Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,892
Mpelekeeni taatifa Mkuu wa mkoa wa dar es salaam mwambieni kwa niaba ya watumishi wote duniani nampinga kwa maandiko zaidi ya saba yanayokanusha uongo aliouongea hadharani:-
1.kwanza hapo mwanzo MUNGU aliziumba mbingu na dunia.
2.Baba anaitwa Muumba wa mbingu na nchi (dunia)
3.Isaya 45:18
Maana BWANA, aliyeziumba mbingu, asema hivi; Yeye ni Mungu; ndiye aliyeiumba dunia na kuifanya; ndiye aliyeifanya imara; hakuiumba ukiwa, aliiumba ili ikaliwe na watu; Mimi ni BWANA, wala hapana mwingine.
4.Isaya 66:1
BWANA asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu......
5.Mathayo 28:18
Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.
6.Paulo anasema katika Waefeso 3:14-15
Kwa hiyo nampigia Baba magoti,ambaye kwa jina lake ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa,
7.makonda asichanganye maandiko ,MUNGU anasema anatawala mbinguni na duniani ,maana yake utawala wake upo hapa tayari,dola ipo hapa,usalama wa taifa la duniani tuko hapa tukishirikiana na usalama wa mbinguni......mwambieni aendelee
tu na siasa ,mambo ya MUNGU atuachie tunaotetea maslahi ya MUNGU wa mbingu na dunia!
Nukuu toka kwa Kuhani Philemon Mwansepe
(Zab 24:1)Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana, Dunia na wote wakaao ndani yake.
The earth is the LORD' s, and the fulness thereof; the world, and they that dwell therein.
MITHALI 16:18 Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.