Malori chakavu ni chanzo kikubwa cha ajali

Mparee2

JF-Expert Member
Sep 2, 2012
2,586
4,274
Kwa watu wanaosafiri kwa magari mara kwa mara watakubaliana na mimi kuwa, madereva wa Malori ni kati ya madereva walio iva kimafunzo pengine kuliko kundi lingine lolote barabarani.

Huwa wapo makini, waangalifu, na hawafanyi maamuzi ya hovyo hovyo kama hawa wengine wanao tusafirisha.

TATIZO; WANAENDESHA MALORI CHAKAVU!

Nafikiri ipo haja ya Serikali kuangalia upya vigezo vya malori yanayo agizwa na kuingia Nchini. Lori sijui limetembea kms milioni tano hilo ni scraper kabisa halafu tunategemea likapande milima ya Kitonga!!!!

Kuhusu Leseni za Madereva wa malori; hata kwa akili ya kawaida, sio rahisi kwa mmiliki kumpa dereva kanjanja akaendeshe Lori la shs milioni 700 + eti akiwa na leseni ambayo haieleweki; wazungu husema " it doesn't connect....na maanisha, leseni zao sio changamoto....

KWA KUWASAIDIA - kwa waombaji wapya, Leseni za daraja C mngeongeza kigezo cha ufaulu wa elimu ya kawaida ili kupima uelewa. Udereva wa abiria ni kazi na sio ubabaishaji.....

Najua visabisha ajali vipo vingi ila kwa leo nimeongelea uchakavu wa malori kwani kwa kiasi kikubwa ndio yamekuwa yanaua watu wengi kwa pamoja
 
Vipuri/Spea feki.
Barabara nyembamba.
Ukaguzi hafifu uliojaa rushwa.
Watumiaji wengi wa barabara kutozingatia Sheria hasa bodaboda/Hawana elimu ya udereva bali ni waendeshaji.
Ulevi. Ni vyanzo vikuuu vya Ajali
 
Factors ziko nyingi jombaa, ata hizi barabara zetu ni hatari sana. Mathalani magari mawili kupishana yakiwa kwenye speed kali is very deadly
Na hapo ndio sababu nimependekeza kuongeza kipimo cha uelewa (ufaulu wa elimu ya kawaida ya darasani) na sio class C pekee ambapo kwa sasa kila mtu anayeweza kusoma na kuandika anaipata
Ukiwa barabarani utaona watu wanaendesha kwa KUPIGA RAMLI kutokana na uelewa mdogo
Mfano: mtu anakata kona speed akifikiri tu huko mbele kuko salama. Ana ng'ang'ana kuovertake wakati anaona barabara nyembamba, Anaovertake kwenye Kona kwa kutegemea miujiza ya Mungu, Anawasha full light kwa kujiwazia yeye mwenyewe nk nk nk
Suluhisho ni sifa za kupata leseni class C ziongezwe ili ziendane na Uzito/umuhimu wa kazi mtu anayokwenda kufanya. Kubeba Abiria (uhai wa watu wengi) haihitaji watu wa kupiga Ramli/bahati nasibu!!!
 
Kwa watu wanaosafiri kwa magari mara kwa mara watakubaliana na mimi kuwa, madereva wa Malori ni kati ya madereva walio iva kimafunzo pengine kuliko kundi lingine lolote barabarani. Huwa wapo makini, waangalifu, na hawafanyi maamuzi ya hovyo hovyo kama hawa wengine wanao tusafirisha......
TATIZO; WANAENDESHA MALORI CHAKAVU!
Nafikiri ipo haja ya Serikali kuangalia upya vigezo vya malori yanayo agizwa na kuingia Nchini.
Lori sijui limetembea kms milioni tano hilo si scraper kabisa
Hata kwa akili ya kawaida, sio rahisi kwa mmiliki kumpa dereva kanjanja akaendeshe gari lake la shs milioni 700 + eti akiwa na leseni ambayo haieleweki; wazungu husema " it doesn't connect....
KWA KUWASAIDIA - kwa waombaji wapya, Leseni za daraja C wangeongeza kigezo cha Elimu ya kawaida ili kupima uelewa
Najua visabisha ajali vipo vingi ila kwa leo nimeongelea uchakavu wa malori kwani kwa kiasi kikubwa ndio yamekuwa yanaua watu wengi kwa pamoja
tuepuke pia kufanya vijiwe pembeni ya barabara
utakuta wasukuma wamekaa kwenye taa za solar pembeni ya barabara wanapiga story
 
Kwa watu wanaosafiri kwa magari mara kwa mara watakubaliana na mimi kuwa, madereva wa Malori ni kati ya madereva walio iva kimafunzo pengine kuliko kundi lingine lolote barabarani. Huwa wapo makini, waangalifu, na hawafanyi maamuzi ya hovyo hovyo kama hawa wengine wanao tusafirisha......
TATIZO; WANAENDESHA MALORI CHAKAVU!
Nafikiri ipo haja ya Serikali kuangalia upya vigezo vya malori yanayo agizwa na kuingia Nchini.
Lori sijui limetembea kms milioni tano hilo si scraper kabisa
Hata kwa akili ya kawaida, sio rahisi kwa mmiliki kumpa dereva kanjanja akaendeshe Lori la shs milioni 700 + eti akiwa na leseni ambayo haieleweki; wazungu husema " it doesn't connect....
KWA KUWASAIDIA - kwa waombaji wapya, Leseni za daraja C wangeongeza kigezo cha ufaulu wa elimu ya kawaida ili kupima uelewa
Najua visabisha ajali vipo vingi ila kwa leo nimeongelea uchakavu wa malori kwani kwa kiasi kikubwa ndio yamekuwa yanaua watu wengi kwa pamoja
Malori yenyewe wanauziana humu humu bongo. Matajiri wengi uchwara
 
ndio sababu watu wengi walishauri kuwe na wakati pekee wa mabasi na malori kusafiri,mabasi mchana na malori usiku.

hapa ingekuwa rahisi sana kutadhmini kwa macho ni kundi gani la madereva hawajitambui,video zote za rough barabarani utakuta ni mabasi dhidi ya malori na mabasi mengine.

nahisi matajiri wanakuwa makini na wanaowapa dhamana maana inaonekana kurudisha faida kwa biashara ya maroli ni miaka mingi tofauti na bus,miaka 3 tu pesa imerudi.
 
Na hapo ndio sababu nimependekeza kuongeza kipimo cha uelewa (ufaulu wa elimu ya kawaida) na sio class C pekee....
Ukiwa barabarani utaona watu wanaendesha kwa KUPIGA RAMLI kutokana na uelewa mdogo........ mtu anakata kona speed akifikiri tu huko mbele kuko salama. Ana ng'ang'ana kuovertake wakati anaona barabara nyembamba nk nk nk

Umeandika kama una vinasaba na huyu ndugu:

FW9WY_7WAAAAxoa.jpeg
 
Factors ziko nyingi jombaa, ata hizi barabara zetu ni hatari sana. Mathalani magari mawili kupishana yakiwa kwenye speed kali is very deadly
Hili la barabara nyembamba ni hatari sana. Ina maana kosa kidogo tu tayari magari yanavaana. Na siyo kama serikali haina uwezo wa kujenga njia mbili mbili kwenye barabara zote muhimu. Pia magari mabovu (mimi siiti chakavu kwa sababu gari linaweza kuwa la zamani lakini likawa zima). Funga kazi ni uendeshaji mbovu na madereva wasio na mafunzo bila kusahau ulevi. All in all, njia mbili mbili zinaweza kupunguza ajali kwa asilimia kubwa.
 
Back
Top Bottom