Makamu wa rais dkt bilal azindua rasmi maghorofa 30 ya kambi ya polisi barabara ya kilwa

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,318
33,125
[h=3] [/h]
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa msimamizi wa Mradi wa ujenzi wa Maghorofa 30 ya Kambi ya Polisi, Dkt. Huba Nguluma, wakati wa uzinduzi wa majengo hayo uliofanyika jana Agosti 16 Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Kulia kwa Makamu ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha. Pichani juu: Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata utepe kuzindua Maghorofa 30 ya Kambi ya Polisi yaliyopo Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam jana Agosti 16. Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha (kulia) ni Inspekta Jenerali wa Polisi, Said Mwema.


Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha, baada ya kuwasili katika viwanja vya maghorofa 30 ya Kambi ya Polisi Barabara ya Kilwa kwa ajili ya kuyazindua rasmi jana Agosti 16.
Wasanii wa kikundi cha Kwaya cha Polisi, wakitoa burudani wakati wa sherehe za uzinduzi wa maghorofa 30 ya Kambi ya Pilisi Barabara ya Kilwa, yaliyozinduliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal.
Inspekta Jenerali wa Polisi, Said Mwema, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi huo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi huo.

Baadhi ya maofisa wa jeshi la Pilisi waliohudhulia hafla hiyo ya uzinduzi, wakisikiliza kwa makini Hotuba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal.Picha na Muhidin Sufian OMR.
 
MziziMkavu,
Nimekuwa nafuatilia kuhusu matukio katika picha hasa zako. Nimeona una 'passion' na mambo ya picha.
Picha nyingi unazoleta hapa zinakuwa katika vyombo vingine vya habari, lakini unavyoziweka hapa huwa ni clear na zina mvuto mzuri sana.
Ile clarity yake na unavyozipanga zinapendeza sana. Thank you for that!

Unakitu fulani lakini hujagundua, please work on that ! explore it.
 
Back
Top Bottom