Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 22,454
- 32,980
MAKTABA IMEPOKEA: MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE PHOTOGRAPHIC JOURNEY
Rafiki yangu ndugu Ali Sultan mmoja wa watayarishaji wa kitabu hiki kikubwa cha Mwalimu jana alikuwa Ikulu Dodoma kwa uzinduzi wa kitabu hiki.
Leo kafika Maktaba kunikabidhi kitabu.
Kiswahili hakina msamiati wa kueleza shukurani zangu kwake.
"Nayajua mapenzi yako kwa Mwalimu," kaniambia akinikabidhi hazina hii.
Kitabu hiki kina historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika katika picha na maelezo.
Yapo mengine mengi katika maisha ya Mwalimu.
Maneno hayatoshi kueleza yaliyomo ila uwe na kitabu hiki wewe mwenyewe mkononi unafungua ukurasa baada ya ukurasa.
Hakika kazi kubwa imepitika.
Tuna deni kubwa kwa waandishi wa kitabu hiki ambalo si rahisi kulilipa.
Rafiki yangu ndugu Ali Sultan mmoja wa watayarishaji wa kitabu hiki kikubwa cha Mwalimu jana alikuwa Ikulu Dodoma kwa uzinduzi wa kitabu hiki.
Leo kafika Maktaba kunikabidhi kitabu.
Kiswahili hakina msamiati wa kueleza shukurani zangu kwake.
"Nayajua mapenzi yako kwa Mwalimu," kaniambia akinikabidhi hazina hii.
Kitabu hiki kina historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika katika picha na maelezo.
Yapo mengine mengi katika maisha ya Mwalimu.
Maneno hayatoshi kueleza yaliyomo ila uwe na kitabu hiki wewe mwenyewe mkononi unafungua ukurasa baada ya ukurasa.
Hakika kazi kubwa imepitika.
Tuna deni kubwa kwa waandishi wa kitabu hiki ambalo si rahisi kulilipa.