Makavu Live - Mwanaume Jitume

ladyfurahia

JF-Expert Member
May 10, 2011
14,733
9,535
Habarini Wadau na wapenzi wangu

Leo mama mfundaji nimekuja na haya machache kuwasomesha WANAUME ambao ni Wavivu
hawajitumi kwa wenzi wao, Wengine hawawajali wala kuwatunza wake wao wanaona kama
kufanya hivyo wanaharibu wallet zao kumbe sivyo hapo ndo raha ya kunogesha pendo

Mwenzi / Mkeo hupenda kuona mwanaume unajituma kwa kila hali na mali kumtunza na kutunza
familia nzima kwani Mwanaume ni kichwa cha familia sio mwanamke ndo kichwa cha familia
hata maandiko yamesema hivyo kuwa kichwa ni DUME na sio JIKE, We uliona wapi jike likawa
kichwa si patachimbika humo ndani. Cha muhimu mwanaume jua sehemu zako za kutekeleza.

Tuangalie mambo ya msingi ambayo mwanaume yakusapa ujitambue wewe ni nani

a) Mwanaume jitambue umepewa jukumu zito na Mungu la kutunza familia:
Kuwa mwelevu wa kutekeleza mambo yako ya kifamilia usimwachie mwanamke atunze familia
nawe ukawa mvivu na mzembe familia nyingi zinateketea kutoka na msingi mbovu wa Mwanaume
kutotekeleza mambo yampasayo kufanya katika familia yake.

b) Katika suala zima la kimpenzi kimahaba nalo uwe wa kwanza kulitekeleza kwa ubunifu wa hali
ya juu. Tambua mwenzi wako anapenda nini ukimfanyia mnapokuwa faragha
Anapenda umpe maandalizi ya kutosha:
Mwanamke huhitaji mda huu kabla ya tendo ili kuamsha hisia zao na kulainisha uke wake vizuri tayari kwa kuingizwa! Asipopata mda mzuari wa maandalizi, tendo zima hugeuka kuwa la maumivu. Maandalizi mazuri pia ni njia nzuri ya kumsogeza kaziba na kilele sio kumkandamiza na
kumchosha na mhindi wako utadhani unatwanga mahindi. Jipeni raha wenyewe kwa wenyewe
kwani Mungu aliweka kitu hicho tujipe kwa raha sio kwa karaha jamani mabestito wangu.

c) Muulize ni kitu gani hasa anatamani umfanyie kitandani:
Kila mtu ni tofauti inapokuja kwenye swala zima la ngono. Njia pekee ya uhakika ya kujua nini mwanamke anapenda kutoka kwako ni kumuuliza. Udadisi wako unaweza pia kumfanya akutamani zaidi. Hauhitaji kuwa mtanashati ili kumridhisha mwanamke kimapenzi! Unahitaji udadisi kidogo na kujifunza zaidi naye ataridhika kabisa wala hatokusumbua tena.

d) Mwanaume usiwe mmbea wala muongeaji kama cherehani yenye morta
Wanawake wengi hawapendi mwanaume muongeaji kama amewekewa kipump cha kusukuma maji
mdomoni mwake hawapendi mwanaume mmmbea kama anajenga helikopta ya umbea.

Wanawake hawapendi mwanaume ambaye mambo ya chumbani anayatoa hadharani kama
hajafundwa huko kwao au kufanyiwa bag party. Mabestito wanaume jirekebisheni si ustaarabu kutoa vitu vya chumbani na kumdhalilisha mkeo/ mwenzi wako. Ndoa haijengwi hivyo bali ndoa
ni kuvumiiliana, kupendana, kufichiana mambo yenu, kusaidiana, kuelekezana na mengineyo.

Natumai wanaume mtajirekebisha na kufanya wajibu wa familia zenu na kujenga nyumba zenu.

Wasalaam;

Lady f.
 
Kesho uje makavu live kwa wanawake....ili at least akidi itimie
 
Nafikiri tu....neno MEBESTITO tu limetosha kuonesha kuwa hukumanisha WANAUME.;);)
 
Tangu enzi za primitive lives, wajibu wa mwanaume ulikuwa:
1.Kulinda familia kwa kuiepusha na maadui pamoja na wanyama wakali.
2.Kutunza familia kwa kuwinda na kuleta msosi home
3.Mechanical works kama kujenga pango (cave)lipia.
4.Kuongoza kundi/ukoo
5.Kuhakikisha ukoo unasonga mbele kwa kuzalisha.

WAJIBU WA MWNAMKE ULIKUWA:

1.Kuweka mazingira ya nyumbani ktk hali ya usafi.
2.Kutunza familia, yaani watoto na mume(wapikiwe, wavae na kulala pasafi)
3.Kulea watoto.n.k

Kwa ufupi mwanaume alikuwa ni family provider and protecter, na mwanamke alikuwa ni family nurture. Ila tangu ww2 imalizike na KE kuanza kufanya kazi na kupata pesa, wanawake walichanganyikiwa totally, hawajui wanataka nini kati ya matunzo au 50/50.
 
Tangu enzi za primitive lives, wajibu wa mwanaume ulikuwa:
1.Kulinda familia kwa kuiepusha na maadui pamoja na wanyama wakali.
2.Kutunza familia kwa kuwinda na kuleta msosi home
3.Mechanical works kama kujenga pango (cave)lipia.
4.Kuongoza kundi/ukoo
5.Kuhakikisha ukoo unasonga mbele kwa kuzalisha.

WAJIBU WA MWNAMKE ULIKUWA:

1.Kuweka mazingira ya nyumbani ktk hali ya usafi.
2.Kutunza familia, yaani watoto na mume(wapikiwe, wavae na kulala pasafi)
3.Kulea watoto.n.k

Kwa ufupi mwanaume alikuwa ni family provider and protecter, na mwanamke alikuwa ni family nurture. Ila tangu ww2 imalizike na KE kuanza kufanya kazi na kupata pesa, wanawake walichanganyikiwa totally, hawajui wanataka nini kati ya matunzo au 50/50.
mkuu umenisaidia sana kuongezea haya mambo ungependa nayo niweke pale kwenye thread yangu
 
Hamna shida kwenye hilo...ila mnatuacha dilema....mnataka nini??? matunzo au 50/50???
hahahahaaaaaaaaaaaaaaaaa kwani hujaona pale juu kwenye thread wanawake tunataka nini kwenu
rudia kusoma tena hahahahaaaaaaaaaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom