Makapuku Forum

Watafiti wa Chuo Kikuu cha Würzburg nchini Ujerumani waligundua kuwa watoto wachanga huanza kuiga mtindo wa lafudhi na intonation ya lugha ya mama zao tangu wakiwa tumboni, na wanapozaliwa, hulia kwa kufuata melodi hiyo.

Kutokana na Kiswahili kuwa na mkazo (accent) unaoangukia karibu kila mara kwenye silabi ya pili kutoka mwisho ya neno (penultimate stress), hivyo watoto hulia kwa sauti zenye mdundo unaotabirika na wenye usawa (rhythmic and balanced).
 
Je, umewahi kujiuliza kwa nini inakuwa ngumu sana kuacha kutazama tamthilia (series) au kusoma riwaya fulani, hasa pale inapofika mwisho wa sehemu moja na kuandikwa "Inaendelea..."? Akili yako inakuwa haina amani na unajikuta una shauku kubwa ya kujua nini kinafuata.

Basi sababu ndio hiyo, kisaikolojia inajulikana kama The Zeigarnik Effect.
 
Kwa nini bado tunafundishwa tano? Inaaminika kuwa mfumo huu ulianzia kwa mwanafalsafa wa Ugiriki, Aristotle, ambaye aliorodhesha tano tu (kuona, kusikia, kunusa, kuonja, na kugusa).

Kwa kuwa hizi ndizo zinazoonekana kwa urahisi zaidi na zinategemea viungo maalum (macho, masikio, pua, ulimi, na ngozi), zimebaki kuwa kama msingi wa mwanzo zaidi kuelewa kuhusu ufahamu.
 
Filamu hii iligharimu zaidi ya takriban $150M kuitengeneza sawa na Tshs. Bilioni 300 kwa thamani ya mwaka 2015. Mapato yaliyopatikana yalikuwa ni $380M sawa na Tshs. Bilioni 760.
 
Ili kuwalinda wasitoweke tena baada ya ujenzi wa bwawa la umeme, serikali iliweka mfumo wa bomba zinazopuliza maji (sprinklers) saa 24 ili kutengeneza ukungu wa bandia unaofanana na ule wa asili wa maporomoko ya maji.
 
Wadudu kama 'mende' wanachukuliwa kuwa "chakula cha baadaye" na rafiki bora zaidi kwa mazingira na gharama kwa sababu wanahitaji maji na chakula kidogo, pia nafasi ndogo zaidi kuzalishwa kuliko ng'ombe, huku wakitoa virutubisho vilevile au zaidi.

NB: Hapa wanaozungumziwa ni mende safi waliofugwa kwa ajili ya chakula!
 
Ili betri yako idumu kwa muda mrefu, jitahidi kuifanya simu iwe kwenye hali ya ubaridi na epuka kuichaji hadi 100% kila wakati; kuifanya iwe kati ya 20% na 85% ndiyo njia bora zaidi ya kuitunza.
 
Instagram imetangaza rasmi kuwa sasa itapunguza kwa kiasi kikubwa uwezo wa kufika mbali (reach) kwa akaunti ambazo zinategemea zaidi kuriposti maudhui ya watu wengine.

Hatua hii ni mwendelezo wa kampeni ya Instagram ya kutoa kipaumbele kwa maudhui asilia (original content).

Mambo makuu katika mabadiliko haya:

- Akaunti za "Aggregator": Akaunti zinazokusanya picha na video za watu wengine na kuzipandisha upya (bila kufanya mabadiliko makubwa) hazitapendekezwa tena kwenye sehemu za Explore au Reels kwa watu ambao hawazifuati.

- Kutoka Reels hadi Picha: Sheria hizi ambazo awali zilikuwa kali zaidi kwenye Reels, sasa zimeingia hadi kwenye picha za kawaida na carousels (zile posti za picha nyingi za kusogeza).

- Kiwango cha Adhabu: Imeripotiwa kuwa akaunti zinazoposti zaidi ya maudhui 10 ya kuriposti ndani ya siku 30 zinaweza kuondolewa kabisa kwenye mifumo ya mapendekezo ya Instagram.

Instagram inataka kuhakikisha kuwa watengenezaji wa maudhui asilia ndio wanaopata wafuasi wapya na sifa (credit), badala ya akaunti zinazofanya "copy and paste.
 
Unapofanya jambo geni, unatumia sehemu ya mbele ya ubongo (Prefrontal Cortex) ambayo uhitaji umakini na nguvu nyingi.

Baada ya kurudia rudia kwa muda mrefu, kitendo hicho huhamishwa kwenye sehemu inayoitwa Basal Ganglia, ambayo inahusika na kuratibu kazi tunazofanya bila kufikiria (kama kufunga kamba za viatu).

Siku 66 ni muda unaohitajika kwa uhamisho huo wote kukamilika kikamilifu.
 
Nauli ya kufika hapo kwenye huu mji bei gani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…