MATHIAS KABYEMERA
JF-Expert Member
- Mar 7, 2013
- 1,793
- 573
Hainiingii akilini kufuta sherehe za uhuru na Muungano ukabakiza mwenge wa uhuru wa kuzinsua shimo la choo na miradi isiyona tija!
6. Ni ishara ya matumaini, upendo na umoja wa taifa letuMimi najua utamu wake,
1) wakimbiza mwenge wanachinjiwa ng'ombe na mbuzi bure
2) Fedha za halmashauri (magari na wafanyakazi vinatumika including kutumia fedha zisizohusika)
3) Kila unapolala mwenge lazima kuwe na mkesha - music, pombe na wanawake - UKIMWI njenje
4) Allowance tamu kwa wote.....
5) Ongeza zako.....
Ni kuwaonea watu na viongozi wa dini wanakaa kimya, siwataki hawa watu . Wao ndio wa kuwasemea watu sio wananyamaza kwa vile yao yanawanyookea![]()
Alisema nia hiyo ya kuwepo kwa Mwenge wa Uhuru kama alivyomnukuu Baba wa Taifa, inaendana na dhana ya kutumbua majipu katika Serikali ya awamu ya tano.
By Matern Kayera, Mwananchi Digital
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amezindua rasmi mbio za Mwenge wa Uhuru kwenye Uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro leo.
Katika uzinduzi huo, Makamu wa Rais alimnukuu Baba wa Taifa, Mwl Julius Nyerere akisema kuwa nia ya Mwenge wa Uhuru tangu mwanzo ni kumulika mipaka ya nchi yetu dhidi ya maadui, kuleta matumaini pale ambapo hakuna matumaini, kuondoa chuki pale ambapo kuna chuki na kuleta heshima pale ambapo kuna dharau.
Alisema nia hiyo ya kuwepo kwa Mwenge wa Uhuru kama alivyomnukuu Baba wa Taifa, inaendana na dhana ya kutumbua majipu katika Serikali ya awamu ya tano. Alisema utumbuaji majipu unalenga kuleta matumaini kwa wananchi ambao wamekata tamaa na kuleta heshima kwa wananchi waliodharauliwa.
“Kaulimbiu ya mbio ya za mwenge mwaka huu ni hii: Vijana ni nguvu kazi ya taifa, washirikishwe na wawezeshwe,”alisema Makamu wa Rais na kuongeza kuwa vijana ambao ndiyo nguvu kazi ya taifa hawajatumika ipasavyo kutokana na sababu mbalimbali.
Alizitaja baadhi ya sababu au changamoto zinazowakabili vijana nchini kuwa ni ukosefu wa ajira, uwezo mdogo wa kuajiri kwenye soko la ajira, ukosefu wa mitaji rafiki kwa vijana, maeneo ya kufanyia kazi pamoja na mitazamo hasi kwa baadhi ya vijana kwa kuchagua kazi.
Makamu wa Rais pia amewataadharisha vijana kutokana na ongezeko kubwa la maambukizi ya ukimwi na matumizi ya madawa ya kulevya. Amesema vijana wenye umri kati ya miaka 16-24 ndiyo wanaongoza kwa kuathiriwa na maambukizi ya ukimwi. Amesema athari za ukimwi na madawa ya kulevya kwa vijana ni kubwa lakini pia zinaongeza mzigo kwa jamii na serikali katika kuwatibu, kuwahudumia na kuongezeka kwa vifo.
Kwa upande wake, Waziri Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama, amemtambulisha George Jackson Kijimba kuwa ndiye kiongozi wa mbio za mwenge mwaka huu akisaidiana na wakimbiza mwenge wengine watano. Alisema sherehe za kuhitimisha mbio hizo za mwenge wa uhuru zitafanyika mkoani Simiyu tarehe 14 Oktoba mwaka huu.
Maisha bora kwa kila mtanzaniaHii miradi inayozinduliwa kila mwaka ingekuwa na mafanikio au manufaa huenda leo Tanzania ingelikuwa ni moja ya nchi tajiri sana na wananchi wake wanaishi maisha mazuri sana.
Lakini gharama za mafuta ya magari, mafuta ya mwenge wenyewe, posho za wakimbiza mwenge; hii ni pesa nyingi sana endapo kama serikali wangetafakari na kuufuta kabisa huu ukimbizaji wa mwenge wa uhuru, hii pesa ingetumika katika shughuli za maendeleo na pia utengenezaji wa madawati katika shule zetu.
Wanafuzi wasingekaa chini kwa asilimia fulani:-
View attachment 340048
View attachment 340050
Serikali wangetafakari gharama za ukimbizaji wa huu mwenge na wangeamua kubana matumizi haya yasiyo na lazima, HOSPITALI ZETU ZINGEKUWA NA HUDUMA BORA ZAIDI KULIKO SASA. WAGONJWA WASINGELALA MZUNGFU WA NNE:
View attachment 340051
View attachment 340052
Endapo kama serikali wangetafakari gharama na kubana matumizi katika ukimbizaji wa huu mwenge,
TUNGEBORESHA BARABARA NA PIA KUEPUKA MAFURIKO:-
View attachment 340053
Endapo kama serikali wangefafakari gharama za ukimbizaji mwenge na kubana haya matumizi yote;
MAISHA YA WATANZANIA VIJIJINI NA PIA MIJINI YANGEBORESHWA:-
View attachment 340055
Endapo kama serikali wangetafakari na kubana matumizi haya yasiyo na lazima:
HUDUMA ZA JAMII IKIWEMO MAJI MAFI NA SALAMA ZINGEPATIKANA KWA WANANCHI WOTE MIJINI NA VIJIJINI. UWEZO HUO TUNAO:-
View attachment 340056
View attachment 340057
SERIKALI ITAFAKARI, ICHUE HATUA........................
MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
Ahsante mkuu suali zuri...Samahani hivi Kenya kuna mwenge? Kama hakuna kwanini wametupita maendeleo