Makongoro Mahanga:Serikali Kuu itavunja tena Katiba kama itachukua bilion 5.8 za UDA

barafu

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
6,739
32,874
image.jpeg

Anaandika Mhe Dr. Milton Mahanga

Nimesoma kwenye gazeti moja leo kwamba Serikali Kuu inaweza kuzichukua na kuzitumia zile shs. bilioni 5.8 za UDA zilizokataliwa na mwenye hisa (Jiji la Dar es Salaam). Wala sibishi kwamba hilo haliwezekani kwa kuwa utawala wa kisheria una walakini katika enzi hizi hapa nchini.

Lakini kama utawala wa kisheria utafuatwa, kinachotakiwa kufanywa kabla ya Serikali Kuu kuchukua fedha hizo ni kuanzisha kwanza mchakato wa kuhamisha hisa zilizokuwa Jiji kwenye Shirika la UDA na kuzihamishia Serikali Kuu. Baada ya hapo Serikali Kuu sasa ndiyo iuze hisa hizo za UDA kwa Simon Group

Hii ni kwa sababu kwa mujibu wa Katiba ya Nchi Ibara ya 145 na 146, ikisomwa pamoja na Sheria zilizoanzisha Serikali za Mitaa, Sheria Na. 7 na 8 za mwaka 1982, Serikali za Mitaa zina mamlaka kamili ya kuamua kuhusu mali na rasilimali zake. Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imeamua kusitisha uuzaji wa hisa zake asilimia 51 kwenye UDA kwenda kwa Simon Group.

NB:Makongoro Mahanga amekuwa muibuaji wa mijadala ya Kikatiba inayoonekana kukiukwa na Serikali ya awamu ya tano.Mjadala wa uteuzi wa Wabunge wanaotokana na nafasi za Rais uliibuliwa na Makongoro Mahanga.

Mjadala huo ulisababisha Mh.Rais kufanya mabadiliko ya "ghafla" ya uteuzi wake kwa kumtoa Dr Possi na kumuweka Anna Kilango Malecela.

Na pia ibaki ktk kumbukumbu kuwa wakati wa uuzwaji huu wa "kisanii" wa UDA,Dr Milton Makongoro Mahanga alikuwa Naibu Waziri na Mbunge wa Jimbo la Segerea ambapo kwa mujibu wa taratibu anakuwa sehemu ya baraza la Madiwani Dsm.

Lakini Marehemu Didas Masaburi ambaye nyaraka nyingi za uuzwaji wa UDA zimemtaja,ni ndugu wa Dr Mahanga.Ukiwa ndani ya mfumo kijani nyeusi huwa na mchangayiko wa blue na kijani,lakini nje ya mfumo....NYEUSI NI NYEUSI KWA MAANA YA NAMNA INAVYOONEKANA
 
Atusaidie tu kwa sababu Mwanasheria mkuu wa serekali na Waziri wetu wa sheria wote ni NANGA!!! Baba endelea na msaada wako kwani NANGA zetu zinahangaika na mahakama za mafisadi ambazo zimekosa wafungwa na NANGA nyingine inahangaika na vifungu vya chama badala ya vifungu vya katiba ya Nchi
 
Ama kweli sasa naanza kuiona mantiki ya Dr Milton Mahanga kuhoji kwa nn kwa kipindi chote kile hakupandishwa kuwa waziri kamili badala yake akasugua na unaibu waziri mwanzo Mwisho.

Kuna uwezekano Kabisa kuna siku alitamani kumwambia waziri wake ampishe kiti kutokana na madudu aliyokuwa anaona anafanya ila tu maadili ya Kazi yakamkaba koo..

Go go go Dr Mahanga endelea kufukunyua madudu ya awamu ya tano..
 
Atusaidie tu kwa sababu Mwanasheria mkuu wa serekali na Waziri wetu wa sheria wote ni NANGA!!! Baba endelea na msaada wako kwani NANGA zetu zinahangaika na mahakama za mafisadi ambazo zimekosa wafungwa na NANGA nyingine inahangaika na vifungu vya chama badala ya vifungu vya katiba ya Nchi


Mkuu wangu we mzaliwa wa Wapi maana hili neno NANGA ni nadra sana kulisikia maeno ya pwani..Kanda ya Ziwa...Kanda ya kati...Kanda ya nyanda za juu magharibi/mashariki....kusini baadhi ya sehemu za kaskazini....



Hahahahaaa......NANGA
 
Sijui AG wa serikali anafanya kazi gani.
Its about time Rais aanze ku go through hotuba na maamuzi yake kwa AG, kabla hajayatamka ili aelezwe kama maamuzi yake yanavunja sheria zozote ama la.
 
Hata aliyekuwa anasema serikali itazichukua hizo bil 5.8 alikuwa anaelewa basi hayo maswala ya hiyo sheria?

Sasa mtu alisikiliza maelezo ya simbachawene tayari akakurupuka!Bila hata kujiridhisha......
Tutaona na kusikia mengi hii miaka mitatu iliyobaki
 
Hata aliyekuwa anasema serikali itazichukua hizo bil 5.8 alikuwa anaelewa basi hayo maswala ya hiyo sheria?

Sasa mtu alisikiliza maelezo ya simbachawene tayari akakurupuka!Bila hata kujiridhisha......
Tutaona na kusikia mengi hii miaka mitatu iliyobaki


Tuombe tu Mungu isije ikawa nane mkuu wangu...maana....khaaaa
 
Mkuu wangu we mzaliwa wa Wapi maana hili neno NANGA ni nadra sana kulisikia maeno ya pwani..Kanda ya Ziwa...Kanda ya kati...Kanda ya nyanda za juu magharibi/mashariki....kusini baadhi ya sehemu za kaskazini....



Hahahahaaa......NANGA
Kwa sisi tuliopitia Jeshini tunaelewa maana ya neno Nanga ni kuwa hasiyejua kabisa au mbabaishaji katika jambo fulani kwenye jeshi ni graride au parade kama utapenda.
 
Kwa sisi tuliopitia Jeshini tunaelewa maana ya neno Nanga ni kuwa hasiyejua kabisa au mbabaishaji katika jambo fulani kwenye jeshi ni graride au parade kama utapenda.


Sawa mkuu nani huko ninakotoka lina maana hyo hyo..mkuu
 
Makongoro Majanga muiba kura ndo leo hii Amekuwa mkosoaji wa serikali? Maajabu kabisaa
 
Tunatarajia Kashfa ya UDA iltaleta aibu kubwa sana katika Tanzania , inaweza kuwa aibu itakayosaidia mambo mengi sana .
 
Back
Top Bottom