Makinda atabiria kifo CCM

Makinda atabiria kifo CCM

Tuanze kuimba mapambio na nyimbo za kumsifu mungu ccm chama hatunaye tena wamebaki magamba tuu dahh ccm wakulima na wafanyakazi walikupenda ila rushwa na ufisadi vilikupenda zaidi...R.I.P CCM
 
makinda ndo unaliona hili leo? na bado moto haujawaka. thank god i made it thru this yr pamoja na govt mbovu kama hii.
 
Huyu mama mpuuzi kwelikweli,yeye ndo ndo mbobezi wa kuweka maslahi binafsi mbele ya yale ya jamii pana,si bungeni hata kwenye mazingira yake anayoishi,ya bungeni wengi mnayajua,sisi majirani zake huku kijitonyama/sinza katusababishia adha ambayo inaendelea kutusulubu mpaka sasa.Katufungi njia pekee ambayo ilikuwa ni ya mkato kwa ajili ya extension ya nyumba yake(haya ni maslahi binafsi) hii ni barabara ambayo tumekuwa tukiitumia miaka nenda rudi.Sasa maslahi binafsi kwake ni sawa kwa wenzake yanaua chama,huu ni upuuzi na unafiki mtupu..Ama kweli unafiki ni moja ya sifa ya wanaccm.
 
Ha ha haa, mbavu zangu, eti kiwanda kimeanza kuzalisha kwa wingi....
 
Ndio anajua leo???? Namshauri Mheshimiwa sana Spika awe anapitaga huku JF tumekuwa tukiyasema haya tangu 2008-2009
 
makinda kasema kweli. utamadun wa kuomba hela wagombea unasababisha mgombea kutafuta njia zngne hata za ovyo ili awape hao wanaomuomba. halaf baadae akianza kufanya madudu ili arudishe hela za wa2 tunaishia kumwita fisad, mwiz, dhaifu, legelege, hana vision, kisa din yake, etc
 
mnafiki tu huyu mama angekuwa na uchungu na nchi yetu asingekuwa anazima hoja za wapinzani zinazododosa ufisadi, mwenyewe fisadi tuu!
 
IMG_7701.jpg
IMG_7626.JPG
​

  • "Upinzani hauwezi kuiua CCM ila CCM itajimaliza yenyewe kwa tabia yake" - Anne Makinda

CCM mazingira ya Kujiondoa yenyewe

SPIKA wa Bunge, Anne Makinda, amesema kuwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kinaweza kujiondoa chenyewe madarakani kutokana na tabia ya baadhi ya viongozi kutanguliza maslahi binafsi badala ya chama na wananchi kwanza. Makinda alitoa kauli hiyo juzi wakati akiwasalimu wajumbe wa mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM mkoa wa Njombe, waliokutana mjini hapa.


Utapeli, Rushwa kuiua CCM
Alisema utapeli ndani ya CCM unatisha na watu hawataki kujenga utamaduni wa ujamaa na kujitegemea na kusisitiza iwapo wanachama watashindwa kujitegemea, chama kitakufa. Alisema hata rushwa kwenye uchaguzi wa CCM inachangiwa na baadhi ya viongozi wasiopenda kufanya kazi na kutegemea kuchuma pesa za rushwa kutoka kwa wagombea.
“Rushwa ndani ya chama inatokana na tabia hii ya watu kushindwa kufanya kazi halali za kujitafutia kipato na kuishia kuwarubuni wagombea na kuwaomba fedha kwa ahadi ya kuchaguliwa. Iwapo wana CCM wataendelea kuomba fedha katika uchaguzi ni mwanzo wa kuua chama na hata vyama vya upinzani haviwezi kuiua CCM ila CCM itajimaliza yenyewe kwa tabia yake,” alisema.


Wabunge si ATM Machine
Alieleza kusikitishwa kwake na tabia ya baadhi ya wapiga kura wa jimbo lake ambao wamekuwa wakimchangamkia na kumsalimia na mwisho wa salamu, huishia kuomba pesa. Makinda amewataka viongozi wa CCM kurejea misingi ya kiapo cha mwachama na kukifanyia kazi kiapo hicho ambacho kinatamka wazi kuwa sitatumia cheo changu kwa maslahi yangu na iwapo kiapo hicho kitaendelea kukiukwa kwa baadhi ya viongozi wanaochaguliwa kugeuza nafasi zao ni mitaji ya kuombaomba fedha kwa wabunge, chama hicho hakitadumu.
“Mimi mwenzenu jana baada ya kumaliza mkutano wa mapokezi ya Mangula nilianza kucheza ngoma na muziki na wananchi waliofika katika mapokezi hayo, cha ajabu wengine walikuwa kukisalimia na kuniomba pesa ....sasa hii ni hatari sana kama watu wamekuja wenyewe katika mapokezi baada ya kumaliza mkutano, wanamvamia mbunge na kumwomba pesa,” alisema Makinda.


Kutokana na hali hiyo, Spika Makinda aliwataka wanachama wa CCM kufanya kazi na kuwa na shughuli nyingine za kuwaingizia kipato badala ya kuendelea kuwavizia wabunge na kuwaomba pesa na wasipopewa wamekuwa wakiwachukia na kukichukia chama. Makinda aliwataka pia wajumbe wa mkutano huo kuwa na miradi ya kiuchumi au kujiunga katika kilimo badala ya kuendelea kuomba fedha kwa wabunge.
Alisema hivi sasa watu wamechoka kuombwa fedha na hata waliokuwa wakikisaidia chama, pia wamechoka hivyo lazima CCM ijitegemee kwa kuwa na miradi ya kiuchumi.



NAKUMBUKA KATI YA MWAKA HUU NA MWAKA JANA PALIKUWA NA MJADALA MZITO WA POSHO BUNGENI NA KATIKA MAJIBU YA KIONGOZI MKUU WA SHUGHULI SERIKALI BUNGEN (WAZIRI MKUU) ALITETEA POSHO PAMOJA ONGEZEKO LA POSHO KWA HOJA KUWA WANANCHI WANAPELEKA SHIDA ZAO KWA WABUNGE, AKAWEKA BAYANA KUWA HATA WAKITOKA UKUMBINI WANANCHI HUENDA KUWAOMBA PESA NA HIVYO INAHALALISHA HIZO POSHO NA NI NDOGO KUFUATANA NA KAZI HIYO.

Mheshimiwa Spika nadhani alisahau hiyo kauli, hivyo wananchi kumuomba hela ni matokeo ya tamko la Waziri Mkuu, maana tayari imeshakuwa ni haki yao kwa sababu kodi zao zinaelekezwa pia kwa wabunge kwa minajili hiyo.

Nawasilisha
 
Jibu hilo ni la upande Mmoja. Hajui kama huo utapeli unaofanywa na Wana-CCM umeibuliwa na CHADEMA?

Atake asitake CHADEMA tunazidi kuiua CCM.Tumeikata Mikono na Miguu tunasubiri time ifike tukate kichwa na sehemu zake zote.
kwa hiyo hao watu wa ccm waliofanya ufisadi, wasingefanya chadema wangeibua nini? mbona unataka kuleta ushabiki? kwa hiyo wewe unataka kukataa kwamba ufisadi haujafanywa na watu ndani ya ccm? au umekariri kuitaja chadema sasa unaitaja hata isipohusika?
 
mnafiki tu huyu mama angekuwa na uchungu na nchi yetu asingekuwa anazima hoja za wapinzani zinazododosa ufisadi, mwenyewe fisadi tuu!
kwani wewe umejua kwamba kuna ufisadi kupitia nini?
 
Tuanze kuimba mapambio na nyimbo za kumsifu mungu ccm chama hatunaye tena wamebaki magamba tuu dahh ccm wakulima na wafanyakazi walikupenda ila rushwa na ufisadi vilikupenda zaidi...R.I.P CCM
hebu oanisha mchango wako na uzi hapo juu.
 
Kama wakati wanaomba kura walikuwa wanawalambisha fedha ambazo wao waliita takrima na ahadi lukuki kwamba wakichaguliwa kuwa wabunge watajenga barabara, shule, kila mwananchi atapata mikopo wakati ukweli mbunge ni kiungo cha wananchi na serikali katika kudai huduma za jamii. kwa mantiki hii ni rahisi kwa mwananchi kumwomba mbunge wake fedha kwa kuwa wabunge wengi kila maendeleo yanayotokea wanajifanya wao ndio wameyaleta jimboni wakati maendeleo yamekuja kutokana na ushirikiano wa taasisi nyingi zilizoko jimboni kwake including madiwani kupitia baraza la madiwani ambao ndio waamuzi wakuu wa mambo yote yanayotokea jimboni (lakini wabunge wengi wanavyopenda kujitutumua wanajifanya wao kila kitu)
 
Kama wakati wanaomba kura walikuwa wanawalambisha fedha ambazo wao waliita takrima na ahadi lukuki kwamba wakichaguliwa kuwa wabunge watajenga barabara, shule, kila mwananchi atapata mikopo wakati ukweli mbunge ni kiungo cha wananchi na serikali katika kudai huduma za jamii. kwa mantiki hii ni rahisi kwa mwananchi kumwomba mbunge wake fedha kwa kuwa wabunge wengi kila maendeleo yanayotokea wanajifanya wao ndio wameyaleta jimboni wakati maendeleo yamekuja kutokana na ushirikiano wa taasisi nyingi zilizoko jimboni kwake including madiwani kupitia baraza la madiwani ambao ndio waamuzi wakuu wa mambo yote yanayotokea jimboni (lakini wabunge wengi wanavyopenda kujitutumua wanajifanya wao kila kitu)

huyu bibi kadata si kidogo maana yeye mwenyewe ndo amekuwa kiongozi wa kukiua chama kwa kuzuia mijadala muhimu bungeni na ccm waliingia chaka kwa kumteua kuwa spika sijui hata vigezo ilikuwa ni nini spika wa ukweli alikuwa mh!6.
 
hebu oanisha mchango wako na uzi hapo juu.


Gamba smell



By JIULIZE KWANZA
Tuanze kuimba mapambio na nyimbo za kumsifu mungu ccm chama hatunaye tena wamebaki magamba tuu dahh ccm wakulima na wafanyakazi walikupenda ila rushwa na ufisadi vilikupenda zaidi...R.I.P CCM
 
huyu bibi kadata si kidogo maana yeye mwenyewe ndo amekuwa kiongozi wa kukiua chama kwa kuzuia mijadala muhimu bungeni na ccm waliingia chaka kwa kumteua kuwa spika sijui hata vigezo ilikuwa ni nini spika wa ukweli alikuwa mh!6.

Tatizo CCM ya sasa inaangalia maslahi ya kundi flani na ndio maana wanapanga safu ya uongozi kwa kuwa wameshafanya conclusion ya hatma ya nchi kwa muda wa miaka mitano hivyo wanaunda timu ya ufundi kuanzia watendaji wateuliwa mpaka nafasi zingine za kisiasa ili hoja zao ziwe zinapita bila kupingwa (in this case wanaogopa challenge kutoka wao kwa wao kama wanachama wakati wanatakiwa wabishane kwanza ili wafikie consensus wao wenyewe ndio itakuwa rahisi kwa kutetea baadhi ya mambo)
 
kwa hiyo hao watu wa ccm waliofanya ufisadi, wasingefanya chadema wangeibua nini? mbona unataka kuleta ushabiki? kwa hiyo wewe unataka kukataa kwamba ufisadi haujafanywa na watu ndani ya ccm? au umekariri kuitaja chadema sasa unaitaja hata isipohusika?
Mkuu naona una Mixed feelings kichwani hasa kati ya Chadema na CCM
 
Back
Top Bottom