OMUSILANGA
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 384
- 227
Ndiyo wakuu! Habari zilizo nifikia muda huu ni kuwa mawaziri Mahanga na Kabaka wamelala mitini i.e. hawajatokea kwenye kikao cha kamati ya bunge ya huduma za jamii kilichokuwa kimepangwa kuanza leo jijini Dares salaam. Lengo la kikao hiki ni mwendelezo wa mjadala mpana kuhusu mafao ya wafanyakazi ndani ya mifuko ya hifadhi za kijamii.
Ikumbwe kabisa kuwa ni bunge hili la serikali legelege na dhaifu lili ipitisha sheria hii mwezi April,mwaka huu ambapo inatakiwa mfanyakazi atimize umri wa miaka 60 ndo apate mafao yake. Naomba nisi eleze sana kwani suala hili si jipya masikioni na machoni mwa watanzania.
Kwa mjibu wa taarifa ni kuwa wadau walio hudhuria ni wengi sana kutoka mifuko mbalimbali ya jamii pamoja na wawakilishi wa wafanyakazi wa migodini kutoka mikoani ambao ndio wahanga wakubwa wa sheria hii kandamizi. Katika hali ya kushangaza ,Mbunge Komba ndiye anaesumbua wajumbe wa kikao hicho kama mpiga debe upande wa serikali.
Kama hali ita endelea hivi, baadae wadau watafanya Press conference kutoa dukuduku zao. Naomba kuwasilisha. Source. Mmoja wa wadau ndani ya kikao.
Ikumbwe kabisa kuwa ni bunge hili la serikali legelege na dhaifu lili ipitisha sheria hii mwezi April,mwaka huu ambapo inatakiwa mfanyakazi atimize umri wa miaka 60 ndo apate mafao yake. Naomba nisi eleze sana kwani suala hili si jipya masikioni na machoni mwa watanzania.
Kwa mjibu wa taarifa ni kuwa wadau walio hudhuria ni wengi sana kutoka mifuko mbalimbali ya jamii pamoja na wawakilishi wa wafanyakazi wa migodini kutoka mikoani ambao ndio wahanga wakubwa wa sheria hii kandamizi. Katika hali ya kushangaza ,Mbunge Komba ndiye anaesumbua wajumbe wa kikao hicho kama mpiga debe upande wa serikali.
Kama hali ita endelea hivi, baadae wadau watafanya Press conference kutoa dukuduku zao. Naomba kuwasilisha. Source. Mmoja wa wadau ndani ya kikao.