Malisa Godlisten
JF-Expert Member
- Jan 20, 2010
- 202
- 1,588
Ndugu zangu, Muda huu (mchana wa leo Disemba 20, 2025) askari wenye silaha wapo nyumbani kwa wazee wangu, kijiji cha Old Moshi Kidia. Leo wameenda na magari mawili, yenye namba za usajili.
Wamemuweka mama yangu mzazi(70) chini ya ulinzi na wamemnyang'anya simu. Majirani walioenda kushuhudia, nao wamewekwa chini ya ulinzi!
Tumewasiliana na Mwenyekiti wa Kijiji ili aende kujua nini kinaendelea lakini naye sasa hapatikani (bila shaka nae kawekwa chini ya ulinzi). Mpaka sasa hatujui nini kinaendelea.
Nalaani vikali tukio hili la kinyama. Ikiwa Polisi wananitafuta mimi, zipo njia nyingi wanaweza kutumia zilizowekwa kwa mujibu wa Sheria za Nchi kuliko kuwaghasi wazazi wangu ambao ni wazee. Huu ni unyama na haukubaliki
Tukio hili limetokea leo baada ya jana kutoa taarifa ya watu wasiojulikana (ambao hawakujitambulisha wala kuwa na magari yenye namba) kuvamia nyumbani usiku wa manane na kukata umeme.
Marafiki zetu ambao ni mawakili waliopo Moshi wanaelekea kijijini kutoa msaada wa kisheria. Naomba watu wa Old Moshi Kidia muende kwa wingi hapo nyumbani kujua kinachoendelea.
Uovu huu usikaliwe kimya!
Wamemuweka mama yangu mzazi(70) chini ya ulinzi na wamemnyang'anya simu. Majirani walioenda kushuhudia, nao wamewekwa chini ya ulinzi!
Tumewasiliana na Mwenyekiti wa Kijiji ili aende kujua nini kinaendelea lakini naye sasa hapatikani (bila shaka nae kawekwa chini ya ulinzi). Mpaka sasa hatujui nini kinaendelea.
Nalaani vikali tukio hili la kinyama. Ikiwa Polisi wananitafuta mimi, zipo njia nyingi wanaweza kutumia zilizowekwa kwa mujibu wa Sheria za Nchi kuliko kuwaghasi wazazi wangu ambao ni wazee. Huu ni unyama na haukubaliki
Tukio hili limetokea leo baada ya jana kutoa taarifa ya watu wasiojulikana (ambao hawakujitambulisha wala kuwa na magari yenye namba) kuvamia nyumbani usiku wa manane na kukata umeme.
Marafiki zetu ambao ni mawakili waliopo Moshi wanaelekea kijijini kutoa msaada wa kisheria. Naomba watu wa Old Moshi Kidia muende kwa wingi hapo nyumbani kujua kinachoendelea.
Uovu huu usikaliwe kimya!
