Makapuku Forum

Muziki: Kimya Kinaendelea

...ni bila maneno, ni bila salamu na ni kwa sababu tukipeana 'Hi' ya kimyakimya hakuna tofauti na ile ya kuambiana maneno. nakupenda kapuku na uwepo wako hapa unanifanya niwe na tabasamu kila wakati.


 
Tafasiri Unavyoweza: Siku ya Wanawake Wanatangulia Wanaume, Safari Bado Ndefu


Kila jinsi (sex) na siku yake, ipo siku ya wanaume na leo ni siku ya wanawake, wapo kwenye siku yao na siku hii ina historia ya kuvutia kusoma. Ilianza kuadhimishwa nchi za Magharibi na kusambaa zaidi karne ya 20, kuanzia magharibi hakumaanishi Africa, Tanzania kwa mfano na makabila yake hayakuwa yakithamini wanawake na kuwakumbuka kila mwaka kwa sherehe na mambo mengi mengine. Fuatilia jinsi makabila yetu yanavyomchukulia mwanamke na hapa ndipo utajua kuna jambo zuri kujifunza wengine wanafanya nini kuwaenzi wanawake zao na sisi tunafanya nini kuwaenzi wanawake katika jamii etu. Binafsi natoka kwenye kabila ambalo mwanamke ana nafasi kubwa ya kuitengeneza asubuhi yako na kukuletea jioni nzuri ukimheshimu na hata kusalimiana tunasalimiana kwa jina la mwanamke. Tafasiri unavyoweza.

Bado kuna changamoto kubwa sana ya usawa wa kijinsia katika jamii yetu leo, wanawake walio wengi wanaishi kwenye umaskini na utegemezi usio na mfano ukilinganisha na wanaume. Ndiyo, wapo wanawake wenye madaraka makubwa nchini na wengine wanashika nafasi nyeti za maamuzi katika jamii lakini unajua takwimu za sensa zinaonesha kuwa wanawake ni wengi kuliko wanaume na vipi sasa uwiano kwenye vyombo vikubwa vya maamuzi kama bunge, serikali na mahakama idadi yao ni ndogo sana, tafasiri unavyoweza. Kuna vikwazo vingi wanakumbana navyo kuanzia ndani ya nyumba, kwenye nyumba za ibada, shuleni, makazini na hata serikalini. Tafadhari bila kulali wewe ni mwanamke au mwanaume usiwe kikwazo cha kuifikia safari ya usawa wa kijinsia

Sijamaliza kuandika nikiamini kabisa utamalizia maana nimeandika kama kuchokoza tu mada na kukufanya utafasiri unavyoweza katika kusheherekea siku hii nzuri ya wanawake kimataifa. Ukijitafakarisha ni vipi pamoja na kelele nyingi za usawa wa kijinsia bado kundi kubwa la watu kiidadi linaongoza kwa umaskini, kukosa elimu, utegemezi, kuonewa kisheria na zaidi kunyanyaswa kijinsia. Tafakari na tafasiri unavyoweza.

Hongera wanawake wote mlio Makapuku forum, BlessedHope , Jimena , Shunie , husna muba , ABJ , demi Valentina , Sakayo , Clkey , Tumosa , Linamo , Madame S , na wewe mwanamke ambaye sijakutaja jina lako ila amini tu kuwa wewe unalifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri sana kuwepo. Hongera na endelea kufurahia siku hii
 
Mr obe naomba wimbo wa sweet mother!!! Sijui kaimba nani hata


...wimbo wa zamani sana na haujaisha utamu,ulichezwa mwaka 1974 nimezaliwa nimeukuta ukiwa na miaka kumi radioni uliimbwa na Nico Mbarga (sio Nico Zengekala aliyeimba Solemba), huyu alikuwa ni Mkameroon upande wa baba na mama Mnigeria.

Nitaucheza
 
Muziki: Umeumbwa na Bahati


...hakuna namna na ni lazima niseme, kama kuna siku ambazo nimewahi kumuona anko wangu Lyon Lee akiwa mpole, kajituliza na aunt yangu basi ni jioni ya leo kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake kimataifa. walinikaribisha kama mgeni mwenyeji. Nikusalimie Kapuku wewe na kukutakia wakati mzuri tunapoenda kuikamilisha siku ya wanawake kimataifa.

Kuna changamoto nyingi zinapitiwa na wanawake katika kufikia usawa wa kijinsia katika maeneo mbalimbali iwe ndani ya nyumba, ofisini na kwenye jamii nzima. tunajua kwa namna gani wanawake wanakuwa na wakati mgumu kujikomboa kiuchumi, kielimu, kiutamaduni na kimaamuzi.

Nitaongelea kiutamaduni ambapo inafikia wakati mwanamke anakuwa hana uhuru wa kuamua avae nini, yaani mwili wake halafu wanaume ndo wanampoangia cha kuvaa na mjoma wangu asipobadilika kwenye kumpangia mavazi aunt yangu basi wote tumkataze kukaa anageukageuka nyuma akipishana na wanawake waliopendeza kwa mavazi wanayoyapenda wao.

Muziki sasa, niliwataja wanawake wote wa MF kwenye kipengele cha Tafasiri Unavyoweza, ninyi mnatupa sababu ya kuwa na tabasamu humu ndani

 
Asante sana
 
Muziki wa Mdhamini: Mama Yangu Ni Mwanamke

...ni bahati iliyoje nikikupa siri ambaye inawezekana ulikuwa huijui. Ninakuambia kwa sababu wewe ni nmtu mzuri na kila wakati unanipa sababu ya mimi kuja hapa makapuku Forum na kufurahia, siri yenyewe ni ndogo sana, niliitunza siku nyingi ila leo nitakuambie na ukiweza katangaze wengine wajue kuwa mama yangu ni mwanamke.

Tufurahie muziki wa mdhamini Sakayo ambaye anataka tufurahi pamoja naye, hakusema anaudedicate kwa nani lakini kwani kuna ubaya kufurahia muziki unaochezwa kwa jirani?

Nitaweka clip mbili za wimbo mmoja, mmoja ni 'original version' na nyingine ni umeimbwa upya 'remix'
Originale





Remix
 
Barikiwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…