Jibaba Bonge
JF-Expert Member
- May 6, 2008
- 1,246
- 401
SPIKA wa Bunge, Anna Makinda, amekanusha madai kuwa amepata nafasi hiyo kupitia mkono wa mafisadi na kwamba Mungu wake alikuwa mlangoni kwake.
Hii si mara ya kwanza kwa Makinda kukanusha madai hayo yanayotolewa kupitia baadhi ya vyombo vya habari, vikidai kuwa ameingia katika nafasi hiyo kwa nguvu na ushawishi wa watu wenye fedha, ili kutengeneza mazingira ya baadaye ya kisiasa.
Hata hivyo akizungumza katika chakula cha jioni alichowaandalia waandishi wa habari za Bunge katika Hoteli ya New Dodoma juzi, Spika huyo alisema hajawahi kufikiria kuwa na urafiki na mtu yeyote ambaye ana tuhuma na wala hafikirii kuwatenga kwa kuwa yeye ni mtu wa watu wote.
"Mimi nitafanya kazi kwa kujiamini zaidi na kwa maslahi ya Watanzania wote maana mimi ndiye spika, wala siigizi kwa sababu niliingia pale kwa lengo la kuwatumikia wabunge kwa hiari yangu si kwa nguvu ya mtu,"alisema Makinda.
Spika huyo alisema hata katika kipindi cha kampeni za uspika zilizofanyika mwishoni mwa mwaka jana, alielezwa kuwa baadhi ya wagombea wenzake walikuwa wakifanya kampeni kwenye mabaa lakini aliendelea kupiga magoti na kumuomba Mungu wake kwa kuwa hakuwa na fedha.
Makinda alisema kipindi chake cha wa miaka mitano ya kuliongoza Bunge, anatarajia kukifanya chombo hicho kuwa kimoja na chenye malengo na maslahi ya nchi na si kwa watu binafsi.
Kuhusu waandishi wa habari za Bunge, aliwataka kuwa makini na kutumia kalamu zao kuiunganisha nchi kwa wimbo mmoja bila ya kuleta machafuko.
Alisema kalamu zao zinaweza kuleta mafanikio makubwa kama zitatumika vizuri na kwa kufuata misingi ya taaluma yao.
Waziri huyo wa zamani wa habari, alisema nia yake si kutaka kuwafunga midomo waandishi bali kuwafanya wasimame katika maadili.
"Sina nia ya kuwafunga midomo waandishi wa habari, nataka wawe huru kuandika habari kwa faida ya Watanzania kama ni kuonya, nataka waonye na kama ni kukosoa wakosoe pia lakini iwe ni kwa kila jambo ambalo ni la kweli bila kumuonea mtu," alisisitiza.
Souce; Mwananchi
Hii si mara ya kwanza kwa Makinda kukanusha madai hayo yanayotolewa kupitia baadhi ya vyombo vya habari, vikidai kuwa ameingia katika nafasi hiyo kwa nguvu na ushawishi wa watu wenye fedha, ili kutengeneza mazingira ya baadaye ya kisiasa.
Hata hivyo akizungumza katika chakula cha jioni alichowaandalia waandishi wa habari za Bunge katika Hoteli ya New Dodoma juzi, Spika huyo alisema hajawahi kufikiria kuwa na urafiki na mtu yeyote ambaye ana tuhuma na wala hafikirii kuwatenga kwa kuwa yeye ni mtu wa watu wote.
"Mimi nitafanya kazi kwa kujiamini zaidi na kwa maslahi ya Watanzania wote maana mimi ndiye spika, wala siigizi kwa sababu niliingia pale kwa lengo la kuwatumikia wabunge kwa hiari yangu si kwa nguvu ya mtu,"alisema Makinda.
Spika huyo alisema hata katika kipindi cha kampeni za uspika zilizofanyika mwishoni mwa mwaka jana, alielezwa kuwa baadhi ya wagombea wenzake walikuwa wakifanya kampeni kwenye mabaa lakini aliendelea kupiga magoti na kumuomba Mungu wake kwa kuwa hakuwa na fedha.
Makinda alisema kipindi chake cha wa miaka mitano ya kuliongoza Bunge, anatarajia kukifanya chombo hicho kuwa kimoja na chenye malengo na maslahi ya nchi na si kwa watu binafsi.
Kuhusu waandishi wa habari za Bunge, aliwataka kuwa makini na kutumia kalamu zao kuiunganisha nchi kwa wimbo mmoja bila ya kuleta machafuko.
Alisema kalamu zao zinaweza kuleta mafanikio makubwa kama zitatumika vizuri na kwa kufuata misingi ya taaluma yao.
Waziri huyo wa zamani wa habari, alisema nia yake si kutaka kuwafunga midomo waandishi bali kuwafanya wasimame katika maadili.
"Sina nia ya kuwafunga midomo waandishi wa habari, nataka wawe huru kuandika habari kwa faida ya Watanzania kama ni kuonya, nataka waonye na kama ni kukosoa wakosoe pia lakini iwe ni kwa kila jambo ambalo ni la kweli bila kumuonea mtu," alisisitiza.
Souce; Mwananchi