Makinda atabiria kifo CCM

Makinda atabiria kifo CCM

Candid Scope

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2010
Posts
11,897
Reaction score
6,933
IMG_7701.jpg
IMG_7626.JPG
​

  • "Upinzani hauwezi kuiua CCM ila CCM itajimaliza yenyewe kwa tabia yake" - Anne Makinda

CCM mazingira ya Kujiondoa yenyewe

SPIKA wa Bunge, Anne Makinda, amesema kuwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kinaweza kujiondoa chenyewe madarakani kutokana na tabia ya baadhi ya viongozi kutanguliza maslahi binafsi badala ya chama na wananchi kwanza. Makinda alitoa kauli hiyo juzi wakati akiwasalimu wajumbe wa mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM mkoa wa Njombe, waliokutana mjini hapa.


Utapeli, Rushwa kuiua CCM
Alisema utapeli ndani ya CCM unatisha na watu hawataki kujenga utamaduni wa ujamaa na kujitegemea na kusisitiza iwapo wanachama watashindwa kujitegemea, chama kitakufa. Alisema hata rushwa kwenye uchaguzi wa CCM inachangiwa na baadhi ya viongozi wasiopenda kufanya kazi na kutegemea kuchuma pesa za rushwa kutoka kwa wagombea.
“Rushwa ndani ya chama inatokana na tabia hii ya watu kushindwa kufanya kazi halali za kujitafutia kipato na kuishia kuwarubuni wagombea na kuwaomba fedha kwa ahadi ya kuchaguliwa. Iwapo wana CCM wataendelea kuomba fedha katika uchaguzi ni mwanzo wa kuua chama na hata vyama vya upinzani haviwezi kuiua CCM ila CCM itajimaliza yenyewe kwa tabia yake,” alisema.


Wabunge si ATM Machine
Alieleza kusikitishwa kwake na tabia ya baadhi ya wapiga kura wa jimbo lake ambao wamekuwa wakimchangamkia na kumsalimia na mwisho wa salamu, huishia kuomba pesa. Makinda amewataka viongozi wa CCM kurejea misingi ya kiapo cha mwachama na kukifanyia kazi kiapo hicho ambacho kinatamka wazi kuwa sitatumia cheo changu kwa maslahi yangu na iwapo kiapo hicho kitaendelea kukiukwa kwa baadhi ya viongozi wanaochaguliwa kugeuza nafasi zao ni mitaji ya kuombaomba fedha kwa wabunge, chama hicho hakitadumu.
“Mimi mwenzenu jana baada ya kumaliza mkutano wa mapokezi ya Mangula nilianza kucheza ngoma na muziki na wananchi waliofika katika mapokezi hayo, cha ajabu wengine walikuwa kukisalimia na kuniomba pesa ....sasa hii ni hatari sana kama watu wamekuja wenyewe katika mapokezi baada ya kumaliza mkutano, wanamvamia mbunge na kumwomba pesa,” alisema Makinda.


Kutokana na hali hiyo, Spika Makinda aliwataka wanachama wa CCM kufanya kazi na kuwa na shughuli nyingine za kuwaingizia kipato badala ya kuendelea kuwavizia wabunge na kuwaomba pesa na wasipopewa wamekuwa wakiwachukia na kukichukia chama. Makinda aliwataka pia wajumbe wa mkutano huo kuwa na miradi ya kiuchumi au kujiunga katika kilimo badala ya kuendelea kuomba fedha kwa wabunge.
Alisema hivi sasa watu wamechoka kuombwa fedha na hata waliokuwa wakikisaidia chama, pia wamechoka hivyo lazima CCM ijitegemee kwa kuwa na miradi ya kiuchumi.


 
Jibu hilo ni la upande Mmoja. Hajui kama huo utapeli unaofanywa na Wana-CCM umeibuliwa na CHADEMA?

Atake asitake CHADEMA tunazidi kuiua CCM.Tumeikata Mikono na Miguu tunasubiri time ifike tukate kichwa na sehemu zake zote.
 
Jibu hilo ni la upande Mmoja.Hajui kama huo utapeli unaofanywa na Wana-CCM umeibuliwa na Chadema?Atake asitake Chadema tunazidi kuiua CCM.Tumeikata Mikono na Miguu tunasubiri time ifike tukate kichwa na sehemu zake zote.

Siasa ni mchezo kama wa karata kumshika pabaya mpinzani wako. Kauli ya Makinda nakubaliana nayo kwa maana kwamba CCM isingeruhusu udhaifu na ulegelege uliopo sidhani kama upinzani ungekuwa na nguvu. Dhahiri CCM imajiua yenyewe.
 
Kwa hiyo ndio maana Makinda kaamua kutokugombea tena ubunge 2015 baada ya kupima upepo na kugundua kuwa CCM imekufa?!!!
 
Mama anajua kitu kinachoendelea na amejitahidi kuzungumzia ukweli kwamba
chama kinapotea kwa sababu ya mambo kadhaa aliyoyabainisha na nafikiri
chama bado kina hazina kubwa ya watu ambao wanaelewa mambo na wanatumia
nafasi hiyo kikikosoa.
Ni muda sasa umefika kuhakikisha kwamba mambo yanabadilika ndani ya chama
ili kuhakikisha kwambakinaenda na mabadiliko yanayohitajika.
 
Nadhani hao wananchi waliomuomba hela makinda wako sahihi. Wanaitikia wito uliotolewa bungeni na waziri mkuu pinda alipokuwa akitetea ili kuhalalisha mishahara minono na marupurupu ya kifisadi kwa wabunge. ". . . . . unatoka bungeni unakutana na mpiga kura wako anakusubiri ana shida ya nauli, unampatia . . . . . . . " by pinda.
makinda aliiunga mkono si tu kwa kutabasamu bali pia kwa kuyasifia majibu hayo kuwa ni mazuri.
serikali imeshindwa kutekeleza maazimio ya bunge, wananchi hawawezi shindwa!!!!!!
sasa itazidi kula kwaoo.
 
Mama anajua kitu kinachoendelea na amejitahidi kuzungumzia ukweli kwamba
chama kinapotea kwa sababu ya mambo kadhaa aliyoyabainisha na nafikiri
chama bado kina hazina kubwa ya watu ambao wanaelewa mambo na wanatumia
nafasi hiyo kikikosoa.
Ni muda sasa umefika kuhakikisha kwamba mambo yanabadilika ndani ya chama
ili kuhakikisha kwambakinaenda na mabadiliko yanayohitajika.

chama si muhimu kwetu, kinaweza kufa tu. muhimu kwetu ni nchi.
ni kujisumbua kumpamba maiti.
 
Jibu hilo ni la upande Mmoja. Hajui kama huo utapeli unaofanywa na Wana-CCM umeibuliwa na CHADEMA?

Atake asitake CHADEMA tunazidi kuiua CCM.Tumeikata Mikono na Miguu tunasubiri time ifike tukate kichwa na sehemu zake zote.

........

Mkuu ESI huo ndio uwezo wa CCM kujitafiti.
 
Sasa kama mliwazoesha kuwahonga hela wawachague kuna ajabu gani wakiwaomba hela leo? ndio yale yale mshapata sasa.
 
Kifo cha CCM hakihitaji utabiri. Labda angesema kitatokea lini ndio ingekuwa ni utabiri.

Hakuna chama kitakachotawala milele katika dunia hii.
 
Makinda haoni mapungufu yake, kwanza kujiamulia juu ya ripoti ya madini na nidshati, kuitolea hukumu, pili lazima watu wawaombe hele maana nyie mkilalamika pesa manpewa tu bila tatizo, watu wanawaomba pesa kuwaonesha bungeni mmekwenda kucheza wakati watu wanazidi kuwa na njaa, na wapinzani wana weza kuitoa CCM kama mtaacha kuchakachua "CCM inapendwa na mafisadi pamoja na watu ambao ni bongolala"
 
Back
Top Bottom