Makubwa: Anna Mghwira adai yeye bado ni mwenyekiti wa ACT Wazalendo na hajajiuzulu

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
Mkuu mpya wa mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira, amesema yeye bado ni mwenyekiti wa ACT-Wazalendo na ataendelea kushika wadhfa huo kama kawaida. Mghwira aliyeapishwa Jumanne kuanza kazi, ametoa maelezo hayo katika mahojiano mahsusi na mwandishi Jamal Hashim wa Azam TV.

Amedai mbona Lipumba aliwai kuwa mshauri wa Museni Uganda yeye kuwa RC Kilimanjaro ndo iwe nongwa?

Anauwezo wa kuwa RC na kuwa mwenyekiti wa ACT
 
Kwa hiyo mkutano wa Act wazalendo kesho atahudhuria? Kuna nafasi za utumishi wa umma ukiteuliwa unatakiwa kujiuzulu vyeo vya kichama
 

Kama ataweza kuweka kofia mbili ninampongeza sana tu.
 
Yale yale ya Lipumba CUF. ACT mkizubaa imekula kwenu; hakikisheni taratibu za kumvua uanachama zinafanyika na kukamilika haraka else atakuja kuwasumbua mahali msipotarajia. Kama vipi uanachama ataomba upya akishamaliza hiyo kazi aliyopewa. Mkizubaa, ya mtungi yanawahusu.
 
Ina maana ACT kama chama hawakuliongelea hilo suala la uteuzi wake na kufikia makubaliano?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…