Amuagiza Mkurugenzi kubadilisha safu yake mara moja.
Aonya watu waache upigaji wawe waadilifu.
Marketing Department yakosolewa. Awataka ambao hawawezi kuendana na kasi inayotakiwa wakae pembeni.
Asema wafanyakazi wa serikali watumie ATCL kusafiri Posta na TTCL zijiandae.
My take..
Kwakweli Marketing Department ya ATCL ni mbovu sana, namuunga mkono. Nenda twitter account yao au hata website yao. Dah! Inasikitisha.
----------------------------------------------------------
Zanzibar ASP Ameongezea maoni yake hapo chini...
Tatizo la ATCL ni kubwa sana kuliko vile watu wanavyodhania.Ni shirika lililoanzishwa kisiasa, Linafanya kazi kisiasa, Lilikufa kisiasa na sasa linafufuliwa kisiasa. Siasa na Biashara ni kama Maji na Mafuta, huwa haviendani kabisa.Yaani, Waziri Mzima anasema, uwekwe utaratibu ili wafanyakazi wa serikali wanaposafiri kwa Ndege basi Walazimishwe kupanda ndege za ATCL pekee!! Sijui kama waziri anajua athari za kauli yake kwa makampuni mengine ya ndege, Ubora wa Huduma za ATCL, Wajibu wa mfanyakazi wa serikali nk.Sijawahi kuona siasa ikifanikisha biashara.Ni suala la muda tu, ATCL itakufa tena, na tutaendelea kumsaka mchawi milele.... Anayeiloga ATCL ni serikali yenyewe.
Chanzo: TBC 1