Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,498
Rais Samia Suluhu ameagiza kujengwa kwa shule mpya 56 za kukuza vipaji vya Watoto ili waandalie na wakidhi vigezo na masharti yanayotakiwa kwenye kununuliwa au kusajiliwa na Timu kubwa ndani na nje ya Tanzania.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema hayo leo Februari 9, 2026 wakati akiongea na Waandishi wa Habari Jijini Dar es salaam.
“Mkakati wa Wizara chini ya maelekezo ya Samia, kwanza tunaanza ujenzi wa shule za mfano 56 ambazo kwa awamu ya kwanza tutajenga shule 7 ambazo zitakuwa maalum kwa ajili ya kukuza na kutengeeneza fursa ya Watoto wenye vipaji kuandaliwa katika umri wa mdogo ili wakidhiti vigezo na masharti yanayotakiwa kwenye kununuliwa au kusajiliwa na Timu kubwa”
“Tunao mpango pia kama Wizara tuanze na Halmashauri 20 ambazo zitaweza kujenga viwanja na kujenga shule au centre za kukuza vipaji vya Watoto, mfano mathalani tupo Temeke alipotoka Samatta ila kwanini Temeke isiwe na shule ya awali ya kukuza vipaji vya Watoto ili club kubwa zije kununua Wachezaji”
Aidha, ameongeza kuwa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Kamati ya Utendaji ya CAF utafanyika hapa Tanzania tarehe 13 Februari 2026 katika Hotel ya Hyatt Regency Jijini Dar es Salaam, ambapo utaongozwa na Rais wa CAF, Dkt. Patrice Motsepe.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema hayo leo Februari 9, 2026 wakati akiongea na Waandishi wa Habari Jijini Dar es salaam.
“Mkakati wa Wizara chini ya maelekezo ya Samia, kwanza tunaanza ujenzi wa shule za mfano 56 ambazo kwa awamu ya kwanza tutajenga shule 7 ambazo zitakuwa maalum kwa ajili ya kukuza na kutengeeneza fursa ya Watoto wenye vipaji kuandaliwa katika umri wa mdogo ili wakidhiti vigezo na masharti yanayotakiwa kwenye kununuliwa au kusajiliwa na Timu kubwa”
“Tunao mpango pia kama Wizara tuanze na Halmashauri 20 ambazo zitaweza kujenga viwanja na kujenga shule au centre za kukuza vipaji vya Watoto, mfano mathalani tupo Temeke alipotoka Samatta ila kwanini Temeke isiwe na shule ya awali ya kukuza vipaji vya Watoto ili club kubwa zije kununua Wachezaji”
Aidha, ameongeza kuwa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Kamati ya Utendaji ya CAF utafanyika hapa Tanzania tarehe 13 Februari 2026 katika Hotel ya Hyatt Regency Jijini Dar es Salaam, ambapo utaongozwa na Rais wa CAF, Dkt. Patrice Motsepe.