCM huku wakijua namna ya kutengeneza mfumo wa wao kuongoza milele.

Ngugu yangu, hakuna mwenye nia ya kumzingua Mama(Rais). Bali wengi wanapiginia haki na utawala bora wa sheria kitu ambacho ni tishio kubwa kwa Chama Cha Mapinduzi.

Mambo ya kupigania Katiba mpya na utawala bora wa sheria yote yanayoeenda kinyume na agenda za CCM. Chama Cha Mapinduzi hakijajengwa wala hakiishi kwa misingi ya haki na usawa.

CCM imejengwa kwa kutumia dola na kila Rais lazima afundishwe namna bora ya kutumia polisi na taasisi zote kiusalama ili kuhakikisha utawala wa chama hiki.

Ndiyo maana Swala lolote lile linaloenenda kinyume na agenda za CCM mama anaona kama watu wanamzingua nayeye anatumia dola kuwachapa wale wote wanao mzingua.

Ndiyo maana alisema swala la Katiba mpya apewe muda kwanza ajenge kwanza wanchi. Na juzi kwenye mahojiana na BBC Swahili alisema wale wote wanaodai katiba mpya ni kama wanafanya siasa za chokochoko dhidi ya utawala wake.

Katiba mpya sio agenda ya CCM na kamwe haiwezi kuwa agenda yao. Kwasababu hakuna binadamu mwenye akili timamu anayependa kujiua mwenyewe.

Siku ambayo CCM itakakubali agenda ya katiba mpya ndio utakuwa mwanzo wa mwisho wa chama hiki na kusahaulika kama kilichotokea kwa chama cha KANU kilivyosahaulika nchini Kenya.

Mama akiwa kama Mwenyekiti wa chama na Amiri jeshi mkuu lazima afanye jambo la kila namna kulinda chama chake. Njia pekee ambayo mama kama mama anaweza kulinda maslahi ya chama chake ni kuwa Dikiteta.

Hali hii ndiyo inayopelekea matukio ya ajabu ajabu na uonevu mkubwa kwa wale wote wenye mawazo pinzani na CCM na serikali kupata mateso makali. Mbowe kuitwa Gaidi sio jambo la kushangaza kwani ndio option pekee walionayo mkononi kwa sasa.

Hali kama hii itaendelee sana na wengi wetu tutaumia. Ndugu zangu Katiba mpya haitapatikana kwa mapenzi mema ya Chama Cha Mapinduzi bali itapatikana kwa mapenzi na utayari wa watanzania kuipigania katiba mpya kwa nguvu, akili na mali zao.

Nakumbuka kipindi Mama anaingia madarakani niliandika Makala fupi sana na kupost humuhumu Jamii Forumu na kusema “CCM ni ileile’’ unaweza kuisoma ukiingia kwenye profile yangu na hakuna mabadiliko yanayoweza kutoka bila ya mabadiliko ya katiba mpya.

Tatizo sio Magufuli au Mama. Tatizo ni Katiba iliyopo sasa inayoruhusu CCM kujenga mfumo kandamizi kwa washindani wake wa kisiasa. Dawa pekee ya tatizo hili ni Katiba mpya na uwezo wa kupatikana kwa Katiba mpya mpo mikononi mwa watanzania.

“Praise team” mnaosema mama anaupiga mwingi, vipi kashafunga magoli mangapi?

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Anataka kukunwa sasa hivi.
 
Binafsi sikuwahi kuwa shabiki wa utawala wa MWENDAZAKE hususani kwa namna alivyokuwa akitumia nguvu kubwa kuwadhibiti wapinzani wake wa kisiasa lakini upande wa sera za kimaendeleo na uongozi kwa ujumla nadiriki kusema alikuwa chuma tena mwamba kweli kweli..ila kwa huu muda mfupi wa utawala wa mama yangu huyu niwazi taifa langu linapitia kipindi kizito sana sijui nyie wakuu magwiji wa siasa na uongozi mnalionaje hili??mama viatu vimekuwa vikubwa? au apewe muda zaidi baada ya 2025?
 
Tuache kumtegemea "Mtu" badala yake tujikite kwenye "Mfumo" hicho ndicho mimi ninaamini.... Mtu ataondoka... Akiondoka mwenye Falsafa A, atakuja mwingine mwenye Falsafa X - na ni kawaida kabisa kwa binadamu kutofautiana, wala sio ajabu. Ndio maana hakuna Nyerere mwingine, hakuna Sokoine mwingine, hakuna Samwel Sitta mwingine, n.k. Kwahiyo tusitegemee Mama atafanya kama fulani... ni ngumu sana, yeye naye ni binadamu na amelelewa kivyake, ana mtazamo wake, ana maono yake, ana namna yake ya kufanya maamuzi, na ana washauri wake ambao ni tofauti na Mwendazake.

Badala ya kutarajia "Mtu" atatuletea majibu ya changamoto zinazotukabili, nadhani tukubaliane kuwa kuondoka kwa Mwendazake kumetufundisha somo moja kubwa kwamba; tusimtegemee mtu... bali tujikite katika kujenga mfumo imara ambao utamuongoza kila anaeingia bila kujali mapungufu au ubora wake binafsi. Vinginevyo tutaendelea kuimba wimbo huu huu wa "bora alipokuwepo fulani."

Na si mara ya kwanza kutokea: Huenda alipoondoka Mkoloni akaingia Mwalimu, watu huenda walisema "Bora tungeendelea kutawaliwa" - pengine ndio maana akang'atuka! Na yeye alipoondoka akaingia Mzee Ruksa, watu wakasema "Bora.....", na Mzee wa Utandawazi nae huenda aliambiwa "Bora alipokuwepo...." mpaka leo tunaendeleza huo mnyororo. Swali ni, tutaendelea kulaumu mpaka lini?

Au tuchukue tu busara za Nyerere kuwa "Ukizoea kula nyama ya mtu, huwezi kuacha abadani!"
 
Usituulize sisi waulize "waliomuua"
Na kama ulimpenda sana kufa ili uzikwe pembeni ya kaburi lake kama alivyoshauri Ayatollah,,
 
Tuache kumtegemea "Mtu" badala yake tujikite kwenye "Mfumo" hicho ndicho mimi ninaamini.... Mtu ataondoka... Akiondoka mwenye Falsafa A, atakuja mwingine mwenye Falsafa X - na ni kawaida kabisa kwa binadamu kutofautiana, wala sio ajabu. Ndio maana hakuna Nyerere mwingine, hakuna Sokoine mwingine, hakuna Samwel Sitta mwingine, n.k. Kwahiyo tusitegemee Mama atafanya kama fulani... ni ngumu sana, yeye naye ni binadamu na amelelewa kivyake, ana mtazamo wake, ana maono yake, ana namna yake ya kufanya maamuzi, na ana washauri wake ambao ni tofauti na Mwendazake.

Badala ya kutarajia "Mtu" atatuletea majibu ya changamoto zinazotukabili, nadhani tukubaliane kuwa kuondoka kwa Mwendazake kumetufundisha somo moja kubwa kwamba; tusimtegemee mtu... bali tujikite katika kujenga mfumo imara ambao utamuongoza kila anaeingia bila kujali mapungufu au ubora wake binafsi. Vinginevyo tutaendelea kuimba wimbo huu huu wa "bora alipokuwepo fulani."

Na si mara ya kwanza kutokea: Huenda alipoondoka Mkoloni akaingia Mwalimu, watu huenda walisema "Bora tungeendelea kutawaliwa" - pengine ndio maana akang'atuka! Na yeye alipoondoka akaingia Mzee Ruksa, watu wakasema "Bora.....", na Mzee wa Utandawazi nae huenda aliambiwa "Bora alipokuwepo...." mpaka leo tunaendeleza huo mnyororo. Swali ni, tutaendelea kulaumu mpaka lini?

Au tuchukue tu busara za Nyerere kuwa "Ukizoea kula nyama ya mtu, huwezi kuacha abadani!"
Great Thinker!!
 
Na hawezi kurudi..kazi iendelee na mama yenu
 
Acheni kufananisha jiwe na vitu vya..........
 
Back
Top Bottom