Makonda aonya Wanasiasa wanaolenga Urais 2030, aahidi kuwashughulikia wanaomsaliti Rais Samia

Makonda aonya Wanasiasa wanaolenga Urais 2030, aahidi kuwashughulikia wanaomsaliti Rais Samia

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Mbunge wa Arusha Mjini, Paul Christian Makonda amesema kuelekea mwaka 2030 wapo wanasiasa wengi wanaotaka kutumia shida za wananchi kupata uongozi Mkuu wa Nchi, akiahidi kushughulikia wale wote wanaopanga njama za kuharibu na kudhoofisha jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan ili kufanikisha ndoto zao za Urais.

Makonda amebainisha hayo leo Jumatano Machi 25, 2026 mkoani Arusha mbele ya Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba wakati wa mkutano wa mwaka wa wadau wa elimu kwa umma nchini, akiwaonya pia wateule wa Rais ambao wamekuwa wakitumia nafasi zao kupanga safu za kuwania Urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2030, akiahidi kutomsaliti Rais Samia Suluhu.

"Mimi tukiwa kwenye vita situmi mtu, nakuja mwenyewe kukushughulikia na nina bahati pia ya kusema na Mungu, watu wote hawa wanaojipanga na Urais hawawezi hata kushika Urais mwaka 2030, mtaniona hapa na hili wekeni kwenye kumbukumbu, hawatapata kwani Watanzania si wasahaulifu na pia tutaweka rekodi ulifanya nini awali na ukweli ni kuwa huwezi kuwa malaika dakika za mwisho kabla ya uchaguzi. Shetani ni shetani tu hata kama akizeeka”, amekaririwa Makonda.

Akibainisha kukerwa na kuona baadhi ya wanasiasa wakiwa kwenye mipango kuelekea 2030 pamoja na kutaja uzoefu wake katika siasa, Makonda ameeleza pia kushangazwa na maigizo ya baadhi ya wanasiasa ambao wamekuwa wakiigiza kusikiliza kero za wananchi, kuikosoa serikali pamoja na kutaka kujiweka kando na serikali, akimpongeza Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu kwa kusimama imara na Rais Samia Suluhu Hassan, kumtaka kutokatishwa tamaa na kuahidi kusimama na Rais Samia dhidi ya wote wanaompinga.

Makonda bhana ...
 
Duh...!, japo namkubali sana bosi wangu huyu, kwasababu mimi ni sehemu wa tuliompendekeza huyu awe RC DSM, tumelitoa pendekezi hili leo usiku wa saa 2:00 Nimemkubali Sana DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam, Chuma kikaona hiyo post ya JF, ilinyanyuliwa simu moja tuu!, usiku huo huo faili mezani!, ilipita siku moja tuu!, kesho yake ni tangazo kwenye bomba!.

Ni mimi nikashauri, Mafanikio ya Makonda ni Uthibitisho Wa Jiwe walilolikataa Waashi litafanywa kuwa Jiwe Kuu la Pembeni

Nikashauri Baada ya Magufuli, 2025 Makonda atatufaa sana kwasababu ana uthubutu kuliko hata JPM!

Aliporejea kama Mwenezi nilimpongeza, Bado kuna ubishi kuwa hiki ni chuma? Je, chuma hiki ni chuma kingine ila ni kama kile au chuma hiki ni kile kile kimerejea kivingine? kisha nikaeleza Nikimwangalia Makonda, mambo anayoyafanya namuona kama Magufuli

Ila nikampa angalizo muhimu sana Pongezi Paul Makonda kuifufua CCM kwa amsha amsha. Twende mdogomdogo ngoma ikivuma sana inakaribia kupasuka! baada ya angalizo hili, Makonda alingolewa kwenye uenezi akatupwa RC Arusha!. Inawezekana yeye aliona ni promotion!, it was demotion!. Anawezekani hamjui ni nani alisababisha awe demoted!. Hii kauli yake ya leo , itamgharibu big time!. Baada ya Rais Samia kushinda awamu yake ya pili kwa ushindi wa kishindo cha kura milioni 32, zilizopigwa asubuhi mpaka saa 5 vurugu zilipoanza, na CCM kushinda kwa asilimia 98%!, Rais Samia sasa hahitaji kutetewa kwa uchawa!, Mhe. Makonda amejibainisha kuwa yeye ana bahati kuzungumza na Mungu kuhusu 2030, kuwa hao wote wanaojipanga for 2030 wote hawapati!. I wish laiti Paulo angelijua...!, hiyo 2030 anayoizungumzia mbona ni mbali sana...!.

P
 
Baada ya kumaliza kuwashughulikia wanaSiasawa wa upinzani, sasa wamegeukiana na kuanza kuchapana wenyewe makonde ya nguvu kuhusu nani kuwa rais 2030 tena mapema sana hata ya Oct 29 hayajapoa wala kutolewa report yake.Acha wachapane maana washaanza kulalamika vifo vya ghafla vya wanasiasa wao!!
mbona mama hajajitanda hapo?
 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Mbunge wa Arusha Mjini, Paul Christian Makonda amesema kuelekea mwaka 2030 wapo wanasiasa wengi wanaotaka kutumia shida za wananchi kupata uongozi Mkuu wa Nchi, akiahidi kushughulikia wale wote wanaopanga njama za kuharibu na kudhoofisha jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan ili kufanikisha ndoto zao za Urais.

Makonda amebainisha hayo leo Jumatano Machi 25, 2026 mkoani Arusha mbele ya Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba wakati wa mkutano wa mwaka wa wadau wa elimu kwa umma nchini, akiwaonya pia wateule wa Rais ambao wamekuwa wakitumia nafasi zao kupanga safu za kuwania Urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2030, akiahidi kutomsaliti Rais Samia Suluhu.

"Mimi tukiwa kwenye vita situmi mtu, nakuja mwenyewe kukushughulikia na nina bahati pia ya kusema na Mungu, watu wote hawa wanaojipanga na Urais hawawezi hata kushika Urais mwaka 2030, mtaniona hapa na hili wekeni kwenye kumbukumbu, hawatapata kwani Watanzania si wasahaulifu na pia tutaweka rekodi ulifanya nini awali na ukweli ni kuwa huwezi kuwa malaika dakika za mwisho kabla ya uchaguzi. Shetani ni shetani tu hata kama akizeeka”, amekaririwa Makonda.

Akibainisha kukerwa na kuona baadhi ya wanasiasa wakiwa kwenye mipango kuelekea 2030 pamoja na kutaja uzoefu wake katika siasa, Makonda ameeleza pia kushangazwa na maigizo ya baadhi ya wanasiasa ambao wamekuwa wakiigiza kusikiliza kero za wananchi, kuikosoa serikali pamoja na kutaka kujiweka kando na serikali, akimpongeza Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu kwa kusimama imara na Rais Samia Suluhu Hassan, kumtaka kutokatishwa tamaa na kuahidi kusimama na Rais Samia dhidi ya wote wanaompinga.

Ccm kwa namna moja au ingine inakosea sana wananchi!
Yaani urais ushaonekana na ni deal!


Watanzania tuamkeni , inavoonekana tunapoenda hamna walichojifunza 2025!
 
Tatizo la hii nchi liko hapa! Yaani kuna watu wanapewa madaraka ya kuongoza wengine huku wakiwa hawana elimu ya uongozi!

Yaani kwenye hii nchi mtu anapewa nafasi ya uongozi kwa sababu tu ni kada wa ccm, ni chawa wa kiongozi fulani, ni ndugu au swahiba wa kiongozi fulani,, ni mtoto wa kiongozi fulani, nk.

Matokeo ya hayo mapungufu ndiyo haya sasa! Uropokaji kushamiri, wizi na rushwa kushamiri, upendeleo kushamiri, nk.
 
Back
Top Bottom