Makapuku Forum

Mkazi wa Kijiji cha Lupande Kata ya Mawengi Wilaya ya Ludewa Mkoani Njombe, Joseph Haule (25), amehukumiwa kifungo cha miezi 11 jela au kulipa faini ya Tsh. 300,000 baada ya kukiri kumtolea lugha ya matusi kwa maandishi Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Ludewa (OCD) SSP Deogratius Masawe, hukumu hiyo imetolewa jana November 16,2021 katika Mahakama ya Mwanzo Mlangali, Ludewa.

Imeelezwa kuwa Mtuhumiwa huyo aliandika ujumbe wa matusi baada ya Mama Mkwe wake Berdeta Njelekela kutoa malalamiko ya kunyanyaswa kwa Mtoto wake ambaye ni Mke wa mtuhumiwa huyo katika mkutano wa hadhara uliofanyika 12/11/2021 ukiongozwa na OCD huyo pamoja na wawakilishi wa dawati la jinsia kutoka ofisi ya Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Njombe.

Baada ya kutolewa malalamiko hayo ya unyanyasaji Masawe aliagiza Joseph na Mkewe Grace Lawrence wafike Kituo cha Polisi Mlangali ili waweze kusikilizwa migogoro yao ambapo katibu wa kitongoji Macarius Haule alifikisha barua ya wito lakini alijibiwa na Joseph kuwa hawezi kufika kufika kituoni hapo, Grace alifika kituoni huku akiwa na barua ya wito waliyopelekewa ambayo chini yake iliongezewa maandishi yenye matusi kutoka kwa Joseph akisisitiza kuwa haendi kituoni hapo na OCD hamfanyi chochote.

Grace alieleza kuwa ujumbe huo umeandikwa na Mume wake na kumkabidhi ili aifikishe kituoni huku akikiri kupata manyanyaso kutoka kwa Mume wake ambapo jeshi la polisi lilichukua hatua ya kumtafuta Mtuhumiwa na kufanikiwa kumkamata jana November 16,2021 na baada ya kukiri kosa akafikishwa Mahakamani.
 
Jeshi la Polisi Mkoani Pwani linawashikilia Watu wanane kwa tuhuma za kulishambulia na kulivunja vioo kwa kutumia mawe Bus la Sauli lililosababisha ajali iliyoua abiria mmoja wa Bodaboda Kibaha jana, mawe hayo yalimjeruhi pia Askari.

RPC wa Pwani, Wankyo Nyigesa amekemea vikali tabia ya Wananchi wachache kujichukulia sheria mkononi kwa kisingizio cha hasira kali kama ilivyotokea katika tukio hilo.

"Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani halitavumilia mihemko ya Watu wachache wasiopenda kutii sheria, tunakusudia kufanya operesheni kali ili kuwakamata wote waliohusika kuharibu na kurusha mawe ambayo pia yalimjeruhi askari Polisi wa Usalama Barabarani aliyekuwa eneo hilo akifanya kazi za kuongoza magari"

"Askari huyo F.3490 SGT Okoka Mbafu amelazwa Hospitali ya Tumbi baada ya kushambuliwa kwa mawe alipofika eneo la tukio kwa ajili ya kuchukua hatua"——— RPC Nyigesa
 
Polisi Mkoani Pwani wanamshikilia Dereva wa Bus la Sauli, Titto Gadau (32), Mkazi wa Mbezi Dar es Salaam kwa kosa la kulipita gari lililokuwa limesimama na kisha akagongana na Bodaboda iliyokuwa inakuja mbele yake eneo la Mathias Wilaya ya Kibaha jana na kusababisha kifo cha abiria wa Bodaboda hiyo, Emma Nambole huku Dereva wa Bodaboda Edwin Mwenda akijeruhiwa.

RPC Pwani, Wankyo Nyigesa amesema mwili wa Marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa Tumbi ili kufanyiwa uchunguzi wa kitabibu na Dereva wa pikipiki (majeruhi) amelazwa katika Hospitali ya Rufaa Tumbi.

Nyigesa amesema chanzo cha ajali ni uzembe wa Dereva wa Bus kulipita gari lililokuwa limesimama na matokeo yake akagongana na pikipiki iliyokuwa inakuja mbele yake.
 
Staa wa Cameroon na FC Barcelona Samuel Eto’o leo saa 15:00 EAT anawasilisha fomu za kuwania Urais wa Shirikisho la soka Cameroon (FECAFOOT), Eto’o anawania Urais na Rais wa sasa wa FECAFOOT Seidou Mbombo Njoya ambaye anatetea kiti chake.

Wengine wanaowania nafasi ya Urais ni pamoja na Denis Onana na Maboang Kessack ila Eto’o anatajwa kama mshindani mkuu na mwenye nguvu zaidi ya Seidou Mbombo Njoya
 
Kundi la Wanawake saba wa Australia ambao baadhi yao wanadai walifanyiwa uchunguzi wa kimatibabu baada ya Mamlaka kumkuta Mtoto mchanga katelekezwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Doha, wanapanga kuishtaki Serikali ya Qatar, Wakili wao amesema.

Inaelezwa kwamba wakiwa Doha, Qatar October 2020 Wanawake hao wanadai waliambiwa washuke kwenye ndege yao ya Qatar Airways na kulazimishwa kukaguliwa bila ridhaa yao bika kupewa maelezo ya wazi ni nini kinaendelea ambapo yote hiyo iligundulika ilikua ni msako wa kumtafuta Mama wa Mtoto huyo mchanga aliyekutwa kwenye mfuko wa plastiki ndani/kando ya pipa la taka kwenye moja ya vyoo vya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hamad.

Kufuatia kupatikana kwa Mtoto huyo mchanga, zaidi ya Wanawake 18 kutoka kwenye ndege 10 tofauti wakiwemo raia 13 wa Australia waliokuwa kwenye ndege inayoelekea Sydney walihusishwa kwenye vipimo hivyo baada ya kutolewa ndani ya Ndege na Askari wa Qatar wenye silaha na kufanyiwa uchunguzi wa kimwili kwenye Ambulance ya uwanja wa ndege. MillardAyoUPDATES ( via CNN )
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…