Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,650
- 218,119
Hakuna asiyefahamu kwamba 2015 ccm ilikataliwa Jijini Dar es Salaam , madiwani wengi na wabunge wengi wa Upinzani walichaguliwa na wananchi , Meya wa Manispaa ya Kinondoni akatokana na wapinzani , Meya wa Ilala vivyo hivyo ikiwa ni pamoja na Meya wa Jiji .
Mengi yalitokea ikiwa ni pamoja na ccm kuleta madiwani mamluki kutoka Mchambawima na Kisiwandui ili kuja kuongeza idadi ya wapiga kura za kuchagua Meya wa jiji , hata hivyo wakaangukia pua , ili maneno yasiwe mengi ngoja nijikite Kinondoni , baada ya CCM kushindwa Kinondoni ikaamua kupanga njama za kuigawa Manispaa hiyo kwenye makundi mawili , huu mpango ulikuwepo ila uliharakishwa kwa makusudi maalum ili kuibeba CCM, pamoja na kuigawanya Kinondoni lakini bado kura za CCM zikawa hazitoshi pande zote mbili , ndipo ukafanyika umafia wa kuwahamisha kibabe madiwani wa Upinzani waliokuwa na haki ya kubaki kinondoni na kuwapeleka Ubungo , wakaletwa na mamluki wa kuteuliwa ili kuiongezea nguvu CCM na Hatimaye Benjamin Sitta akawa Meya kwa njia ya dhuluma iliyoacha manung'uniko makubwa sana .
Labda kwa ajili ya kuweka kumbukumbu vizuri ni kwamba ccm ililazimisha umeya wa Kinondoni ili kuongeza wigo wa wizi na upigaji , ushahidi ni hili la Kinondoni la kujenga Coco Beach kwa Bil 14 , huu ni wizi wa mchana , sasa hili ni moja vipi kuhusu miradi mingine ?
Benjamin Sitta ulipewa Umeya kimafia kwa huruma ya baba yako , hukuwa na uwezo wowote na wala hukuwahi kuwa na uwezo kokote ulikopita , Sasa wamekutumia na wanajiandaa kukung'oa ili kuua soo .
Kila lenye mwanzo halikosi mwisho .
Mengi yalitokea ikiwa ni pamoja na ccm kuleta madiwani mamluki kutoka Mchambawima na Kisiwandui ili kuja kuongeza idadi ya wapiga kura za kuchagua Meya wa jiji , hata hivyo wakaangukia pua , ili maneno yasiwe mengi ngoja nijikite Kinondoni , baada ya CCM kushindwa Kinondoni ikaamua kupanga njama za kuigawa Manispaa hiyo kwenye makundi mawili , huu mpango ulikuwepo ila uliharakishwa kwa makusudi maalum ili kuibeba CCM, pamoja na kuigawanya Kinondoni lakini bado kura za CCM zikawa hazitoshi pande zote mbili , ndipo ukafanyika umafia wa kuwahamisha kibabe madiwani wa Upinzani waliokuwa na haki ya kubaki kinondoni na kuwapeleka Ubungo , wakaletwa na mamluki wa kuteuliwa ili kuiongezea nguvu CCM na Hatimaye Benjamin Sitta akawa Meya kwa njia ya dhuluma iliyoacha manung'uniko makubwa sana .
Labda kwa ajili ya kuweka kumbukumbu vizuri ni kwamba ccm ililazimisha umeya wa Kinondoni ili kuongeza wigo wa wizi na upigaji , ushahidi ni hili la Kinondoni la kujenga Coco Beach kwa Bil 14 , huu ni wizi wa mchana , sasa hili ni moja vipi kuhusu miradi mingine ?
Benjamin Sitta ulipewa Umeya kimafia kwa huruma ya baba yako , hukuwa na uwezo wowote na wala hukuwahi kuwa na uwezo kokote ulikopita , Sasa wamekutumia na wanajiandaa kukung'oa ili kuua soo .
Kila lenye mwanzo halikosi mwisho .