Wanafunzi wa kike wakisubiri usafiri jijini Dar es Salaam, wanafunzi wengi wamekuwa wakijichelewesha vituoni, huku wakidaiwa kuchagua mabasi ya kupanda. Picha na Sunday George
Wakati uzoefu ukionyesha walimu kuwanyanyasa kijinsia wanafunzi wao wa kike, imebainika katika baadhi ya nyakati wapo wasichana wanaowaweka walimu wao kwenye wakati mgumu.
Uchunguzi wa Mwananchi umebaini kuwa malezi duni ya wanafunzi hao, ugumu wa maisha wanaopitia baadhi yao, yanawasukuma wasichana kujihusisha na uhusiano wa kimapenzi sio tu na walimu wao, lakini hata watu wengineo wakiwamo makondakta.
Kwa mujibu wa uchunguzi, kuna matukio kadhaa ya wanafunzi wa kike kuwataka kimapenzi walimu na watu wengineo, wakitumia njia ya kujirahisisha ili kukidhi mahitaji yao yakiwamo hata ya kimaisha.
Mwananchi