Makampuni mengine 58 yatoa gawio Serikalini

elivina shambuni

JF-Expert Member
May 31, 2018
461
295
1576163370957.png


Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt Philipo Mpango leo amepokea gawio na ziada nyingine kwa Makampuni 58 ambayo yalikuwa hayajatoa gawio kwa serikali ambapo Rais Magufuli alitoa siku sitini (60) wawe wametoa gawio.

Pia Waziri Mpango ameagiza Makampuni na taasisi ambazo bado hazijatoa gawio la serikali ifikapo January 23 mwakani bodi na Wakurugenzi wa Kampuni na taasisi hizo ambazo zitakuwa hazijatoa gawio bado na Wakurugenzi watakiwa wamejifuta wenyewe.

Akizungumza wakati wa gawio hilo leo Jijini Dodoma, Waziri Mpango amesema tayari mpaka sasa makampuni 58 yametoa gawio la jumla ya shilingi za kitanzania bilioni 12.12, ambazo awali hazikutoa gawio hilo.

"Kiukweli siku ya leo ninafuraha Sana kwa sababu, kutoa gawio ndio kunafanya nchi iweze kujitegemea, na Leo nimepokea gawio kwa makampuni 11 lakini kiujumla makampuni ambayo yameleta gawio ambao Awali hawakuleta ni 58, ambao jumla wametoa Bilioni 12.12" amesema Dkt Mpango.

Aidha ameyataka makampuni na taasisi zote ambazo serikali imewekeza na bado hawajatoa gawio la Serikali hadi ifikapo January 23 mwakani wawe wametoa na ambao watakuwa bado bodi zake na Wakurugenzi wake watakuwa wamejiondoa rasmi kwenye nafasi zao.

Amesema serikali imewekeza katika makampuni hayo ili ipate faida na lengo likiwa ni kuondoa utegemezi wa serikali kwa Mataifa ya nje ambayo yamekuwa yakiweka masharti magumu lakini njia pekee ni kuwekeza katika makampuni na taasisi ili kuweza kujitegemea na sio kutegemea misaada ya nje.

"Sio vizuri kuona Waziri wenu kila siku naenda kukinga bakuli huko nje, huko nje niende kukopa na ninapokopa niwe na uhakika wa kulipa madeni hayo lakini Kama tutakuwa hatutoi magawio kwa serikali tutaendelea kwenda kuomba misaada nje ya nchi" amesema.

Amewahakikishia watanzania kuwa fedha hizo zitatumika vizuri ili kuleta matokeo chanya kwa wananchi na miradi hiyo mnayoiona sio hiyo tu serikali italeta miradi mikubwa zaidi ili kuleta tija kwa watanzania.

Kwa upande wake Msajili wa Hazina, Athumani Mbuttuka, amesema awali ni Makampuni 79 tu ndio waliotoa gawio kwa serikali, na baada ya maagizo ya Rais Kuna makampuni yamekuwa yakitoa gawio na mpaka Leo makampuni na taasisi hizo zinafikia 58, na kutoa jumla ya shilingi bilioni 12.12.
 

Attachments

  • 1576156790246.png
    1576156790246.png
    89.3 KB · Views: 1
Na hivi kalibuni tutashuhudia shule za Msingi zikitoa Gawio,na muda huohuo wakiomba kujengewa mashimo ya choo na madawati.
 
Nchi inachanja mbunga kwenda uchumi wa kati

Wapinzani wakija kushituka watakuwa wamechelewa sana
 
Samahani Ndg. zangu kwa uelewa wangu mdogo labda ni kwa uchache wa elimu niliojaaliwa, ila kwa mtazamo wangu VETA kutoa gawio kwa Serikali ni upopoma ulio pitiliza Katika kujipendekeza.

Nasema hivyo kwa sababu ninavyojua mimi ni kuwa VETA ni miongoni mwa taasisi chache za Serikali katika sector ya elimu zilizo pewa upendeleo kwa kupata fedha moja kwa moja kutoka Katika chanzo kikuu cha mapato ya Serikali ambacho ni kodi za wananchi kupitia TRA.

Lengo likiwa ni kukuza sector ya elimu ya kujitegemea na kutengeneza daraja kwa vijana walio kosa fursa za kuendelea na elimu ya kawaida

Sasa unaporudisha gawio serikalini kutokana na kile unachoona ni surplus ya mapato yako ambayo umepata kutoka katika mfereji wa mapato ya moja kwa moja kutoka Serikalini maana yake ni nini??? Basi bora wafute SDL isiwepo tujue moja

Tunasahau kuwa leo TRA inatumia resources za serekali Kuu kukusanya pesa kwa niaba ya VETA halafu kesho eti unatoa gawio Kurdisha Serikali Kuu huu si ni kama mchezo wa pata potea hii imekaaje jamani???

Hivi ni kwa kiwango gani cha elimu ya VETA kimekua kikubwa kiasi cha kutosheka na kurudisha pesa serikali kuu??? vifaa vyenyewe vya kufundishia ni majanga acheni hizo bana mnatuzingua sasa.

Kwa nini leo taasisi za elimu hawalipi SDL kwa wafanyakazi wanaoajiriwa na taasisi hizo??? Jamani mbona kama tunazidi kujipendekeza mpaka inafikia mahali unatoa gawio mfuko wa Kulia na kujiwekea mfuko wa kushoto ili iweje ???

Kujipendekeza kwa sataili hizi jamani kumezidi sana, inafikia mahali tunasahau mpaka dhamira za uhai wa taasisi zetu kwa kumfurahisha bwana yule, huku Sasa ni kuumizana

Haya tena nyinyi ndio mlioshika mpini si wachoma mahindi wacha tuwapigie makofi kwa upuuzi huu hakika huu ni upuuzi uliopitiliza

Mnyanyembe wa Mboka
Karibuni Mahindi ya kuchoma
Stendi Kuu Unyanyembeee!!!


20191212_175640.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wenye uelewa waje saidia kutoa maelezo kuhusu gawio kwa mashirika ,taasisi na kampuni ambazo serikali imewekeza maana ni mkanganyiko tu
 
Samahani Ndg. zangu kwa uelewa wangu mdogo labda ni kwa uchache wa elimu niliojaaliwa, ila kwa mtazamo wangu VETA kutoa gawio kwa Serikali ni upopoma ulio pitiliza Katika kujipendekeza.

Nasema hivyo kwa sababu ninavyojua mimi ni kuwa VETA ni miongoni mwa taasisi chache za Serikali katika sector ya elimu zilizo pewa upendeleo kwa kupata fedha moja kwa moja kutoka Katika chanzo kikuu cha mapato ya Serikali ambacho ni kodi za wananchi kupitia TRA.

Lengo likiwa ni kukuza sector ya elimu ya kujitegemea na kutengeneza daraja kwa vijana walio kosa fursa za kuendelea na elimu ya kawaida

Sasa unaporudisha gawio serikalini kutokana na kile unachoona ni surplus ya mapato yako ambayo umepata kutoka katika mfereji wa mapato ya moja kwa moja kutoka Serikalini maana yake ni nini??? Basi bora wafute SDL isiwepo tujue moja

Tunasahau kuwa leo TRA inatumia resources za serekali Kuu kukusanya pesa kwa niaba ya VETA halafu kesho eti unatoa gawio Kurdisha Serikali Kuu huu si ni kama mchezo wa pata potea hii imekaaje jamani???

Hivi ni kwa kiwango gani cha elimu ya VETA kimekua kikubwa kiasi cha kutosheka na kurudisha pesa serikali kuu??? vifaa vyenyewe vya kufundishia ni majanga acheni hizo bana mnatuzingua sasa.

Kwa nini leo taasisi za elimu hawalipi SDL kwa wafanyakazi wanaoajiriwa na taasisi hizo??? Jamani mbona kama tunazidi kujipendekeza mpaka inafikia mahali unatoa gawio mfuko wa Kulia na kujiwekea mfuko wa kushoto ili iweje ???

Kujipendekeza kwa sataili hizi jamani kumezidi sana, inafikia mahali tunasahau mpaka dhamira za uhai wa taasisi zetu kwa kumfurahisha bwana yule, huku Sasa ni kuumizana

Haya tena nyinyi ndio mlioshika mpini si wachoma mahindi wacha tuwapigie makofi kwa upuuzi huu hakika huu ni upuuzi uliopitiliza

Mnyanyembe wa Mboka
Karibuni Mahindi ya kuchoma
Stendi Kuu Unyanyembeee!!!


View attachment 1289935

Sent using Jamii Forums mobile app
Bila samahani ndugu yangu, Ni kwamba nijuavyo Mimi VETA wanashughuli nyingi za kuwaongezea kipato zitokanazo na huduma ya kufundisha na Miradi mingineyo, Mfano. Kozi fupi, Mafunzo ya Udereva na pia wanatoa huduma za ushauri wa kitaalamu kuhusiana na masuala ya Ufundi, Hivyo sasa akikusanya mapato yake yote na Kisha akatoa gharama zote za uendeshaji uwezekano wa ziada huenda ukapatikana. Tofautisha VETA na shule za sekondari na Msingi ambazo hazina vyanzo zaidi vya mapato.
 
Back
Top Bottom