Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais ( Muungano na Mazingira), Selemani Jafo amepiga marufuku uingizaji, uzalishaji, usambazaji na matumizi ya mirija ya plastiki inayotumika kwenye unywaji wa maji na vinywaji baridi baada ya miezi sita kuanzia October 11, 2021 pia amesema Serikali inaelekeza wazalishaji bidhaa hizo wajielekeze kuzalisha mirija iliyo rafiki kwenye mazingira na kuepuka matumizi ya mirija ya plastiki ambayo haiwezi kurejelezeka.
"Katika kutunza na kuhifadhi mazingira, Serikali inaelekeza wenye hoteli, migahawa na maduka mbalimbali yanayotumia mirija ya plastiki katika kunywa maji na vinywaji mbalimbali, kuanza kutumia mirija ambayo ni rafiki wa mazingira ikiwemo mirija iliyotengenezwa kwa kutumia mali ghafi kama vile mirija iliyotengenezwa kwa karatasi, miti, nk."
"Baada ya miezi sita kuanzia October 11 , 2021, itakuwa ni marufuku kwa wenye hoteli, baa, na maeneo mengine ya kibiashara kuendelea kutumia mirija ya plastiki kama chombo cha kunywea vinywaji"——— JAFO
View attachment 1970662