Samwelbaruti
Member
- Dec 14, 2012
- 24
- 5
Wanaoujua ufisadi wa IPTL katika ukubwa, mapana na urefu wake wanatambua kuwa kushughulika na Escrow Account pekee (kisha kujiaminisha tumeshughulikia IPTL katika ujumla wake) ni mzaha unaoweza kuvumiliwa kwa minajili ya kuacha muda au wakati uwe hakimu mzuri. Lakini kwa wale wanaoujua undani wa IPTL namna mkataba wa kilaghai na kifisadi ulivyosainiwa tangu miaka ile ya 90 wakati nchi ilipoingia katika shida kubwa ya umeme, huku wahusika wakituingiza katika uvundo mkubwa ambao umezalisha matawi mengi, mojawapo likiwa ni hili la Escrow Account (cha mtoto?), watakuwa na maswali mengi hasa baada ya kuwasilishwa kwa Ripoti ya PAC. Mojawapo ya maswali hayo ni je; Kweli kwa ufisadi mkubwa kama huu, ukiwa ni sehemu ya matokeo ya moja ya mikataba mibovu katika sekta ya nishati, kwamba mabilioni ya fedha yaliyochotwa sehemu nyeti kama benki kuu, yakagawiwa kwa kiwango kile, kiasi ambacho mtu anaweza kujenga hoja na kuhitimisha kuwa kulikuwa na elements za state capture or rather an institutionalized corruption, kwamba ofisi kuu ya nchi na mwenye ofisi ambaye kimamlaka ni Rais Mtendaji alikuwa hajui yote haya? Kwamba aliyekuwa anajua ni Waziri Mkuu pekee! It is a question which remained to be answered! Time will tell, alisema Bob.
rais akiwajibika it minz nchi inaingia kwenye uchaguz.....
bunge ktk jambo hilo naona linasura mbili au tatu kwa upandewangu
1. wabunge wanaogopa wanaweza waschaguliwe tena hivyo kupata aibu na kukosa zile posho na feva kabla ya wakt wao muafaka wa kustaafu/kuachia ngaz
2. nchi itaingia gharama ktk uchaguzi hivyo fedha kutotumika kwenye shughuli za maendeleo
3. chama tawala hakitakubali coz wapowengi bungeni....