Makonda: Walimu kusafiri bure

Kuna watu mnaishi kwakukariri kupondea kila kitu
 
D
Kama namuona vile Mwalimu Nanaa anavyozuiwa kupanda daladala hadi lijae kwanza!!!
Du!
Wanafunzi wawili na walimu wawili tu nndio mwingie ndani alafu msimame mwapishe wenye fedha zao wakae"

Kama namwona kinda akichonga vile
 
Sasa naona hii nchi inakoelekea siko. Serikali isiwatupie mizigo watu wengine ikubali tu kubirwsha maslahi ya waalim, inakuwaje maombi yao hayasikilizwi na badala yake wanaletewa ambayo hawajuwahi hata kutamani!!
Mwanafunzi tu anayelipa nusu nauli anasafiri kwa mbindw na purukushani itajuwa mwalimu anayesafiri bure?
Serikali ijikite katika kutatua matatizo ya kimsingi iachane na hizo cheap drama ambazo zitaishia kuleta sintofahamu.
 
 
Hakuna DC Anayeijua Kazi Yake Na Kubobea Kama Paul Makonda. Hongera Kwa Kusaidia Walimu WETU.
 
...mtafanyaje ili kondakta aridhike kumsafirisha mwalimu bure? na kwa nini manesi nao wasisafiri bure?, kwani wao hawana umuhimu kwenye jamii? na kwa nini mtu mwenye mshahara asafiri bure?,na kwa nini isiwe wanafunzi ndio wasafiri bure?
Mbona mishahara inatofautiana pakubwa tu!!!?kama umuhimu wao unafanana basi wawalipe mishahara sawa,sio mwalimu mwenye degree anaanza na laki saba,mwingine mwenye elimu sawa na mwalimu anaanza na laki tisa,hapo usawa uko wapi!!!?
 
Mheshimiwa Makonda, baba yangu koplo Chacha wa kambi ya Lugalo naye anastaafu mwezi huu, tutakualika uwepo kwenye sherehe ya kumuaga ili uje utoe kauli ma RSM na maSameja nao wawe wanasafiri bure kuwahi master paredi za asubuhi.
 
Mimi naona ni Good idea, Kama mwanajeahi au askari anasafiri bure.. Kwa nini mwalimu asidafiri bure na yeye? Wawe na vitambulisho tu... Mwalimu ni mtu muhimu sana ...
na daktari nae ni muhimu sana nae asafiri bure,dereva anaweza kupata dharura ya ugonjwa daktari akamhudumia akapata nafuu mkaendelea na safari.

Ila Makonda ni mbunifu na ana nia njema.
 
MPANGO HUU NI WAKUUFUTA KABISA / TAASISI ZIWE NA VYOMBO VYAO VYA USAFIRI! FULL STOP!!/
---->>> WANYONGE WASIO NA KAZI WALA CHOCHOTE WASAFIRI BURE.
 

Itakuwa kama hivi

 
Kusafiri bureee si sahihi sana.labda kuwaboreshea mishahara
 
Mimi naona ni Good idea, Kama mwanajeahi au askari anasafiri bure.. Kwa nini mwalimu asidafiri bure na yeye? Wawe na vitambulisho tu... Mwalimu ni mtu muhimu sana ...
vp kuhusu waaguzi na madaktari?
 
Acha hizo baadae na madaktari nk watasafir bure? Hii haiwezekani...... atafute njia mbadala sio hii...
 
vipi kuhusu walimu wa wilaya ya ilala, temeke na bara nao watakuwa katika mpango huo wa makonda au ni kinondoni tuu ndo wahusika?
 
Hakuna DC Anayeijua Kazi Yake Na Kubobea Kama Paul Makonda. Hongera Kwa Kusaidia Walimu WETU.
Amewasaidia nini walimu? Kwanza ni nani aliyemwambia kwamba tatizo kubwa la waalimu ni hizo nauli za daladala? Watu wanafanya kazi muhimu serikali inatakiwa iwape maslahi mazuri kulingana na umuhimu wa kazi wanayofanya. kwanza hakuna mttu anayetaka vitu vya burebure labda wewe kwani bure ni kama udhalilishaji tu. Yeye amekurupuka tu, hana uwezo na mamlaka ya kutoa tamko kama hilo kisha litekelezwe.Amkubushe kwaza Magu ahadi za laptop kwa walimu lini itatekelezwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…