MaxShimba
JF-Expert Member
- Apr 11, 2008
- 35,772
- 4,054
Mama aua bintiwe kwa kupata mimba
Written by Administrator
Wednesday, 15 July 2009 15:05
Na Stella Shoo
MKAZI wa Kijiji cha Kilemfua Mokala wilayani Rombo, Kilimanjaro anayefahamika kwa jina la mama Kubwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi Wilayani Rombo kwa tuhuma za kumuua bintiwe kwa kuwa na ujauzito.
Akizungumza na gazeti hili jana asubuhi kwa njia ya simu, Diwani wa Kata ya Kemfua Mokala, Bw. Festo Kilawe alisema tukio hilo lilitokea Jumamosi saa 3:00 usiku.
Bw. Kilawe alimtaja marehemu kuwa ni Bi. Lilian Mrema ambapo
alisadikiwa kuwa na ujauzito wa karibu miezi 6 na kuwa mama mzazi wa Bi. Liliani alikuwa hataki ujauzito wa mawanae huyo.
"Ndugu mwandishi huyu mama alikuwa na ugomvi wa mara kwa mara na marehemu huyu baada ya kuona kuwa ana ujauzito,sasa ilipofika usiku huo wa Jumamosi alimfuata marehemu chumbani kwake na kuanza kumshambulia kwa mwiko hapo marehemu alipiga kelele majirani walipofika alikuwa ameumia vibaya,sasa wakati anapelekwa hospitali ndipo alipofariki, " alisema Bw. Kilawe.
Alisema baada ya kutokea kwa tukio hili ndio majirani walipotoa
taarifa katika Kituo cha Polisi cha Rombo na mtuhumiwa alikamatwa na kutiwa mbaroni kwa tuhuma za mauaji.
"Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Huruma na mtuhumiwa amekamatwa na Polisi na sasa yupo chini ya ulinzi na kuwa upelelezi unaendelea utakapokamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu shitaka la mauaji"alifafanua Bw. Kilawe
Written by Administrator
Wednesday, 15 July 2009 15:05
Na Stella Shoo
MKAZI wa Kijiji cha Kilemfua Mokala wilayani Rombo, Kilimanjaro anayefahamika kwa jina la mama Kubwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi Wilayani Rombo kwa tuhuma za kumuua bintiwe kwa kuwa na ujauzito.
Akizungumza na gazeti hili jana asubuhi kwa njia ya simu, Diwani wa Kata ya Kemfua Mokala, Bw. Festo Kilawe alisema tukio hilo lilitokea Jumamosi saa 3:00 usiku.
Bw. Kilawe alimtaja marehemu kuwa ni Bi. Lilian Mrema ambapo
alisadikiwa kuwa na ujauzito wa karibu miezi 6 na kuwa mama mzazi wa Bi. Liliani alikuwa hataki ujauzito wa mawanae huyo.
"Ndugu mwandishi huyu mama alikuwa na ugomvi wa mara kwa mara na marehemu huyu baada ya kuona kuwa ana ujauzito,sasa ilipofika usiku huo wa Jumamosi alimfuata marehemu chumbani kwake na kuanza kumshambulia kwa mwiko hapo marehemu alipiga kelele majirani walipofika alikuwa ameumia vibaya,sasa wakati anapelekwa hospitali ndipo alipofariki, " alisema Bw. Kilawe.
Alisema baada ya kutokea kwa tukio hili ndio majirani walipotoa
taarifa katika Kituo cha Polisi cha Rombo na mtuhumiwa alikamatwa na kutiwa mbaroni kwa tuhuma za mauaji.
"Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Huruma na mtuhumiwa amekamatwa na Polisi na sasa yupo chini ya ulinzi na kuwa upelelezi unaendelea utakapokamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu shitaka la mauaji"alifafanua Bw. Kilawe