mike2k
JF-Expert Member
- May 12, 2016
- 1,458
- 3,127
Huyu dogo ameanza kuchanganyikiwa. Moshi ilianza kuendelea zamani za pontio pilato kabla ya ujio wa Dr.Livingstone na Gavana Edward Twining.
Mwaka 1902 barabara zinazounganisha mitaa mbalimbali ya Moshi zilikuwa na lami, enzi hizo CCM haijazaliwa, mama yake TANU wala bibi yake TAA.
Mwaka 1895 Ikulu ya kwanza ya kisasa ya Mangi mkuu wa wachagga ilijengwa eneo la KDC Moshi. Ikulu hiyo hadi sasa ndiyo inayotumika kama Ikulu ndogo ya Rais akija mkoani Kilimanjaro.
Mwaka 1917 dola ya wachagga ilikuwa na mfumo rasmi wa serikali na baraza la mawaziri, ikiwa ni pamoja na ofisi na magari kwa watendaji waandamizi wakiwemo mawaziri. Ofisi za mawaziri ndio zinatumika leo kama ofisi za halmashauri ya wilaya ya Moshi.
Miaka 100 iliyopita Moshi kulikuwa na viwanda mbalimbali kikiwemo kiwanda kikubwa zaidi cha kubangua kahawa eneo la Afrika Mashariki. Mwaka 1940 dola ya wachagga tayari ilikuwa na gazeti lake (Komkya), lililokuwa likisomwa maeneo yote ya wachagga kuanzia Siha hadi Rongai. Gazeti hilo liliandikwa kwa lugha ya Kiswahili.
-
Kufikia mwaka 1950 karibu kila kata au tarafa ilikuwa na shule ya sekondari, zahanati au kituo cha afya pamoja na kanisa la kisasa, kuanzia Siha mpaka Tarakea. Sio zote lakini nyingi zilikuwa na shule zilizojengwa na wamisionari miaka mingi sana iliyopita.
Wakati chakubanga na babu yake wanatembea kilomita 50 kwenda kuchoma chanjo ya tetekuwanga, wazee wa kichagga walikua wakipata huduma za afya kwenye vituo vya afya vya mission vilivyopo kwenye kata/tarafa zao.
Leo mtu mmoja pengine kwa sababu ya kukosa chanjo ya pepopunda anaropoka kwamba maendeleo ya Moshi yameletwa na CCM? What a shame.!!
-
Kimsingi CCM na serikali yake zimezorotesha maradufu maendeleo ya Moshi kuliko wakati mwingine wowote katika historia. Moshi ya wakati ule (kama dola yenye mamlaka kamili), na Moshi ya leo (kama wilaya) ni vitu viwili tofauti. Moshi ingeachwa kuwa dola huru kama ilivyokuwa zamani, ingekuwa na maendeleo maradufu kuliko leo.
Halafu kama kweli CCM inaleta maendeleo, mbona kuna mikoa haijawahi kuchagua upinzani na bado haina maendeleo? Kwanini maendeleo hayo CCM isipeleke kwenye ngome zake? Next time mwambieni kabla hajabwatuka ajifunze historia kdg.!!!!!!!!!
Source instagram:Malisa_gj
Last edited by a moderator: