Nimebahatika kutembelea jijini Mwanza mwisho wa mwaka huu na nimekutana na kitu cha ajabu ambacho sijawahi kukiona duniani kokote kuhusu jinsi ya kulipia maegesho ya gari. Mtu anakuja kuscan plate number yako bila hata wewe kujua, hivyo ni wajibu wako kujua hata kama ni mgeni kuwa unatakiwa kulipa sh 1500 kupitia mtandao hata kama umekaa dakika 30.
Kwa hili wadau wa TARURA ni mnaonea tafuteni njia mbadala ila si kwa kiwango hicho ambacho nacho usipolipa crossing the third day faini inakuwa elfu 20. Sijui mnapotunga hizi sheria huwa mnafikiliaje in other side.
Yaani parking Mwanza kwa mwezi ni sh 45,000/=. Utaratibu wenu wa kujua mtu anadaiwa nao ni mbovu au basi mkiscan plate no muweke TRA receipt ili mhusika akija anaona kuwa ana deni.
Ni hayo tu TARURA Mwanza ila nawaomba tu mkaribishe watu watoe maoni ili kuboresha haya makusanyo, less to this kwanza mnaipotezea Serikali mapato before mtu ukipaki 1 hour unalipa 500 na mimi kwa budget yako one hrs ilitosha sana kukaa town.
Zipo kesi nyingi huko, baada siku 3,1500 ada ya siku inakuwa 20,000! Baada ya mwezi 200,000.....Wizi wa ajabu. Mara nyingi wanatapata sms 1500.....wachache, Tin no. ina match majina
Nchi imefilisika "MAARIFA" ya ukusanyaji mapato, huko tunapoelekea kama taifa mtu hata "UKIJAMBA" utaambiwa ulipie malipo ya "SUMATRA, HALAMASHAURI, TARURA, KUTUNZA MAZINGIRA" na uoneshe risiti ya EFD.
Zipo kesi nyingi huko, baada siku 3,1500 ada ya siku inakuwa 20,000! Baada ya mwezi 200,000.....Wizi wa ajabu. Mara nyingi wanatapata sms 1500.....wachache, Tin no. ina match majina
Sasa hii kinachotafutwa ni nini? Yaani from 1500 to elfu 20 to laki 2, daaah kunawatu wanapata pesa kirahisi sana na hapo hakuna ulinzi wa gari ukipaki. Au tuwe tunagonga daladala tu