Makanisa 2 yombo nusura kuchomwa moto, maaskofu lutheran watoa salamu juu ya vitendo

Jicho la Tai

JF-Expert Member
Oct 10, 2012
1,449
574
Watu wasiofahamika usiku wa kuamkia leo wamevamia kanisa la kilutheri Yombo jijini Dar es salaam kwa lengo la kufanya uharibifu kanisani hapo majira ya saa 9 kasoro za usiku lakini walinzi wa kanisa hao walifanikiwa kuzuia zoezi lao hilo.

Kwa mujibu wa mmoja wa watu waliofika kutoa msaada baada ya walinzi hao kugonga kengele iliyowaamsha wakazi wa eneo hilo ambaye pia husaidia kazi ya ulinzi kanisani hapo bwana Hosea Mbwambo amesema vijana wapatao saba waliingia kanisani humo kwa kuruka ukuta kwa nia ya kwenda madhabahuni lakini mlinzi aliyekuwepo aliwaambia mnataka nini ndipo walipomfuata nakusema kwamba tunakutaka wewe nakuanza kumpiga kabla mlinzi mwingine aliyekuwepo gorofani kushuka ili kusaidia ndipo vijana hao wakagundua kwamba kuna walinzi wengi hivyo kuamua kutimua mbio lakini wakiwa wamemuachia jeraha mlinzi Nkya ambaye alipelekwa hospitali ya Buguruni kisha Amana kwa matibabu zaidi hali yake inaendelea vizuri pia ulinzi ukiwa umeimarishwa kanisani hapo.

Pia habari ambazo GK imezipata kutoka kwa chanzo kingine cha habari ikiwemo Wapo Radio Fm inasema kwamba watu wasiofahamika waliwasha moto katika kanisa la Faraja International Gospel lililoko huko huko Kiwalani ingawa watu waliweza kuudhibiti baadaye. Wakati huo huo maaskofu wapatao 20 wa kanisa la Kiinjili la Kilutheri nchini (KKKT) wakiongozwa na mkuu wa kanisa hilo Dkt. Alex Gehaz Malasusa, wamekutana hii leo katika kanisa lililofanyiwa uharibifu la Mbagala na kutoa tamko zito juu ya vitendo vilivyofanywa na waumini wa dini ya kiislamu dhidi ya makanisa ya eneo hilo.

Chanzo: Samsasali.blogspot.com
 
Back
Top Bottom