pilipili kichaa
JF-Expert Member
- Sep 3, 2013
- 17,660
- 13,719
Kwa jina gani?Amesema kuhusu kutaka kugombea ubunge hapo jimbo la Ubungo.
Kwa jina gani?Amesema kuhusu kutaka kugombea ubunge hapo jimbo la Ubungo.
Watu wakishamchukia mtu hata afanye jema gani bado watamponda tu.It's not always about popularity, let's us learn to appreciate what other people do
Sawa...Watu wakishamchukia mtu hata afanye jema gani bado watamponda tu.
This is Tanzania, watu wana chuki mpaka kwenye mikono
Kupambana ili wamiliki magari?Nadhani anawapa hamasa vijana kupambana
Umetumia kiungo gani kufikiri? Unadhani gari ukiifanyia checkup tu inapona tatizo?Makonda is a very creative person. Anaona mbali sana. Ubunifu huu sio tu utawapunguzia gharama wamiliki wa vyombo hivyo bali pia kupunguza ajali. Ajali zinazotokea, zaidi ya 85% hutokea kutokana na ubovu wa vyombo (one can conduct a research on this). Tumpe ushirikiano ili kupunguza kama sio kumaliza kabisa tatizo la ajali.
Ujinga ujinga tu, likionekana tatizo unaingia mfukoni kuliko kawaida.Hivi anaposema Bure
Kama mtu anataka abadilishiwe engen oil, hydraulic oil etc atapewa Bure pia
Mimi naona kama Kuna mtu anatafutiwa kik tu hapo kwenye garage yake
Ova
Kwani kikawaida kufanya checkup ya gari kunaghalimu kiasi gani?Leo Kwa mara ya Kwanza ninatoa pongezi Kwa MAKONDA itabidi nipele gari Yangu nikachek
Mara nyingi ukifanya check up lazima ujipange Kwanza na pesa ya kununua spare pia inategemea na mafundi wenyewe kuna wengine watakuambia vitu vya kubadilisha karibia engine yote na wengine watakuambia vitu vichache Tu na ukibadilisha unafanya Safari mwanzo mwisho bila shida yeyoteKwani kikawaida kufanya checkup ya gari kunaghalimu kiasi gani?
Kwa hiyo hko utafanyiwa Bure hadi kuwekewa spea bureMara nyingi ukifanya check up lazima ujipange Kwanza na pesa ya kununua spare pia inategemea na mafundi wenyewe kuna wengine watakuambia vitu vya kubadilisha karibia engine yote na wengine watakuambia vitu vichache Tu na ukibadilisha unafanya Safari mwanzo mwisho bila shida yeyote
Spare parts juu yetuKwa hiyo hko utafanyiwa Bure hadi kuwekewa spea bure
Ova
Spare parts juu yetu
Daudi BashiteKwa jina gani?
OkayAmesema kuhusu kutaka kugombea ubunge hapo jimbo la Ubungo.
Kigamboni bhanaAmesema kuhusu kutaka kugombea ubunge hapo jimbo la Ubungo.
Dar es Salaam. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ametangaza siku tano, kuanzia Desemba 10 hadi 15, 2019 kwa wenye magari kufanya ukaguzi ili wasafiri salama kwenda mikoani kwa ajili ya mapumziko ya sikukuu za mwisho wa mwaka.
Makonda ametangaza ukaguzi huo leo Alhamisi Desemba 5, 2019 baada ya kukutana na wamiliki na mafundi gereji ambao walikubali kufanya kazi hiyo bure ikiwa ni ofa ya mwisho wa mwaka.
Amesema ajali nyingi za barabarani zinatokana na wamiliki wa magari kutojenga tabia ya kufanya ukaguzi wa mara kwa mara ili kubaini kasoro.
"Kwa hiyo tutatangaza gereji zilizo tayari kwa kazi hii pelekeni magari yenu ili safari iwe salama," amesema Makonda.
Awali, baadhi ya wamiliki na mafundi wa gereji walisema wapo tayari kufanya kazi hiyo kwa sababu watu wengi watajua changamoto za magari yao kabla ya kuanza safari.
"Tutawashauri kulingana na changamoto tutakazokutana nazo," amesema Elgius Mndale, fundi gereji kutoka wilayani Temeke.
Mkurugenzi wa Evolution Investment & General Supplies Ltd, Anthony Mganja amesema pamoja na kufanya ukaguzi huo, wapo tayari kutengeneza magari ya Serikali ya Mkoa wa Dar es Salaam kwa kipindi cha miezi sita.
"Tunaunga mkono kazi za Rais John Magufuli za kuleta maendeleo, kwa hiyo pamoja na ukarabati wa magari ya Serikali tupo tayari kusaidia," amesema Mganja.
Chanzo: Mwananchi