Matayarisho ya Kipindi cha Nyerere Day 2022

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,897
30,235
KATIKA KUTENGENEZA KIPINDI CHA SIKU YA BABA WA TAIFA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE
Sijapata kufanya kipindi kama hiki.
Jua lilikuwa kali sana asubuhi ya saa tatu.

Gari la Azam TV lina ''full kiyoyozi,'' pembeni yangu amekaa Jaffar Mponda mtayarishaji wa kipindi hiki na hapo tulipokaa miguu yetu tumenyoosha kama vile tuko kwenye Emirates ''business class.''

Ipo nafasi ya kutosha sana ya kunyoosha miguu hata kuweka nne yaani unaonyanyua mguu mmoja unauweka juu ya mwingine.

Mponda alikuwa anapanga kipindi hiki siku nyingi na alikuja na wazo kuwa itapendeza sana ikiwa katika kumuenzi Mwalimu Nyerere tukafanya kipindi kueleza nyumba ambazo Mwalimu aliishi na halikadhalika sehemu ambazo zina kumbukumbu ya matukio muhimu katika historia yake Baba wa Taifa.

Zaidi akashauri kuwa kipindi hiki tukifanyie mabadiliko makubwa badala ya kufanya kipindi Maktaba iliyoko nyumbani kwangu tuhame twende kwenye nyumba na sehemu zinazomuhusu Mwalimu na yalipotokea matukio yenyewe.

Mwalimu kaishi Kariakoo ile ya miaka ya 1950 Karikaoo iliyokuwa na soko lililoezekwa kwa mabati na yote aliyofanya siku zile sasa imepita miaka 70.

Mwalimu kaikuta ofisi ya TANU New Street barabara ya vumbi na jengo lilijengwa kati ya mwaka wa 1929 - 1933.

New Street leo ni Lumumba Avenue na TANU haipo kuna CCM yenye ofisi ya kupendeza.

Huu ni mwendo mrefu sana.
Kutoka mwaka wa 1929 hadi leo ni miaka 93.

Nimempitisha Jaffar Mponda sehemu kadhaa ambazo zina historia za kusisimua lakini kwa bahati mbaya ni historia ya mambo ambayo watu wachache sana wanafahamu.

Tumeingia Mtaa wa Sikukuu tukitokea Mtaa wa Uhuru tunaelekea nyumba iliyokuwa ya Abdul Sykes Mtaa wa Aggrey kiasi cha saa tatu asubuhi.

Hii ndiyo nyumba ya kwanza Mwalimu aliishi mwaka wa 1955 baaada ya kuacha kazi ya Ualimu Pugu.
Mtaa huu umebadilishwa jina mara kadhaa kuanzia Stanley, Aggrey hadi sasa unaitwa Makisi Mbwana lakini kibao hakijabadilishwa bado kinasomeka kibao cha zamani Aggrey ingawa ''spelling'' ya jina imekosewa vibaya sana ''Agray.''

Majina yote haya yana uhusiano mkubwa na historia ya Tanganyika.

Jua ni kali sana, watu na magari yameshonanana mwendo wa binadamu na vyombo vya moto magari, bodaboda na Bajaj zimejaza barabara yote.

Kama haya hayatoshi pembeni mwa barabara wafanyabiashara wameweka bidha zao kuanzia vikabu vyenye ubuyu wa Zanzibar wa kila rangi hadi nguo na vitu vingi.

Dereva wetu Bwana Ismail kaibanisha pembeni gari tushuke haraka na mizigo yetu vifaa vya kazi camera, stendi na korokoro nyingine.

''Bye bye,'' kiyoyozi nalisikia joto na jua kali linanipiga vizuri.

Tuko kwenye kona ya Makisi Mbwana na Sikukuu huoni zaidi ya mgongo wa mwenzako.

Watu wameona gari la Azam linashusha watu na camera wakajua leo hapa kuna jambo.

Muda si muda tumezingirwa.
Nimeipa mgongo biashara ya dada mmoja namtaka radhi.

Jaffar Mponda yuko tayari na mike yake na mtu wa camera ''headphones,'' kichwani, anampa ishara ya vidole kuwa yeye yuko tayari.

Anaanza kuzungumza.

Namuonyesha nyumba ya Abdul Sykes ile ya zamani ambayo haipo badala yake kuna ghorofa.

Sote tunaangalia jengo zuri la gorofa tano.
Naeleza upande wa nyumba ile ya zamani iliyojengwa mwaka wa 1942.

Naeleza na naonesha upande wa nyumba aliyokuwa anaishi Mwalimu Nyerere wakati wa kupigania uhuru.

Mlango wake aliokuwa akiingia na kutokea ulikokuwa Mtaa wa Sikukuu.

Naeleza aivyokuwa anatembea kwa miguu kutoka pale anaelekea Soko la Kariakoo asubuhi anakwenda ofisini kwa Abdul Sykes ofisi ambayo zamani ilishikwa na Brian Hodges Mwingereza.

Nendelea kueleza na wasikilizaji wangu nawaona wako makini sana historia hii imewavutia.

TANU imepamba moto Soko la Kariakoo na kwa Mwalimu kuwa pale sokoni watu sasa ndiyo wanaanza kumfahamu Rais wa TANU chama kinachopigania uhuru wa Mwafrika katika nchi yake.

Wasikilizaji wameongezeka sasa wamenizunguka wananisikiliza kwa makini na wanasikilkiza maswali ninayoulizwa na Jaffar Mponda.

Gumzo limenoga...

Tulipomaliza watu wametuzunguka kama vile wanatuzuia tusiondoke wanataka kujua zaidi historia ya nyumba ile ambayo haipo badala yake kuna jumba ambalo wao kwa miaka sasa wanaliona pale lakini hawakuwa wanafahamu kuwa hapo ndipo Baba wa Taifa alipoanza kampeni yake na TANU dhidi ya ukoloni wa Mwingereza.

Kazi yetu hapo imekamilika.

Hatuna muda tunakimbilia nyumbani kwa Clement Mtamila Mtaa wa Kipata (sasa Mtaa wa Kleist Sykes) ukivuka Mtaa wa Uhuru ushafika ilipokuwa nyumba yake.

Hapa ndipo palipofanyika kikao cha Halmashauri Kuu ya TANU mwenyekiti akiwa Mzee Mtamila kujadili barua ya Mwalimu kutoka kwa mwajiri wake iliyomtaka achague siasa au kazi ya ualimu.

Mponda anawatuliza watu na maswali yao anawaambia wawe na subra kipindi kitarushwa siku ya Nyerere Day.

Kutoka ilikpokuwa nyumba ya Mzee Clement Mtamila tukavuka upande wa pili wa Mtaa wa Sikukuu tukasimama kwenye kona ya Mtaa wa Lindi na Sikukuu kuangalia sehemu ambayo Mwalimu Nyerere siku moja akipita mitaa ya Gerezani alimuona Bi. Mruguru bint Mussa, mama yake Abdul Sykes akasimamamisha masafara wake akatoka ndani ya gari kumwamkia.
Vijana wa bodaboda waliokuwa pale walisisimkwa na kisa hiki.
Wanamjua Nyerere lakini hawamjui Bi. Mruguru wala hawajamsikia Abdul Sykes.

Tulipotoka hapo tukaenda Mtaa wa Kipata alipokuwa akiishi Ally Sykes na mkewe Bi Zainab.

Nyumba ndogo ya kawaida haipo na badala yake kuna gorofa ndefu ya kuishi watu na chini kuna ofisi na maduka.

Hapa nilihadithia kisa cha mashine iliyokuwa ikichapa makaratasi ya kuhamasisha wananchi kujiunga na TAA mashine ambayo Special Branch makachero wa serikali walikuwa wanaitafuta.

Nikaeleza na kikao kilichofanywa hapo mwezi Julai 1954 kati ya Abdul Sykes, Ally Sykes na Julius Nyerere kupokea kutoka kwa Nyerere taarifa ya tasjila ya TANU mara tu baada ya kupeleka maombi ya kusajili TANU.

Waingereza walikataa kuisajili TANU.

Tulipotoka hapo tukaende Arnautoglo Hall mahali ambao mwaka wa 1953 Nyerere aligombea nafasi ya urais wa TAA dhidi ya Abdul Sykes.

Nilimuonyesha Mponda ukumbi wenyewe ulipofanyika mkutano na kueleza ilikuwaje hadi Nyerere kufika pale na kueleza kuwa hafla ya kumuaga Nyerere safari ya pili UNO ilifanyika Ukumbi wa Arnautoglu na safari ya kwanza hafla ilifanyika jengo la Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika Mtaa wa Stanley na New Street.

Tukaondoka hapo tukaenda Mtaa wa Lumumba na Kariakaoo kwenye nyumba ya Bi. Mwamtoro bint Chuma aliyekuwa akivunja ua wake na kuunganisha na ua wa TANU kila Mwalimu alipokuwa anataka kuwa na mkutano wa ndani na wanachama wa TANU.

Nyumba hii bado ipo hadi leo ngawa watu wachache sana ndiyo wenye kuijua historia yake na Mwalimu Nyerere.

Tukahitimisha kwa kufika Nyumba ya Kumbukizi ya Mwalimu Nyerere Mtaa wa Ifunda Magomeni.

PICHA:
Mwandishi akizungumza.
Jaffar Mponda.
Watu wanasikiliza.r
Nyumba ya Abdul Sykes ya zamani aliyoishi na Julius Nyerere na nyumba ya sasa.
Bi. Mruguru bint Mussa.
Kushoto wakwanza aliyesimama ni Said Chamwenyewe na wa mwisho kulia waliokaa ni Mzee Clement Mtamila.
Ally Sykes na Julius Nyerere 1958.
Ukumbi wa Arnautoglu kama ulivyokuwa 1950.
Abdul Sykes na Nyerere Ukumbi wa Arnautoglu, 1956.
Bi. Mwamtoro bint Chuma akipiga kura 1970.

1665522810613.png

Bi. Mwamtoro bint Chuma mama yake Haidar Mwinyimvua mama alikuwa mstari wa mbele TANU na halikadhalika mtoto wake.
 
Hongera kwa kuandika bila kuzungumzia dini leo. Nyerere bado anaishi katika integrity and responsibility aliyoionesha. Tutaendelea kumkumbuka.
 
Mzee Mohamed Said naona kituo cha televisheni kimeamua kutumia usemi wa wahenga kuwa 'Mchawi mpe mtoto'.

Huyu mwanasiasa kutoka kijijini miaka ya 1940 na 1950 aliyekaribishwa na wazee wa Darisalama.

Mwaka huu 2022 tunasubiri jinsi utakavyo mwasilisha katika kipindi hiki maalum cha Julius Kambarage Nyerere.
 
Mzee Mohamed Said naona kituo cha televisheni kimeamua kutumia usemi wa wahenga kuwa 'Mchawi mpe mtoto'.

Huyu mwanasiasa kutoka kijijini miaka ya 1940 na 1950 aliyekaribishwa na wazee wa Darisalama.

Mwaka huu 2022 tunasubiri jinsi utakavyo mwasilisha katika kipindi hiki maalum cha Julius Kambarage Nyerere.
Maelezo ya Mzee Saidi kuhusu Mwalimu ni lazima uwe kwenye hali ya "za kuambiwa changanya na zako".
 
Hongera kwa kuandika bila kuzungumzia dini leo. Nyerere bado anaishi katika integrity and responsibility aliyoionesha. Tutaendelea kumkumbuka.
Champ...
Hupendi kusoma historia ya Waislam katika historia ya uhuru wa Tanganyika?
 
Mzee Mohamed Said naona kituo cha televisheni kimeamua kutumia usemi wa wahenga kuwa 'Mchawi mpe mtoto'.

Huyu mwanasiasa kutoka kijijini miaka ya 1940 na 1950 aliyekaribishwa na wazee wa Darisalama.

Mwaka huu 2022 tunasubiri jinsi utakavyo mwasilisha katika kipindi hiki maalum cha Julius Kambarage Nyerere.
Bagamoyo,
Mtu yeyote kama angefunguliwa Nyaraka za Sykes akazisoma angeyajua haya yote niliyoyajua mimi na angewatangulia wengi kwa kuifahamu historia ya Mwalimu Nyerere.
 
Champ...
Hupendi kusoma historia ya Waislam katika historia ya uhuru wa Tanganyika?
Mkuu huwa unakuwa biased sana, hapo ndio changamoto ilipo. Pia, tunatakiwa kuhesabu na kukumbuka michango ya watu kama watanganyika na baadae watanzania badala ya kufanya hivyo kwa kigezo cha dini.

Imani za watu tuziache kwenye nyumba za ibada na maisha binafsi. Tuzungumze huku nje kama watanzania.
 
23 May 2022
Maputo, Mozambique

Jakaya Kikwete akizungumzia maisha ya baba wa Taifa, mwl. Julius Nyerere 1922 - 2022, alivyojitoa mhanga kwa kila hali kuongoza kudai uhuru .....

Julius Nyerere 100 anos- 1922 -2022 Pan-Africanismo Presente e Futuro



Para assinalar a passagem do centésimo aniversário do nascimento do primeiro presidente tanzaniano e Pan-africanista, Julius Kambarage Nyerere, realiza-se amanhã, 23 de Maio de 2022, uma Conferência intitulada: Julius Nyerere 100 Anos - 1922-2022, Pan-Africanismo; Presente e Futuro.

A conferência terá como orador principal Jakaya Kikwete, antigo presidente da República Unida da Tanzânia, que vai falar sobre a figura emblemática do ícone libertário de África. Nyerere foi um dos fundadores da Organização da Unidade Africana (OUA), actual União Africana, em 1963 e da SADCC, liderou o seu Comité de Descolonização da OUA, deu sempre um grande apoio à FRELIMO, na sua luta pela independência de Moçambique.
Source : samora machel foundation
 
Mkuu huwa unakuwa biased sana, hapo ndio changamoto ilipo. Pia, tunatakiwa kuhesabu na kukumbuka michango ya watu kama watanganyika na baadae watanzania badala ya kufanya hivyo kwa kigezo cha dini.

Imani za watu tuziache kwenye nyumba za ibada na maisha binafsi. Tuzungumze huku nje kama watanzania.
Champ.
Nachukulia unaposema ''bias,'' unakusudia kuwa napendelea.
Nitajaribu kujieleza.

Nimeandika historia hii kwenye kitabu mwaka wa 1998 bada ya kuona kuwa historia ya TANU imepotoshwa.

Nilipogundua hili ndiyo nikanyanyua kalamu kuandika historia ya kweli ya TANU.

Imetokea kuwa historia hii ni historia ya jamii ambayo mimi nimetoka na kwa hakika ni historia ya wazee wangu walioishi Dar es Salaam katika miaka ya 1920 walipounda African Association na kufanya haya yote unayosoma hapa.

Ikiwa mimi ningeiandika historia hiyo ya hawa Watanganyika na nikaacha Uislam wao katika historia hiyo ningekuwa nimefuta sehemu muhimu ya historia hii.

Ningefanya hivi utafiti wangu ungekuwa una makosa.

Ungekuwa na makosa kwa kuwa hawa wazee wangu baada ya kuunda African Association (Umoja wa Waafrika) 1929 mwaka wa 1933 wakaunda Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) pembeni ya African Association.

Vyama vyote hivi viwili vilifanya kazi kwa karibu sana kuupambana na ukoloni.
Umepata kuona picha yeyote ya Maaskofu na Nyerere wakati wa kupigania uhuru?

Hakuna.
Wewe hujajiuliza kwa nini?

Kwangu mimi kueleza kwa nini hawakuunga mono TANU imesaidia kuieleza historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika kwa ukamilifu wake.

Walioandika historia ya TANU hili waliliona na likawajaza hofu na uamuzi wao ikawa kuandika historia ya uhuru na kuufuta mchango wa Waislam.
 
Champ.
Nachukulia unaposema ''bias,'' unakusudia kuwa napendelea.
Nitajaribu kujieleza.

Nimeandika historia hii kwenye kitabu mwaka wa 1998 bada ya kuona kuwa historia ya TANU imepotoshwa.

Nilipogundua hili ndiyo nikanyanyua kalamu kuandika historia ya kweli ya TANU.

Imetokea kuwa historia hii ni historia ya jamii ambayo mimi nimetoka na kwa hakika ni historia ya wazee wangu walioishi Dar es Salaam katika miaka ya 1920 walipounda African Association na kufanya haya yote unayosoma hapa.

Ikiwa mimi ningeiandika historia hiyo ya hawa Watanganyika na nikaacha Uislam wao katika historia hiyo ningekuwa nimefuta sehemu muhimu ya historia hii.

Ningefanya hivi utafiti wangu ungekuwa una makosa.

Ungekuwa na makosa kwa kuwa hawa wazee wangu baada ya kuunda African Association (Umoja wa Waafrika) 1929 mwaka wa 1933 wakaunda Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) pembeni ya African Association.

Vyama vyote hivi viwili vilifanya kazi kwa karibu sana kuupambana na ukoloni.
Umepata kuona picha yeyote ya Maaskofu na Nyerere wakati wa kupigania uhuru?

Hakuna.
Wewe hujajiuliza kwa nini?

Kwangu mimi kueleza kwa nini hawakuunga mono TANU imesaidia kuieleza historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika kwa ukamilifu wake.

Walioandika historia ya TANU hili waliliona na likawajaza hofu na uamuzi wao ikawa kuandika historia ya uhuru na kuufuta mchango wa Waislam.
Mimi ninachojua uhuru walipigania watanganyika na sitahusisha dini walizokuwepo.

Kama wakristo wangekuwa wabaguzi basi waislam wasingepata elimu nchi hii maana asilimia kubwa walikuwa wanamiliki shule wao.

Miaka ile watanganyika wengi walikuwa na dini za asili hivyo hakuna point ya kumtambua mtu kwa dini yake.

Besides, Nyerere aliyempa dr salimu ubalozi akiwa teenager na tena akawa anataka awe rais mwaka 1995 (mkapa ameandika hili) sioni kama alikuwa mdini.

Waislam hamtaki kuface the truth na kikwete aliwachana live kipindi kile ni rais. Jengeni shule na vyuo vitakavyowapa elimu bora.

Dubai na qatar wameachana na misimamo mikali ya dini na wameendelea baada ya kuwekeza kwenye western education.
 
Mimi ninachojua uhuru walipigania watanganyika na sitahusisha dini walizokuwepo.

Kama wakristo wangekuwa wabaguzi basi waislam wasingepata elimu nchi hii maana asilimia kubwa walikuwa wanamiliki shule wao.

Miaka ile watanganyika wengi walikuwa na dini za asili hivyo hakuna point ya kumtambua mtu kwa dini yake.

Besides, Nyerere aliyempa dr salimu ubalozi akiwa teenager na tena akawa anataka awe rais mwaka 1995 (mkapa ameandika hili) sioni kama alikuwa mdini.

Waislam hamtaki kuface the truth na kikwete aliwachana live kipindi kile ni rais. Jengeni shule na vyuo vitakavyowapa elimu bora.

Dubai na qatar wameachana na misimamo mikali ya dini na wameendelea baada ya kuwekeza kwenye western education.
Champ...
Sina tatizo na unavyoiona historia ya uhuru wa Tanganyika.

Mimi nimeandika historia hii ya wazee wangu ili dunia ifahamu mchango wao.

Ikiwa wewe hukupendezewa hiyo ni bahati mbaya kwako.

Hayo mengine uliyoleta ya elimu ya Waislam wala sitakujibu.

Fungua uzi nitakupa historia vipi Nyerere aliipiga marufuku EAMWS wakati inajenga Chuo Kikuu mwaka wa 1968 akamfukuza nchini Mufti Sheikh Hassan bin Ameir na akawaundia Waislam BAKWATA.

Usijadili usiyoyajua.
 
Back
Top Bottom