kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 9,000
- 17,909
Jihad al Islami: Kambi ya muqawama haitoruhusu adui kuwa na utulivu
Msemaji wa harakati ya Jihad al Islami ya Palestina amegusia mazungumzo yaliyofanyika baina ya wakuu wa kambi ya muqawama huko Beirut Lebanon na kusisitiza kuwa, kambi ya muqawama kamwe haitouruhusu utawala wa Kizayuni wa Israel kuwa na utulivu.
Kwa mujibu wa televisheni ya Falastin al Yaum, Musab al-Breim amesema hayo na kuongeza kuwa, kambi ya muqawama inaendesha harakati zake katika janibu zote za kisiasa, kijeshi na za kwenye medani, kuanzia Palestina hadi maeneo mengine na kamwe kambi hiyo haitoruhusu adui Mzayuni aishi kwa utulivu na amani.
Matamshi hayo ya Msemaji wa Jihad al Islami ya Palestina yamekuja baada ya mkuu wa harakati hiyo Ziyad al-Nakhalah na Saleh al-Arouri, Naibu wa Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS, kuonana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon, Sayyid Hassan Nasrullah.
Msemaji wa harakati ya Jihad al Islami amesisitiza kuwa, mshikamano imara ndani ya kambi ya muqawama unaakisiwa na unaonekana wazi katika medani mbalimbali za kupambana na adui Mzayuni.
Wakati huo huo mchambuzi mmoja Mzayuni amekiri kwamba jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limeonesha udhaifu mkubwa katika medani tofauti na hali ni mbaya ndani ya jeshi hilo tofaudi na jinsi viongozi wa Israel, iwe wa kijeshi au wa kisiasa wanavyojaribu kuwaonesha walimwengu.
Shirika la habari la Tasnim limemnukuu Tal Ram, mchambuzi wa masuala ya kijeshi wa gazeti la Kizayuni la Maariv akiandika: Utendaji kazi wa jeshi la Israel una hali mbaya na maandamano dhidi ya serikali ya Netanyahu yamezidi kuliweka jeshi hilo la Israel, katika hali mbaya.
Msemaji wa harakati ya Jihad al Islami ya Palestina amegusia mazungumzo yaliyofanyika baina ya wakuu wa kambi ya muqawama huko Beirut Lebanon na kusisitiza kuwa, kambi ya muqawama kamwe haitouruhusu utawala wa Kizayuni wa Israel kuwa na utulivu.
Kwa mujibu wa televisheni ya Falastin al Yaum, Musab al-Breim amesema hayo na kuongeza kuwa, kambi ya muqawama inaendesha harakati zake katika janibu zote za kisiasa, kijeshi na za kwenye medani, kuanzia Palestina hadi maeneo mengine na kamwe kambi hiyo haitoruhusu adui Mzayuni aishi kwa utulivu na amani.
Matamshi hayo ya Msemaji wa Jihad al Islami ya Palestina yamekuja baada ya mkuu wa harakati hiyo Ziyad al-Nakhalah na Saleh al-Arouri, Naibu wa Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS, kuonana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon, Sayyid Hassan Nasrullah.
Msemaji wa harakati ya Jihad al Islami amesisitiza kuwa, mshikamano imara ndani ya kambi ya muqawama unaakisiwa na unaonekana wazi katika medani mbalimbali za kupambana na adui Mzayuni.
Wakati huo huo mchambuzi mmoja Mzayuni amekiri kwamba jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limeonesha udhaifu mkubwa katika medani tofauti na hali ni mbaya ndani ya jeshi hilo tofaudi na jinsi viongozi wa Israel, iwe wa kijeshi au wa kisiasa wanavyojaribu kuwaonesha walimwengu.
Shirika la habari la Tasnim limemnukuu Tal Ram, mchambuzi wa masuala ya kijeshi wa gazeti la Kizayuni la Maariv akiandika: Utendaji kazi wa jeshi la Israel una hali mbaya na maandamano dhidi ya serikali ya Netanyahu yamezidi kuliweka jeshi hilo la Israel, katika hali mbaya.