Nililijua hili...Machinga Jijini Dar es Salaam wameongezewa siku 12 kuanzia leo kuhama maeneo yasiyo rasmi ya kufanya biashara.
Kuondoka kwa wafanyabiashara hao mwisho ilikuwa iwe leo Oktoba 18,2021 baada ya kutolewa kwa siku 30 ambazo zilianza Septemba 18.
Nyongeza hiyo ya ya siku 12 imetolewa leo Jumatatu Oktoba 18, 2021 na Mkuu wa Mkoa huo, Amos Makalla alipokuwa akizungumza na wafanyabiashara wa Kariakoo kuhusiana na mpango huo wa kuwaondoa.View attachment 1978638