Maktaba Ndani ya Kibatari cha Mchina

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,921
30,266
MAKTABA NDANI YA KIBATARI CHA MCHINA

Inawezekana kabisa kuwa katika wasomaji wangu wakawepo ambao hawajasikia neno, "kibatari," wala hawajakiona kibatari.

Nilipata kuwahadithia wanangu kuku wangu niliyekuwa nalalanae chumba kimoja yeye analalia yuko pembeni kwenye kona.

Mshtuko mkubwa.

Nawatahadharisha kuwa kuku akilalia mpitie kwa mbali ama sivyo atakuparura.

"Baba unalala na kuku chumba kimoja?

"Naam tunalala chumba kimoja."
Najua wapi shida yao ilipo.

Wao kuku wanamuona mezani katoka super market keshachinjwa.

Nyumba wanayojua wao ni hiyo waliyozaliwa yenye korokoro zote za kisasa pamoja na air-condition na mengineyo.

Nyumba yetu ilikuwa juu makuti na chini udongo na sakafu ni ardhi yenyewe ya Allah.

Moyoni wanajiambia baba analeta porojo kututisha.

"Taa yangu kibatari."
"Kibatari?"

Naulizwa.

Hawa hawawezi kuchangia computer moja kila saa naitwa kuamua ugomvi.

"Game over," mtu hataki kumpisha mwenzake wananishauri kila mtu anunuliwe computer yake kumaliza tatizo.

Hawana habari kuwa sisi sahani moja ya ugali tunakula watoto zaidi ya saba na hatugombanii chochote si katika ugali wenyewe wala yale maharage au dagaa.

Nikawaeleza kibatari kilivyo.

Kama ningewawashia kibatari chumbani kwao wote wangekimbia wanaogopa nyumba itawaka moto.

Hii shida ya umeme kazi nyingi zimesimama.
Maktaba huwezi kuifungua gizani.

Waingereza wana msemo: "An idle mind is a workshop for the devil," yaani ubongo usio na kazi ya kufanya ni karakana ya shetani."

Kutwa nzima sijaandika hata maneno 1000 naona shida.

Sasa kuepuka mimi kuwa gereji ya Iblis nimeona nitafute taa ya solar inisaidie kumulika Maktaba na kuiona keyboard.

Huo hapo chini ndiyo muonekano wa Maktaba nilipokiwasha kibatari cha Mchina leo TANESCO walipochomoa waya wao.

Kazi inaendelea.
 
MAKTABA NDANI YA KIBATARI CHA MCHINA

Inawezekana kabisa kuwa katika wasomaji wangu wakawepo ambao hawajasikia neno, "kibatari," wala hawajakiona kibatari.

Nilipata kuwahadithia wanangu kuku wangu niliyekuwa nalalanae chumba kimoja yeye analalia yuko pembeni kwenye kona.

Mshtuko mkubwa.

Nawatahadharisha kuwa kuku akilalia mpitie kwa mbali ama sivyo atakuparura.

"Baba unalala na kuku chumba kimoja?

"Naam tunalala chumba kimoja."
Najua wapi shida yao ilipo.

Wao kuku wanamuona mezani katoka super market keshachinjwa.

Nyumba wanayojua wao ni hiyo waliyozaliwa yenye korokoro zote za kisasa pamoja na air-condition na mengineyo.

Nyumba yetu ilikuwa juu makuti na chini udongo na sakafu ni ardhi yenyewe ya Allah.

Moyoni wanajiambia baba analeta porojo kututisha.

"Taa yangu kibatari."
"Kibatari?"

Naulizwa.

Hawa hawawezi kuchangia computer moja kila saa naitwa kuamua ugomvi.

"Game over," mtu hataki kumpisha mwenzake wananishauri kila mtu anunuliwe computer yake kumaliza tatizo.

Hawana habari kuwa sisi sahani moja ya ugali tunakula watoto zaidi ya saba na hatugombanii chochote si katika ugali wenyewe wala yale maharage au dagaa.

Nikawaeleza kibatari kilivyo.

Kama ningewawashia kibatari chumbani kwao wote wangekimbia wanaogopa nyumba itawaka moto.

Hii shida ya umeme kazi nyingi zimesimama.
Maktaba huwezi kuifungua gizani.

Waingereza wana msemo: "An idle mind is a workshop for the devil," yaani ubongo usio na kazi ya kufanya ni karakana ya shetani."

Kutwa nzima sijaandika hata maneno 1000 naona shida.

Sasa kuepuka mimi kuwa gereji ya Iblis nimeona nitafute taa ya solar inisaidie kumulika Maktaba na kuiona keyboard.

Huo hapo chini ndiyo muonekano wa Maktaba nilipokiwasha kibatari cha Mchina leo TANESCO walipochomoa waya wao.

Kazi inaendelea.
Mohammed Said,

Umeandika hali halisi ambayo watu wa umri kuanzia miaka 40 na kuendelea wengi tulipitia hayo maisha ya kibatari. Wachache wa umri huo walizaliwa mijini hivyo maisha ya kibatari ni hadithi kwao lakini taa ya chemli nina hakika wanaifahamu labda wawe wakulia London.

Umeme umefikia vijiji miaka ya karibuni na sehemu nyingine bado, hivyo maisha ya kibatari na taa ya kandiri bado si hadithi bali ni maisha halisi ambayo watu wanaendelea kuyaishi.,
 
Back
Top Bottom