Malecela avunja ukimya!

KLHN Wire
Alipoulizwa kuhusu mipango yake ya kisiasa ya baadaye na hasa kama ataingia tena katika kinyang'anyiro cha kugombea Urais Mzee Malecela alisema kuwa imekuwa ni utamaduni ndani ya CCM kwa Rais aliyeko madarakani kuachwa kukamilisha vipindi viwili vinavyoruhusiwa kikatiba na hivyo mpango huo kwake kwa mwakani haupo. Hata hivyo alionesha kuwa ana mpango wa kuendelea kulitetea jimbo lake la Mtera ambalo ameliongoza kwa karibu miaka 40 sasa.

Utamaduni huu wa kumuachia mgombea wa CCM akae madarakani kwa awamu mbili inabidi upigwe vita hasa pale ambapo kuna ushahidi wa kutosha kwamba yule aliye madarakani hastahili kupewa awamu nyingine. Kikwete Urais umemshinda hivyo huu utamaduni ndani ya CCM inabidi usitishwe haraka sana kwa maslahi ya nchi.
 
Hata hivyo alionesha kuwa ana mpango wa kuendelea kulitetea jimbo lake la Mtera ambalo ameliongoza kwa karibu miaka 40 sasa.

Malecela amekuwa mbunge wa Mtera kwa miaka 40?
 
Ingawa ukilinganisha na vigogo wengi wa CCM, huyu angeweza kuwa na moral authorty (mamlaka ya kimaadili) ya kukemea -- bila kutafuna maneno... Lakini hajafanya hivyo kabisa, amekaa kimya tu kama mtu mwenye woga mkubwa -- utadhani anaogopa naye mdhambi yake ya ufisadi yatakuja kutolewa hadharani...

Hasemi lakini anatenda chinichini na hiyo ni moja ya dhambi zake kubwa
 
Kiranga,

Miaka 40 kweli not fair! Lini tutawapa nafasi wengine vijana?

Mtu nakuwa mbunge miaka 40???

taratibu na katiba yetu ina matatizo!

That was a question Mzalendohalisi, not a statement, not even a rhetoric question.

Rekodi za bunge hizi hapa

Chama Cha Mapinduzi-CCM Member of Parliament of Tanzania 1995 2010
Commonwealth Group-South Africa Appointed Member 1985 1986
Chama Cha Mapinduzi - CCM Vice Chairman - Tanzania Mainland 1977 2007
Chama Cha Mapinduzi-CCM Member of Parliament of Tanzania 1975 1985

Miaka 40 inatoka wapi? Wandishi wakikosea vitu kama hivi tutawaamini vipi katika vitu vingine vilivyojificha zaidi? Miaka 40 iliyopita kulikuwa na jimbo la Mtera? Miaka 40 iliyopita ni 1969, Malecela alikuwa mbunge wa Mtera 1969? Muandishi kwa kutofafanua anaonyesha kuwa Malecela amekuwa mbunge wa Mtera kutoka 1969 mpaka leo, hii ni kweli?
 
- Ahsante kwa member aliyenifahamisha kuhusu huu mjadala kuwepo, ni mjadala mwema na naona wananchi wanatoa mawazo yao ya kulisaidia taifa letu,

- Ila mimi kwangu naomba nisamahewe maana ndio mambo yenyewe haya ya conflict of interest,

- Lakini so far so good naona the main theme ni kwamba next uchaguzi wananchi wa Tanzania tutakuwa na mapya kuliko hawa wzee na CCM maana hawana mapya na wote ni mafisadi, fair analysis.

Mjadala mwema.

william.
 
That was a question Mzalendohalisi, not a statement, not even a rhetoric question.

Rekodi za bunge hizi hapa

Chama Cha Mapinduzi-CCM Member of Parliament of Tanzania 1995 2010
Commonwealth Group-South Africa Appointed Member 1985 1986
Chama Cha Mapinduzi - CCM Vice Chairman - Tanzania Mainland 1977 2007
Chama Cha Mapinduzi-CCM Member of Parliament of Tanzania 1975 1985

Miaka 40 inatoka wapi? Wandishi wakikosea vitu kama hivi tutawaamini vipi katika vitu vingine vilivyojificha zaidi? Miaka 40 iliyopita kulikuwa na jimbo la Mtera? Miaka 40 iliyopita ni 1969, Malecela alikuwa mbunge wa Mtera 1969? Muandishi kwa kutofafanua anaonyesha kuwa Malecela amekuwa mbunge wa Mtera kutoka 1969 mpaka leo, hii ni kweli?

Kiranga, ukitaka kusahihisha unasahihisha tu. Kama ulivyofanya hapo juu na kama masahihisho tutayafanya na wala si mbingu kupasuka. Kama huwezi kuwaamini waandishi, hulazimiki kuwaamini. Katika habari kupata facts zisizosahihi inatokea.

Ninachojua Malecela alikuwa Waziri (sina uhakika) kuanzia mwaka 1969. Sasa kama alikuwa anawakilisha jimbo hilo hilo la Mtera ya sasa au la zamani na kwa muda gani ni mambo ambayo yanaweza kutolewa hapa. NI wakati gani Malecela hakuwa Mbunge kati ya 1969-2009?
 
William...can you please at least tell us for how long the Honourable Malecela has been an MP? I see no conflict of interest there, sir.
 
John Samuel Malecela (born 1934) in Bugiri Dodoma, was Prime Minister of Tanzania from 1990-11-09–1994-12-07. He was born in Bugiri, Dodoma.

* Secondary Education - Minaki secondary school 1957-1958
* Bachelor of Commerce - Bombay University 1958-1959
* Post Graduate Studies - Cambridge University 1961-1962
* Ph.D. Honoris Causa (Humanities) - Texas University 1977

Positions held

* Tanzania Permanent Representative to the United Nations - 1964-1966
* Tanzanian Ambassador to Ethiopia and the OAU - 1967
* Minister of Foreign Affairs - 1972-1973
* Communication and Transport - 1973-1974
* Mineral Resources and Agriculture 1975-1975
* Minister in the East African Community - 1975-1976
* Regional Commissioner of Iringa - 1980-1984
* Member of the Group of Eminent Persons of the Commonwealth on South African situation - 1985
* Tanzanian High Commissioner to the United Kingdom - 1989-90
* Prime Minister and First Vice President 1990-1994
* Vice Chairman of the ruling Party, Chama cha Mapinduzi (CCM) - 1995 to 2007
* Member of Parliament for Mtera - 1990 to date
 
Kiranga, ukitaka kusahihisha unasahihisha tu. Kama ulivyofanya hapo juu na kama masahihisho tutayafanya na wala si mbingu kupasuka. Kama huwezi kuwaamini waandishi, hulazimiki kuwaamini. Katika habari kupata facts zisizosahihi inatokea.

Kuna tofauti kati ya kusahihisha na kutaka ufafanuzi. Kuna maswali yameibuka ambayo hata mimi sina majibu yake, lakini yanaleta utata kwenye habari, ni wajibu kutaka kupata kitu kinachoeleweka.Kama habari haiwezi kupata kitu basic kama timeline ya career ya Malecela right utalaumu watakaosema kuwa mwandishi hayuko makini na pengine amekosea mengine? tatizo si kwamba siwezi kuwaamini waandishi, tatizo waandishi wenyewe wanajivunjia kuaminika kwa kuleta stories zilizokuwa half baked, ambazo zinashindwa kupata kitu basic kama timeline sawa, halafu baada ya hapo, badala ya kuomba kunradhi na kushukuru kwa kupewa heshima ya kukosolewa kama waandishi wa kweli wanapata audacity na temerity ya kusema "wala mbingu si kupasuka" wapi journalistic integrity? Unashindwa kuandika, sawa, pengine hujapata this or that fact right, unashindwa hata uungwana wa kusema kunradhi nilikosea basi? Au hata kusema sikukosea hii hapa source yangu?


Ninachojua Malecela alikuwa Waziri (sina uhakika) kuanzia mwaka 1969. Sasa kama alikuwa anawakilisha jimbo hilo hilo la Mtera ya sasa au la zamani na kwa muda gani ni mambo ambayo yanaweza kutolewa hapa. NI wakati gani Malecela hakuwa Mbunge kati ya 1969-2009?

Ukishasema "ninachojua...." huwezi kusema tena "sina hakika", hivi vitu viwili viko mutually exclusive, ukijua una hakika na ukiwa huna hakika huna kujua, kwa hiyo hii dhana nzima ya "ninachojua.. (sina hakika)" inaonyesha ulivyo na standards ndogo, kwamba una consider unajua kitu usicho na hakika nacho, kwamba unaweza kutuandikia uzushi ukasema unajua, si unajua lakini huna hakika bwana?

Mimi nimekupa rekodi za bunge hizo hapo, na nilishasema tangu juu kwamba hili ni swali na si statement, kwa hiyo kama wewe una rekodi zenye kupinga hizo kuonyesha Malecela alikuwa mbunge wa Mtera kutoka 1969 mpaka sasa tuonyeshe.
 
Nadhani amekuwa Mbunge wa Mtera kuanzia mwaka 1990. Kabla ya hapo (1989-1990) alikuwa Balozi wetu Uingereza.
Pia, Mtera ni jimbo la miaka ya karibuni, halikuwepo mwaka 1969.
 
William...can you please at least tell us for how long the Honourable Malecela has been an MP? I see no conflict of interest there, sir.

- Sure, nitasema kwa haraka haraka meaning ninaweza kukosea pia, amekuwa waziri wa Mawasiliano na fedha wa East African Community kati ya 1968 na 1972, akawa waziri wa nje mpaka 1975, akagombea ubunge wa Dodoma vijijini akashinda na kuwa waziri wa Kilimo, Mwaka 1980 akagombea ubunge wa Chilonwa baada ya jimbo la Dodoma vijijini kukatwa, akashinda na kuwa mbunge tena mpaka 1985, alipogombea tena akashindwa hakuwa mbunge tena mpaka 1990 alipogombea jimbo jipya la Mtera na kushinda amekua mbunge wake hadi leo.

- Amekuwa mbunge kuanzia 1975-1980, baadaye 1990 -2009 = 40?

- Je hii inasaidia au?

Ahsante.

William.
 
Last edited:
Hahhahandio yule yule jumanne aliemuoaa tatu ntimizi ili aje awe Pres kibaraka wa iran...leo anawageuka wenzake??hahaa haya ngojatusubiri jibu lake
 
Kiranga, ukitaka kusahihisha unasahihisha tu. Kama ulivyofanya hapo juu na kama masahihisho tutayafanya na wala si mbingu kupasuka. Kama huwezi kuwaamini waandishi, hulazimiki kuwaamini. Katika habari kupata facts zisizosahihi inatokea.

Ninachojua Malecela alikuwa Waziri (sina uhakika) kuanzia mwaka 1969. Sasa kama alikuwa anawakilisha jimbo hilo hilo la Mtera ya sasa au la zamani na kwa muda gani ni mambo ambayo yanaweza kutolewa hapa. NI wakati gani Malecela hakuwa Mbunge kati ya 1969-2009?

Kipindi alichopigwa chini ubunge na uwaziri akaenda kuwa mkuu wa mkoa wa iringa, tume ya kina Obasabjo au Adedeji, ilikuwa seven people wanafanya vitu flani siukumbuki alafu akaenda kuwa balozi ndio mwinyi akamchukua toka Uingereza kumpa ubunge wa kuteuliwa na kuwa waziri mkuu.....i hope memory yangu ipo right.
 
Mzalendo umeniwahi tu hapo.. nilikuwa najaribu kujumlisha miaka hiyo..kwa hiyo ni mbunge karibu miaka mingapi (ukijumlisha na hii ya sasa)?
 
KLHN Wire

Mbunge wa Mtera Mhe. John S. C Malecela amevunja ukimya wake wa muda mrefu ..................... Amesema kuwa endapo malumbano hayo yataendelea basi ataenda hatua mbele zaidi ya kuzungumza kwenye vikao vya chama akitahadharisha kuwa CCM haitosita kumtimua mtu yeyote ambaye chama kinaona haendani nacho. Alitoa mifano ya huko nyuma jinsi CCM ilivyoshughulikia uasi ndani ya CCM ambapo baadhi ya viongozi wake (wabunge) walichukuliwa hatua.

Akikumbushia maneno ya Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kuwa "upinzani madhubuti utatoka CCM" mzee Malecela aliwahakikishia wananchi kuwa bado CCM kina muda mrefu wa kutawala na hakuna mtu au kikundi ambacho kinaweza kutoka na kusababisha chama hicho kumeguka.

.........................

Najaribu kuelewa hapa:

Kwa hiyo ukileta upinzani ndani ya CCM, utatimuliwa kwani huendani nacho.
Ila pia, anamuenzi Mwalimu kuwa upinzani wa kweli utatoka CCM.......how? Kwa kutimuliwa? Kama umetimuliwa, basi hauko ndani ya CCM tena. Vinginevyo akina Maalim, Mrema, Mapalala na wapinzani wengi basi bado ni CCM!

Nimesoma taarifa ya KLHN hapo juu, naona japo Mzee kasema mengi lakini bado hajasema kitu. Mama na mtoto, by proxy, wanasema mengi muhimu na mazito.

Kwa jinsi ninavyomfahamu na kumuheshimu Mzee, nadhani angechukua mwelekeo wa akina Kawawa na Mwinyi (You can swim in the ocean, but you don't have to swim with sharks).
 
Kipindi alichopigwa chini ubunge na uwaziri akaenda kuwa mkuu wa mkoa wa iringa, tume ya kina Obasabjo au Adedeji, ilikuwa seven people wanafanya vitu flani siukumbuki alafu akaenda kuwa balozi ndio mwinyi akamchukua toka Uingereza kumpa ubunge wa kuteuliwa na kuwa waziri mkuu.....i hope memory yangu ipo right.

- Naomba kukusaidia mkuu,

1985 alishindwa ubunge, akaenda kuwa Balozi Maalum wa Tanzania katika usuluhishi wa mali za EAC, baada ya hapo akaenda London/Lagos kwenye ECOWAC kundi la viongozi saba waliopewa jukumu la kutayarisha mabadiliko ya uhuru wa South Africa na kuishia kumtoa Mandela jela, alipomaliza hiyo akaenda kuwa RC Iringa, ndipo akahamishiwa Ubalozi UK na hatimaye kurudi kuwa Waziri Mkuu,

- Ila haukuwa mbali sana na ukweli.

Ahsante.


William.
 
Back
Top Bottom