Tofautisha kumkumbuka mtu na kumtaja mtu mwingine badala ya mlengwa. Shuleni ulijifunza ujinga tu?Kikwete atakumbukwa sana, ni vigumu kumsahau Kikwete haraka haraka.
Hilo si kwa Makonda tu, wengi wanamkumbuka sana tu, mpaka tumewasikia upinzani wakimkumbuka wazi wazi mara kadhaa na kwa makusudi kabisa si kwa kukosea kama Makonda.
Ukweli ubaki kuwa ukweli.
Kumbe katoka huko? Ndio maana kahororojaJina Kikwete likitajwa tu,wewe hutoka mbio hata kama uko msalani!
Na anaporipoti huko inakuwaje?Namsikiliza Makonda hapa Clouds alipokwenda kujikosha kuhusu shisha na rushwa ya Polisi akikosea tena badala ya Rais Magufuli na kuanza kutaja Rais Kikwete.
Hii sii Mara ya kwanza, hilo kosa analifanya sana na Magufuli ana zaidi ya mwaka ndani ya cheo hicho.
Wataalamu wa saikolojia wanaamini kuwa yule aliyejaa kichwani mwako ndiye mwepesi kumtamka mdomoni.
Jee Makonda akili yake bado imejaa kwa Rais Kikwete kuliko Magufuli au hilo linatokea kwa vile anaripoti mambo kwa Kikwete kinyemela?
JPM Ajichunge kwani wapo wateule wake ambao akili zao hazipo kwake Bali kwa mtangulizi wake.